Ajali Tanzania: Mawazo mbadala kuhusu udhibiti wa ajali Tanzania

Ajali Tanzania: Mawazo mbadala kuhusu udhibiti wa ajali Tanzania

Habari za mapumziko ya wiki wapendwa!

Kabla ya yote natanguliza pole kwa ndugu na jamaa wote wenye simanzi na majonzi ndani ya mioyo yenu kutokana na misiba mbalimbali iliyowahi kuwakumba, Yaliyopita yamepita lakini hapa naomba sasa tujadili ili kuepuka kama si kupunguza misiba hii kabisa.

Kutokana na aina ya wasomaji, nalazimika kuandika makala hii kwa ufupi sana kama ifuatavyo;kwanza pitia maana ya maneno haya kabla;

AJALI ni tukio lolote la ghafla linalotekea na kuumiza vitu au watu;

HATARI/HAZARD ni ile hali ya kwama kuna tukio au ajali itatokea.

KIWANGO CHA HATARI/RISK ni ule uwezekano uwe mkubwa au mdogo wa kwamba kuna tukio la hatari litatokea.

HATARI YA KITU AU JAMBO/DANGEROUS ni ile hali ya kitu au jambo kusababisha /kuleta maumivu au ajali.

Ebu pitia mfano huu; Wanakijiji wa MBONDORE wanaishi karibu na ghala la mabomu yaliyo isha mda wake . (wanakiji wa mbondore wapo kwenye RISK) (Mabomu kuisha mda wake ni DANGEROUS) (Mabomu yakilipuka ni AJALI itayoleta HAZARD kwa wananchi)

AJALI NYINGI TANZANIA NI ZA KIZEMBE ASILIMIA 98%

Naomba kuanza kwa kusema waafrika wengi hasa watanzania tuko bize sana kushughulika na ajali na si vyanzo vyake, Hatujishugulishi kutatua tatizo kabla ya ajali hata kama tupo katika hali ya hatari, mara nyingi ajali inapotokea Hujifariji kwa kauli “AJALI HAINA KINGA” hii kauli mimi huwa naiona waliyo ibuni walikuwa wazembe kabisa na siipendi kabisa na wanangu nawafundisha kuichukia kauli kwa nguvu zote, Kwakuwa karibu ajali zote 98% huwa zina chanzo chake, kwanini tusijikite kuwa makini na vyanzo vinavyoleta ajali? Hivi mtu anaendesha gari hana leseni, kalewa na anatembea speed kubwa hadi dash bod inapitisha jeneza, Sasa hapo ajali ikitokea tuseme HAINA KINGA? MABASI yanatembea speed kubwa kwenye barabara mbovu halafu tunasema AJALI HAINA KINGA? Hivi kweli kabisa kabisa haina kinga? Mi nakataa kabisa kauli za kizembe kama hizi na ningekuwa na mamlaka ningeifuta kwenye orodha ya Kiswahili.

MAPENDEKEZO

Watu wengi tumeishauli serikali namna ya kupunguza ajali barabarani, labda huenda wengine ujumbe hawakuupata kutokana na changamoto mbalimbali- naomba serikali iandae warsha hata ya kiushindani, PROJECT itakayo onekana nzuri kunusuru AJALI za barabarani mwenye project apewe MOTISHA kama si pesa basi hata Kuipa jina lake tu wakati serikali inapoitekeleza ibaweza kuwa kama Motisha.

Halafu kuna viongozi wanajisahau kabisa katika hili na kuona kama AJALI haziwahusu;

Lakini ukiangalia Viongozi wengi sana wamekufa katika AJALI mbalimbali za barabarani, lakini naomba waelewe kwamba MWENYE AKILI HUWEZI UKAWA SALAMA KUENDESHA GARI LAKO KWENYE BARABARA MBOVU INAYOTUMIWA PAMOJA NA WAJINGA WENYE LESENI ZA KUGUSHI .

Watanzania tubadilike, tusikimbilie kuandika koment nyingi zenye neno R.I.P na mapenzi, Twaweza jadili kwa wingi pia ni namna gani ajali hizi tutaziepuka AHSANTE!

…ACCIDENTS IS AVOIDABLE WHEN THE SITUATION IS ALARMING…
 
  • Thanks
Reactions: y-n
58mins ago, na nimekuwa mtu wa kwanza kureply. Aisee kweli watu hatujui vitu muhimu vya kujadili. Laiti kama ungekuwa umeandika kuhusu mambo ya mapenzi nk ungekuwa umepata replies nyingi Kwa mda huu mchache.
Umeongea ukweli sana. Hili suala la ajali huwa linanichukiza sana na mbaya zaidi vile jinsi watu walivyolala kulishughulikia. Yani sio viongozi sio raia wote tunaliangalia hili suala km vile halituhusu wakati linatugusa wote moja Kwa moja. Ina bore sana
 
Hili somo ni gumu sana ndugu yangu kueleweka, Mimi napenda kuongea kwa mifano. Mfano wangu wa leo ni ajali iliyotokea morogoro dakawa kwa siku ya jana ambayo imegharimu maisha ya watu 11!!
Kwa taarifa wanasema ajali ya kwanza ilitokea saa 12 jioni na kusababisha vifo vya watu watano (5) baada ya malori mawili kugongana na kuungua. Mimi kwa uelewa wangu nilitegemea kwa polisi ambao walifika kwenye eneo la ajali wangekuwa na weledi wa kuweka ishara za kutosha kuashiria ajali! Cha kushangaza ajali ilitokea na polisi kuja na hawakujua umuhimu wa kuweka ishara za tahadhari!! Hadi saa nane usiku inakuja kutokea ajali nyingine inayoyagonga magari haya yaliyopata ajali na kuua watu 6 papo hapo!! Jamani hivi jeshi la polisi lina askari wenye weledi? Hivi vifo sita havikupaswa kutokea!! 8 hours watu hawajaweke warning to an accident scene?? Hata wangetumia njia ya asili ya kuweka majani?? Jamani hawa polisi waliofika eneo la ajali ya kwanza wahojiwe kwa negligence na ikibidi wachukuliwe hatua ili iwe fundisho kwa makosa ya wazi!! Ndio nasema we need training from above from law enforcers!!
 
  • Thanks
Reactions: y-n
Amen nawaambieni,jmbo kubwa linaloweza kumaliza ajali Tanzani sio warsha wala makongamano wala speed governor,kitu kikubwa cha msingi na naomba nirudie tena cha msingi ni :kuwapima madreva urevi,pia pawe na kipimo cha kupima watumiaji wa mdawa ya kulevya kama bhangi ,ugoro nk kama kigezo kabla ya kutoa leseni.Madreva wengi wa masafa kable ya kuendesha magari wanapata kitu ya Arusha na viroba kadhaa,tutawalaumu sana lakini wanapokuwa barabarani akili inakuwa sio yao kabisa na wanakuwa so reckless.
Mimi ni dreva kuna wakati unapishana na mtu unajiuliza mara mbilimbili kama akili zinamtosha au la.
 
Serikali ije na sheria inayolitaka jeshi la polisi kwa kushirikiana na wamiliki wa mabasi kuajiri traffic na askali wanaosindikiza mabasi yote yaendayo mikoani. Hii itasaidia sana kupunguza ajali zitokanazo na uzembe na mizaha kama ilivyotokea kwa city boys.

Kwanza askali wa barabarani watakuwa namerahisishiwa kazi ya kusimamisha mabasi bila sababu za msingi. Pili madereva watendesha gari kwa kuzingatia taaluma yao. Tatu Abiria watajihisi wako salama muda wote. Nne itakuwa rahisi kugundua magendo yanayofanyika huko barabarani. Tano itarahisisha kuchukua hatua sitahiki kwa makosa yatokanayo na uzembe barabarani, kwa dereva abiria na askali wenyewe wasindikizaji. Sita tutakuwa tumepunguza rushwa za barabarani.

Mwisho Askali hawa lazama wapewe mafunzo maalumu na wawe committed kwa kazi yao, walipwe pesa ya kutosha na ili wasinunuliwe wawapo kwenye chombo. Wajibu wa abiria ni kuripoti mienendo ya Askali ndani ya gari mwisho wa safari na wajibu wa Askali itakuwa kuripoti usalama wa abiria na gari kila wanapofika standi kuu kwa mkuu wa usalama barabarani wa mkoa
 
Nimeandika uzi huu kwenye jukwaa la siasa ili wanasiasa wengi wausome na kuchukua hatua. Ni jambo la kawaida sasa kwa ajali za mabasi ya abiria kutokea kila mwezi nchini mwetu.

Mimi ni mmojawapo wa waathirika wakubwa wa ajali zinazousisha mabasi ya abiria. Ni ukweli usiopingika kuwa ajali nyingi zinasababishwa na uzembe madereva. Taifa linazidi kupoteza mamia ya watu na watu wengi kupata vilema vya maisha.

Asilimia kubwa ya madereva wa mabasi ya abiria hawana elimu ya kutosha au hawana elimu kabisa, wengine ni walevi kupindukia na wavuta bangi. Ni wakati muafaka kwa serekali kuufanya udereva wa mabasi na hata malori kuwa taaluma yenye hadhi yake ili tupate professional drivers watakaojali maisha yetu. Pia, serekali iwabane wenye mabasi na malori wawalipe vizuri madereva wao.

Nawaomba mlio karibu na Waziri wetu wa mambo ya ndani mhe. Mwigulu Nchemba na Rais wetu mhe. Dr. John Magufuli muwafikishie haya maoni yangu na mengine yatakayochangiwa na wadau.
 
thread kama hii inakosa support? nimekuelewa ila wafanye wilaya moja hadi nyingine askari anabadilishwa hasa kwa safari ndefu,
 
abiria na sisi tunachangia sn ajali,huwa tunakaa kimya tu,hata akijitokeza mmoja kumuonya dereva utashangaa wengi wanakua upande wa dereva,tusipobadilika na sisi tutazidi kuangamia siku zote.
 
Serikali ije na sheria inayolitaka jeshi la polisi kwa kushirikiana na wamiliki wa mabasi kuajiri traffic na askali wanaosindikiza mabasi yote yaendayo mikoani. Hii itasaidia sana kupunguza ajali zitokanazo na uzembe na mizaha kama ilivyotokea kwa city boys.

Kwanza askali wa barabarani watakuwa namerahisishiwa kazi ya kusimamisha mabasi bila sababu za msingi. Pili madereva watendesha gari kwa kuzingatia taaluma yao. Tatu Abiria watajihisi wako salama muda wote. Nne itakuwa rahisi kugundua magendo yanayofanyika huko barabarani. Tano itarahisisha kuchukua hatua sitahiki kwa makosa yatokanayo na uzembe barabarani, kwa dereva abiria na askali wenyewe wasindikizaji. Sita tutakuwa tumepunguza rushwa za barabarani.

Mwisho Askali hawa lazama wapewe mafunzo maalumu na wawe committed kwa kazi yao, walipwe pesa ya kutosha na ili wasinunuliwe wawapo kwenye chombo. Wajibu wa abiria ni kuripoti mienendo ya Askali ndani ya gari mwisho wa safari na wajibu wa Askali itakuwa kuripoti usalama wa abiria na gari kila wanapofika standi kuu kwa mkuu wa usalama barabarani wa mkoa
kwani hayo mabasi yanabeba mbuzi mpaka yasindikizwe!? Wanaopanda humo ni ni watu na akili zao na jeshi la polisi na SUMATRA wanatoa maelezo kila wakati toeni taarifa kama unaona mambo yanayofanywa na dereva safarini sio ya kawaida, matrafiki siku hizi wako wengi sana barabarani na wametoa namba za mawasiliano, hamtaki kuwasiliana nao mnataka msindikizwe na askari kwenye mabasi kuwa control madereva!
 
kwani hayo mabasi yanabeba mbuzi mpaka yasindikizwe!? Wanaopanda humo ni ni watu na akili zao na jeshi la polisi na SUMATRA wanatoa maelezo kila wakati toeni taarifa kama unaona mambo yanayofanywa na dereva safarini sio ya kawaida, matrafiki siku hizi wako wengi sana barabarani na wametoa namba za mawasiliano, hamtaki kuwasiliana nao mnataka msindikizwe na askari kwenye mabasi kuwa control madereva!
Mara nyingi kinacho washinda abiria kutoa taarifa ni suala la usalama wao. Ukiwa ndani ya gari ni vigumu kumpigia trafiki simu ukizingatia wapo wengi watakao kupinga wakiona kama unawakwaza na wengine watakutishia kukushusha njiani.

Mawasiliano ya abiria na askali wakati mwingine yanahitaji privacy ili kutoa taarifa sahihi itakayo mtia dereva hatiani na sio taarifa za kishabiki na mihemko ndani ya gari. Mara nyingi dereva na konda huwa na watu wao ndani ya gari wanaoandaliwa kupinga na kukutukana ikiwa umeona jambo si zuri safaraini na kwa vile unajua wote ni abiria utahisi wewe ndio hujui

Matrafiki wengi wameshazoeana na madereva barabarani na wanaposimamisha gari huingia ndani kama namna ya kuwaridhisha tu abiria kuwa wapo kazini hutaona hatua yeyote inayochukuliwa hata kama uliripoti uzembe. Chukulia mfano, mzaha uliotokea city boys unakiri ungemwambia trafiki wa kituo cha mbele angeamini? Abiria gani angekubali kupoteza muda kisa unamshawishi askali mzaha unaofanya na dereva? Askali na abiria wengi hukumbuka wajibu wao baada ya ajali kutokea.
 
Habari enyi wapendwa!

"Uchungu wa msiba usikie kwa jirani tu"

Kabla ya yote natanguliza pole kwa ndugu na jamaa wote wenye simanzi na majonzi ndani ya mioyo yao kutokana na misiba mbalimbali iliyowahi kuwakumba, Yaliyopita yamepita lakini hapa naomba sasa tujadili ili kuepuka kama si kupunguza misiba hii kabisa.

Ni rahisi sana kwa mtu Mtanzania asiyejali akutapo msiba au ajali Apite pembeni pasipo hata kuuliza msiba upoje. (Hakuna msiba usiofunza jambo)

Watanzania tubadilike, tusikimbilie kuandika koment nyingi zenye neno PUMZIKA KWA AMANI NA R.I.P na hoja za mapenzi kwa wingi, Twaweza jadili kwa wingi pia usalama wetu na ni namna gani ajali hizi tutaziepuka AHSANTE!

…ACCIDENTS ARE AVOIDABLE WHEN THE SITUATION IS ALARMING…

TAFAKARI (yawezekana kabisa Mtu aliyebuni kuwepo kwa SAFETY BELT, Alipata wazo hilo baada ya kuona ajali na akagundua Umhimu wa kufunga mkanda" wiki iliyopita niliandika makala hii;
UJINGA WETU TANZANIA NA AJALI HIZI ZA KIZEMBE, TUJIPANGE KUZITOKOMEZA

Kutokana na aina ya wasomaji, nililazimika kuandika makala hii kwa ufupi sana kama ifuatavyo;kwanza pitia maana ya maneno haya kabla;


AJALI ni tukio lolote la ghafla linalotekea na kuumiza vitu au watu;

HATARI/HAZARD ni ile hali ya kwamba kuna tukio au ajali itatokea.

KIWANGO CHA HATARI/RISK ni ule uwezekano uwe mkubwa au mdogo wa kwamba kuna tukio la hatari litatokea.

HATARI YA KITU AU JAMBO/DANGEROUS ni ile hali ya kitu au jambo kusababisha /kuleta maumivu au ajali.

Ebu pitia mifano hii;
1. Wanakijiji wa MBONDORE wanaishi karibu na ghala la mabomu yaliyo isha mda wake . (wanakiji wa mbondore wapo kwenye RISK) (Mabomu kuisha mda wake ni DANGEROUS) (Mabomu yakilipuka ni AJALI itayoleta HAZARD kwa wananchi).

2. Roli bovu lililo simama Msituni pembezoni mwa barabara bila tahadhari, Limegongwa na bus kwakuwa dreva wa roli aliliwa na Simba punde kabla ajali. (Gari bovu ni DANGEROUS, Kusimama Msituni ni RISKY, roli kupaki na Bus kuendeshwa bilaTahadhari ni HAZARD,Dreva wa roli kuliwa na simba na Bus kugonga roli ni AJALI.


AJALI NYINGI TANZANIA NI ZA KIZEMBE ASILIMIA 98%

Naomba kuanza kwa kusema waafrika wengi hasa watanzania tuko bize sana kushughulika na ajali na si vyanzo vyake, TUJAFANYA KAMA ZIMA MOTO TU Hatujishugulishi kutatua tatizo kabla ya ajali hata kama tupo katika hali ya hatari, mara nyingi ajali inapotokea Hujifariji kwa kauli “AJALI HAINA KINGA” hii kauli mimi huwa naiona waliyo ibuni walikuwa wazembe kabisa na Huwa siipendi kabisa na wanangu nawafundisha kuichukia kauli hiyo kwa nguvu zote, Kwakuwa karibu ajali zote 98% huwa zina chanzo chake, kwanini tusijikite kuwa makini na vyanzo vinavyoleta ajali?

Mfano wa ajali zilizo tokea majuzi morogoro na Singida:
AJALI za juzi; Bila kuwa na chembe ya kumumunya maneno; zile ajali zote zinathibitisha uzembe wa hali ya juu kabisa kuanzia kwa MADREVA, TRAFFIKI NA ABIRIA; Ajali zile zimetoa taswira na kuthibitisha tu uzembe wa nyuma.

SERIKALI INAMAKUSUDI GANI?
Kwakweli naomba mamlaka husika zichue hatua za kudumu kunusuru haya matatizo, Nashauri wasitegemee TOCHI za bararani pekee, Yamkini Tochi zikawa chanzo cha ajali zinapotumiwa kama mradi, wakumbuke madreva wanapeana taarifa kwahiyo pale panapostahili hutembea zaidi, na kufanya tochi kuwa kama matuta ya barabarani yalivyo, Wafikilie Kuweka control ya kudumu, yaweza ikawa kwenye mafunzo ya udereva, mikataba ya ajira,uchakavu wa magari na rushwa kwa askari wetu.

NINI KIFANYIKE?
Kuna mambo mengi sana, lakini yanahitaji wataalamu wakae na kujadili, twaweza weka hata sheria za kulazimisha GPS Monitoring kwa mabasi yote Au wanaweza boresha kukawa na mfumo wa log book Bus transportation-Yaani kila kituo kuwepo mda maalum wa kufika kwa kila basi, sheria kali ziwekwe kwa dreva yeyote atakaye kamatwa na kosa la ulevi au kuvunja sheria n.k

Hivi mtu anaendesha gari hana leseni, kalewa na anatembea speed kubwa hadi dash bod inapitisha jeneza, Sasa hapo ajali ikitokea tuseme HAINA KINGA? MABASI yanatembea speed kubwa kwenye barabara mbovu halafu tunasema AJALI HAINA KINGA? Hivi kweli kabisa kabisa haina kinga? Mi nakataa kabisa kauli za kizembe kama hizi na ningekuwa na mamlaka ningeifuta kauli hii kwenye orodha ya Kiswahili.


MAPENDEKEZO
Usafili wa Tanzania kwakweli siyo wa uhakika kabisa kwa asilimia kubwa, Ni vyema japo bunge walau mara moja moja likajadili mambo haya, Matokeo ya ajali tanzania ni makubwa sana ukilinganisha na inchi za wenzetu walivyo.
Watu wengi tumeishauli serikali namna ya kupunguza ajali barabarani, labda huenda wengine ujumbe hawakuupata kutokana na changamoto mbalimbali- naomba serikali iandae warsha hata ya kiushindani, Mtu au Taasisi itakayo andaa PROJECT itakayo onekana nzuri kunusuru AJALI za barabarani mwenye project apewe MOTISHA kama si pesa basi hata Ile project ipewe jina lake tu wakati serikali inapoitekeleza itaweza kuwa kama Motisha kwao.
VIONGOZI WANAFANYA NINI?
Kuna viongozi wanajisahau kabisa katika hili na kuona kama AJALI haziwahusu;
Lakini ukiangalia Viongozi wengi sana wamekufa katika AJALI mbalimbali za barabarani, lakini naomba waelewe kwamba MWENYE AKILI HUWEZI UKAWA SALAMA KUENDESHA GARI LAKO KWENYE BARABARA MBOVUINAYOTUMIWA PAMOJA NA WAJINGA WENYE LESENI ZA KUGUSHI

karibuni!.
 
Ajari aina kinga
Sio kweli kwamba ajali haina kinga kinga unayo wewe abiria na dereva wako. Huwezi ona shimo mbele ya barabara na kwa vile umezoea kupita hapo siku zote bila shimo hilo kuwepo ukadharau kwa kuhisi umeona vibaya ukaamua tu upite. Mazoea waliokuwa nayo City boys ni mfano tosha kuthibitisha hili.
 
Uzembe kwa kiasi kikubwa unaweza ukadhibitiwa na abiria.. Kwa mfano overtaking kwenye eneo la hatar, michezo ya madereva, mwendokasi, hivi vyote hakuna askari wala mfanyakazi wa sumatra wala mtu wa mamlaka nyingine yeyote ile anaweza kuviona ila ni abiria.. Abiria tupo kimya na tunafumbia macho haya mambo.. Binafsi nawalaumu sana abiria.. Je watu ambao walishawah kuona michezo kama hiyo ya kubadilishana njia walishawahi kutoa taarifa..? Mpaka gar inapigwa tochi speed 122 je humo ndan hakuna abiria??? Ni upuuz wa sisi wasafir ukijumlisha na dereva... Sio suala la kublame serikali.. Serikali itahusika pale tu patakapokua na ubovu wa miundombinu kwa mfano mashimo barabarani.. Huo ndo mtazamo wangu
"Msiba usikie kwa jirani" co JILANI
 
Back
Top Bottom