Ajali Tanzania: Mawazo mbadala kuhusu udhibiti wa ajali Tanzania

Ajali Tanzania: Mawazo mbadala kuhusu udhibiti wa ajali Tanzania

Ndugu zangu wa jf naomba nirudie mchango ule ule nilotoa kwa post nyngine kwa herufi kubwa "CHANZO CHA AJALI ZA KIZEMBE NA ZA KIPUUZ NI KINATOKANA NA UPUUZ WA SISI ABIRIA UKIJUMLISHA KIDOGO NA DEREVA... NIANZIE KWA ABIRIA.. KAMA WACHANGIAJ NI WASAFIR MTAONA KILA BASI LINA NAMBA ZA VITUO /WAKUU WA MIKOA WA ASKAR WA USALAMA BARABARANI-RTO , JE NI WANGAPI TUMESHAWAH KURIPOTI UZEMBE WA MADEREVA?? HAKUNA AFISA WA SUMATRA,TRAFIK ,RSA AU AFISA YOYOTE WA SERIKALI ANAEONA UZEMBE UNAOFANYIKA BARABARANI KAMA SIO SISI ABIRIA.. SISI ABIRIA TUMEKUA HATUONGEI WALA HATUPAZI SAUTI ZETU KUKEMEA.. KAMA DEREVA ANAOVERTAKE KWENYE ENEO LA HATARI NI WAJIBU ABRIA KUMWAMBIA NA IKIWEZEKANA KUMKARIPIA, JE MNAFANYA IVO??? KWA MFANO AJAL YA JUZ YA CITY BOY NDO NIMESKIA WATU WANASEMA ETI NDO KAWAIDA YAKO KUSALIMIANA IVO, JE KUNA HATA ABIRIA ALIEWAHI KUTOA RIPOTI??? MPAKA DEREVA ANAPIGWA TOCHI YUPO SPEED 122 KM/H JE HAKUKUWA NA ABIRIA HUMO NDAN YA BASI?? AU NDO TUNAJIFANYAGA TUNA HARAKA NA KUSHANGILIA MWENDOKASI ILA LIKITOKE LA KUTOKEA MZEMBE NI DEREVA???? ABIRIA TUSIWE WA KULALAMIKA TU... TUPAZE SAUTI KUKEMEA TUWAPO NDANI YA MABASI. MFANO NILIWAH KUPANDA SIMBA MTOTO KUELEKEA TANGA YAN HUYO DEREVA ALIKUA ANATEMBEA MWENDO CJAPATA KUONA YAN MPAKA KUNA MUDA UNASKIA KAMA MKOJO UNAKUTOKA VILE... CDHAN KAMA NISHAWAH KUPANDA BASI INATEMBEA HUO MWENDO.. ILA TULIMWAMBIA NA AKATUELEWA AKAPUNGUZA... upande wa pili ni uzembe wa madereva KUNA MADEREVA WANAFATA MKUMBI WA ABIRIA. WAKIAMBIWA FUTA KISAHANI BASI MTAJUTA KUZALIWA, NA KWA NN DEREVA ULIESOMEA TAALUMA UPELEKESHWE , DEREVA ENDESHA MWENDO WA WASTANI 80-100KM/H HAO WANAOTAKA 140,KM/H WANGEPANDA FASTJET TU... BADO SIJASUPPORG WAZO LA MTOA MADA.. KIUKWEL WANAWAKE WENYE KUHIMILI MIKIKIMIKIKI YA BARABARA NI WACHACHE SANAAA KUENDESHA BARA BARA KUU NI MTHANI MZITO NDO MANA KUNA MADEREVA WANAUME HAWATAK HATA KIDOGO KUINGIA BARABARA ZA MIKOANI.. KUNA KILA AINA YA USHETANI,UCHAWI NA MABALAA YOTE.. MWANAUME NI MWANAUME TU... hayo ndo maoni yangu. ABIRIA TUACHE UPUUZI
 
Kwa muda mrefu tumekuwa tukipoteza ndugu, jamaa marafiki na maadui zetu kwa ajali za KIZEMBE kama ile ya mabasi ya kampuni ya City Boy.
Imefika wakati wa kusema basi.... maana inawezekana kama ilivyowezekana kwa nchi za wenzetu. Kwa nchi kama Tanzania ajali zinaweza kudhibitiwa kwa matumizi ya nguvu tu.

Nashauri kuanzia sasa ikitokea ajali basi mkuu wa mkoa ilipotokea ajali atumbuliwe yeye pamoja na mkuu wa wilaya, na viongozi wa usalama barabarani wa maeneo husika. Hii itafanya wafanye kazi kwa tahadhari na watahakikisha askari wa usalama barabarani wanawanyoosha madereva wazembe.

Bila kufanya hivi tutaendelea kushuhudia mfululizo wa ajali nyingi sana siku za usoni.

KWANINI NIMESHAURI WAKUU WA MIKOA NA WILAYA WATUMBULIWE? Kwasababu wao ni viongozi wa ulinzi na usalama ktk maeneo yao... Inapotokea ajali na kuua watu wao wanapaswa kujibu nikwanini wameshindwa kuhakikisha usalama wa raia katika maeneo yao ya kazi.
Mheshimiwa Rais ukifanya hivi ajali zakizembe zitatoweka nchini.
 
Hao City Boy nasikia walikua wanafanya madoido, sasa hapo ukimtumbua mtumishi wa umma kwa uzembe kuwa ameshindwa kuzuia ajali itakuwa sahihi kweli!?
 
Hao City Boy nasikia walikua wanafanya madoido, sasa hapo ukimtumbua mtumishi wa umma kwa uzembe kuwa ameshindwa kuzuia ajali itakuwa sahihi kweli!?
Yap....wangekuwa wanatumbuliwa... Madereva wangeisoma namba pia hivyo wasingeleta mchezo. Walikuwa wanacheza kwakuwa hakuna wa kuwabana
 
Jiulize kwanza kwanini ajali zinakuwa nyingi na za kizembe.

Sio suala la wakuu wa mkoa wala wilaya bali ni traffic department ambao ndio wa kubeba mzigo wote huu na dhambi zote ziwe kwao.

Madereva wengi hawajui sheria za barabarani
Dereva wa bus ana jukumu kubwa la kulinda usalama wa abiria na kuwa fully trained kwa kazi hiyo.

Nashauri madereva wote wa mabasi wapelekwe wakasome na kuonyeshwa video za matukio ya ajali kama moja ya training na wapasi kihalali kwa usimamizi wa kweli hakuna bla bla.
Wawe professional drivers na kuwa na licence tofauti pindi wanapopasi na kujua sign post zote.

Pia barabara sign zote ziandikwe kiswahili/English maana wasimamizi wa sheria za barabarani hawalioni kama ni tatizo hilo ajabu sana ni kama nyumba bila choo
 
Wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya wanahusikaje hapo?

Ni ujuha wa hali ya juu na usiomithilika ajali isababishwe na dreva halafu umtumbue mkuu wa mkoa au wilaya ilikotokea ajali na kuwaadhibu matraffic barabarani kwa kosa lisilo lao.Basi kwa kuwa utumbuaji umezoeleka utekelezwe kiwehu wehu hivyo na mchangiaji anajiona ametoa mchango wa maana jukwaani.
Tukirudi kwenye visababishi vya ajali zenyewe ni pamoja na leseni za magari ya abiria kupewa vijana wadogo mno wengine hawajafikisha hata miaka 20 ya umri na mara nyingi huamkia asubuhi kwenye majumba ya starehe na kuja kuendesha bus la safari ndefu.Hawana wajibu wowote kwa maana ya kuwa na mke wala mtoto hivyo hawana hofu yoyote.Anawabwaga na kuua abiria wengi anakimbilia mikoa ya mbali tena wilaya za mipakani.Ni walevi wa kutupa chupa za maji wanazoweka juu ya dashboards ni mchanganyiko wa konyagi na viroba kwa kuwa rangi zake ni nyeupe abiria na maaskari wanafikiri ni maji ya kawaida.Akifika kila kituo anapotea kwa muda ameenda kuvuta bangi akirudi anaongeza na maji ya viroba hivyo kadri anavyoendelea na safari ndivyo atakavyozidi kulewa ukiongezea na joto la engine pale mbele na hatimae uwezo wa kulimudu gari utapotea na ajali kutokea.Miaka ya nyuma kidogo bus la abiria kuanzia taxi na magari ya safari ndefu asingeruhusiwa kijana mdogo hivyo na mara nyingi ungewakuta watu wazima kuanzia miaka 40 na kuendelea kwa maana kuwa huyu ana woga wa familia aliyoiacha nyumbani hivyo asingethubutu kukimbiza bus mwendo mkali na asingelewa akiwa anaendesha.Sasa ushauri wangu kwa raisi wa nchi wapo wanawake wengi wenye uwezo wa kuyaendesha mabus ni kiasi cha kuwapeleka veta na kupata mafunzo na uzoefu.Wao kidogo wana moyo wa huruma na woga pia sio walevi wakiwa kazini.Magari yote ya abiria ya safari ndefu yasiruhusiwe kutembea barabarani baada ya saa 12.30 jioni kuepuka ajali na kutekwa usiku badala yake yaegeshwe katika miji midogo hadi asubuhi saa 12.Usiku traffic hawapo na gari hukimbizwa sana na utekaji na wizi wa fedha na mali za abiria hutokea usiku huo.Ni hatari zaidi inapotokea ajali usiku gari ikarushwa bondeni,kurushwa mbali na barabara au kulalia abiria.Misaada ya usiku ni ya matatizo sana watu kuaminiana hivyo abiria wanaweza kufa kwa kuvuja damu muda mrefu au kukosa msaada na pengine kulaliwa na gari.Abiria katika hili waikubali hali kwani nao mara nyingi humhimiza dereva kukimbiza gari wawahi makwao au biashara zao.Matajiri wa mabus waache kuwaamuru madereva wao kutembeza gari usiku ili asubuhi gari lipakie abiria wengine bila hata matengenezo na usafi.Njia hizi chache zitapunguza sana ajali za mabasi na kufa wananchi ovyo ovyo tu.
 
Nashauri kuanzia sasa ikitokea ajali basi mkuu wa mkoa ilipotokea ajali atumbuliwe yeye pamoja na mkuu wa wilaya, na viongozi wa usalama barabarani wa maeneo husika. Hii itafanya wafanye kazi kwa tahadhari na watahakikisha askari wa usalama barabarani wanawanyoosha madereva wazembe.

Mheshimiwa Rais ukifanya hivi ajali zakizembe zitatoweka nchini.

Kwa jinsi tunavyombebesha Raisi Magufuli majukumu, ni kama hatuhitaji kiongozi mwingine tena, yeye ndie awe one man government - raisi, waziri mkuu, waziri wa wizara, mkuu wa mikoa, mkuu wa wilaya, polisi, askari trafiki, mkusanya kodi, mfagia barabara, mwalimu mkuu wa shule zetu, dereva na konda wa dala dala zetu, mpiga debe, dereva wa boda boda, nk! Hivi ataweza kweli?
 
Kwa iyo JPM atoke magogoni aje barabarani ashike tochi ya speed au awapime akili madereva au arekebishe bara bara mbovu ushauri wako ni wa kipuuzi kuliko upuuzi
 
Wakuu wa mikoa na wilaya ni viongozi wa kamati za ulinzi na usalama katika maeneo yao. Inapotokea ajali wanakuwa wameshindwa kuhakikisha usalama wa raia ktk maeneo yao hivyo wanastahili kutumbuliwa maana wameshindwa kuwasimamia askari wa usalama barabarani....
 
Kwa jinsi tunavyombebesha Raisi Magufuli majukumu, ni kama hatuhitaji kiongozi mwingine tena, yeye ndie awe one man government - raisi, waziri mkuu, waziri wa wizara, mkuu wa mikoa, mkuu wa wilaya, polisi, askari trafiki, mkusanya kodi, mfagia barabara, mwalimu mkuu wa shule zetu, dereva na konda wa dala dala zetu, mpiga debe, dereva wa boda boda, nk! Hivi ataweza kweli?
Ndilo tatizo hilo, kila kitu Rais na ndio maana anajisikia kama anaweza kuwa Mungu. Itafika mahali hata chenji ya mahotelini tutadai rais ahakikishe inarudishwa
 
Kumfukuza mtumishi wa umma kwa kosa la dereva wa basi itakua sio sahihi dawa nikumfungia dereva husika leseni yake kwa angalau miaka isiyopungua sita ili arudi shambani akaendeshe jembe.
 
Jamani tupeni maoni yenu jinsi ya kupunguza ajali za barabarani

Suala hili ni nyeti ambapo ilikuwa ni muhimu kuliangalia mbali zaidi badala ya kufikiria ajali zinahusisha mabasi ya abiria peke yake. Ajali zinahusisha magari na pikipiki ambapo magari yanaweza kuwa magari madogo, binafsi, mabasi, malori nk. Walio wengi wa wana jamii wanaendesha magari na wanao uzoefu wa kutosha barabarani. Tunapotathimini haya ingesaidia sana tunapojiweka katika nafasi za madereva kuona kuwa japo wao haya leo yamewakuta siku nyingine yawezekana kabisa kuwa ni sisi.

Yafuatayo yangeweza kupunguza ajali barabarani kama si kuziondoa kabisa:

1. Kuhakikisha kuna minimum (Secondary) education na pia minimum age kwa madereva wa kada mbali mbali. Mfano dereva wa basi, dereva wa Lorry, dereva wa tiper ya mawe, nk. Udereva unahitaji mtu mwenye uwezo wa kutosha kufanya mawazo sahihi kwa wakati ambapo kinyume chake yawezekana kusababisha upotevu wa maisha ya watu wengine.
2. Kuhakikisha serikali inawajibika kuona kuwa barabara kuu zinafanyiwa matengenezo kwa wakati. Kusiwepo mashimo barabarani katika barabara kuu. Ni kweli kuwa Serikali haiwezi kutengeneza barabara zote kwa wakati lakini barabara kuu hili halina excuse. Kuna barabara Nyakanazi - Benako barabara kuu ielekeayo Burundi, Rwanda, Congo na Uganda. Hali iliyomo katika barabara hii hapana - haikubaliki. Ajali katika kipande hiki ni jambo la kila mara.
3. Malori makubwa yawe na muda maalumu wa kutembea.
4. Kiwango cha mwendo wa kutembea magari uongezwe kufikia 100km/h kwenye highways kulingana na ushauri wa wajenzi (si polisi) na faini ziwe kubwa zaidi iwapo kiwango hicho kikizidishwa. Kwa hakika kiwango cha 80km/h kwenye highways ni kidogo mno na kimsingi haipo gari ya polisi, kiongozi, wala raia yeyote inayotembea kwa speed ya 80km/h katika highway hali hakuna tochi karibu. Wakati 100km/h itasaidia kumfanya psychologically dereva aone kiwango hicho ni muafaka hatakuwa na haja ya kwenda kununua ugomvi usiokuwa na sababu zaidi ya hapo. Serikali ingejaribu hili na (bila ya miye kuwa nabii) isishangae kuwa na matokeo chanya.
5. Kuondoa kero za polisi wa usalama barabarani njiani. Ieleweke wazi wazi mipaka ya askari wa usalama barabarani. Hawa jamaa wana kero nyingi hasa wanapokuwa katika kutafuta rushwa. Ifahamike kuwa uwezo wa kufanya maamuzi wa dereva unachangiwa sana na hali yake ya utulivu kiakili. Sasa unapokuta mtu anakuwa harassed bila sababu yoyote hali ya utulivu wa kiakili baada ya hapo huwezi kuitabiri. Jifikirie hali uliyokuwa nayo baada ya kukerwa na kero za askari wa usalama barabarani ambaye waziwazi alichotaka kwako kilikuwa rushwa. Psychologically tuko tofauti na kila mtu ana matatizo yake. Mtu kaamka asubuhi hayuko na hili wala lile unakutana na solicitor wa rushwa anayeyanya hayo kinyume cha sheria. Feelings za watu ni tofauti.
6.
7.
8.
.
.
100.

Huu uzi ni muhimu ilikuwa ni jambo la heri kuujadili pasipo na mihemuko isiyo na tija. Tuendeshapo magari tujaribu kuangalia 80km/h iko je na kisha tuitafakari kwa gari linalotoka Mwanza hadi Dar au hata Morogoro hadi Dar. Si tunayaona magari ya serikali barabarani? Lipi hata linatembea 120km/h yanaenda hadi 150km/h na hata zaidi.

Tutafakari tujitendee haki sisi wenyewe kabla ya kuwaning'iniza wengine.
 
Wanajamii tumekua tukijadili mambo mengi Jukwaani , mingi ya mijadala husika inagusa masuala ya kusiasa! Binafc naumizwa sana kusikia ajali za barabarani kila kukicha! Ukweli ukiona majeruhi, maiti zitokanazo na ajali zinatisha, majeruhi wanatisha!
Wakati watu wanapoteza maisha kila iitwapo leo, wanasiasa wametuweka busy kujadili siasa tu!
Ni ombi langu leo kuomba Wanajamvi, tujadili nini kifanyike kupunguza ama kuondoa kabisa tatizo la ajali, mjadala wetu uzingatie wadau wote wanaohusika na usafiri wa barabarani tu; Sumatra, Traffic pamoja na abiria! Nini kifanyike ili kuondoa tatizo hili?
Ni imani yangu ajali hizi zinaepukika kila mdau akiwajibika kwa nafasi yake! Karibu!


Ajali za barabarani husababishwa na vitu vikuu vitatu:


1.Barabara 2.Vyombo ya usafiri 3.Watu


1. Barabara zinaweza kupunguza ajali kama zitakuwa zinatengenezwa mara zinapoanza kuharibika(pot holes) na sio kuachwa hadi kugeuka mahandaki. Alama za barabarani ziwepo kila mahali penye risk na hizi alama ziwekwe hata kwenye barabara za vumbi ili kuwafahamisha watumiaji hali ya barabara huko mbele ikiwa ni pamoja na speed wanayopendekeza wataalamu kufuatana na profile ya barabara, milima, kona, miteremko, madaraja, upepo mkali, utelezi, maporomoko nk. Sasa hivi ukitoka Mbezi Mwisho kuelekea Mbezi Beach kupitia Goba barabara ina kona nyingi sana na matuta ila hutakutana na alama yoyote ya barabarani tangu mwanzo hadi mwisho kitu ambacho ni hatari kwa watumiaji wote wa barabara.


2. Wengi wetu hatuna uwezo wa kununua magari mapya(0-mileage) hivyo tunanunua magari yaliyotumika nchi zingine na yanapoingizwa nchini hatujui kama huko lilikotoka liliwahi kupinduka (overturn) au la. Mimi sio mtaalamu ila nasikia gari likipinduka kwenye baadhi ya nchi haliruhusiwi tena kurudi barabarani kwa sababu aerodynamics za gari hiyo zinabadilika na kulifanya lisiwe stable barabarani tena. Gari kama hilo linaishia kutolewa spares tu. Tuache hayo. Ni wajibu wa kila mtumiaji kuhakikisha chombo chake chausafiri kiko salama kila siku kabla ya kukiingiza barabarani kama mtumiaji anathamini maisha yake na ya watumiaji wengine wa barabara. Je wangapi kweli huwa tunakagua vyombo vyetu vya usafiri kila siku kabla ya kuingia barabarani? Walau hata level ya coolant, brake fluid, power-steering fluid level tu? Sijui! Ila pia mamlaka husika za usalama barabarani huwa zina taratibu ya kukagua hali ya usalama wa vyombo vya usafiri wa barabarani (Vehicle road-worthy) angalao mara moja kwa mwaka kwa magari yenye umri wa zaidi ya miaka 3 tangu litoke kiwandani. Kwa nchi yetu naona ni tofauti kabisa. Mamlaka inayohusika na usalama barabarani inauza STICKERs za kuonyesha kuwa gari lako limekaguliwa na linafaa kuwepo barbarani bila kuhatarisha usalama wa wengine!! Kwa wenzetu Road-worthness inakaguliwa na Agencies/makampuni/magereji makubwa yenye viwango vilivyokubalika na kukuarifu mmiliki hali ya usalama wa gari lako, na vitu gani unatakiwa urekebishe/ubadili ili kukuhakikishia usalama wako na wa watumiaji wengine wa barabara. Ni hiari yako kutengenezea hapo hapo au kupeleka gari lako kutengenezea chini ya mwembe mradi uimalize checklist waliyokupatia ya vitu vya kurekebisha/kubadili then unarudi tena kwao kwa verification. Wakiridhika wanakupa barua unakwenda traffic kupewa STICKER ya usalama barabarani. Sasa hapa kwetu Tz sijui wenzangu kama magari yenu yana funuliwa hata hiyo bonet? Mimi sijawahi kukaguliwa pamoja na kuhitaji kukaguliwa gari! Madereva wa malori wa safari ndefu nasikia ndio kabisa hata akimwambia tajiri yake gari lina ubovu anaweza kuambiwa arudishe funguo kama hataki kazi. Kwa hali hii naona kwa upande wa vyombo vya usafiri risk ya ajali ni kubwa sana kwa ajili yaUZEMBE!


3. Watu tunachangia pia katika ajali. Unakuta mtu kanunua gari bila hata kwenda driving school. Then anamtafuta dreva wa kumfundha kwenye "Off-roads" siku nne, then tayari wiki inayofuata yuko peke yake anaendesha kuelekea kwenye shughuli zake! Driving Licence wanajua wanakozipata ila nasikia sio issue. Na watu kama hawa wapo wengi tu. Group lingine ni "incompetent drivers" wanaofundishwa chini ya viwango kutoka kwenye utitiri wa driving schools zilizopo. Kuna driving schools zenye "MAADILI" na kuna zingine wanatengeneza fedha tu. Mke wangu bahati mbaya alisomea kwenye hizo zinazotengeneza fedha tu. Basi alipomaliza akarudi nyumbani na leseni yake "halali" kabisa(zile za zamani kama kakitabu). Sasa nilipoanza kumuuliza vipi vehicle inspector kwenye road test amekupa marks gani na maelezo/maoni gani, ndipo nilipotaka kuzimia! Ananishangaa "vehicle inpector? Road-test? Marks? Ndio vitu gani hivyo?" Duh, anasema wao siku wanaanza masomo ya udereva walipeleka picha na siku ya mwishi wa vipindi waliletewa leseni darasani kila mtu bila hata mtihani wa aina yoyote ile! Anyway nilimwambia wife twende lunch Mlimani City tukitokea Kibaha na aendeshe yeye na tulipofika Kibamba aliegesha gari kwa "hasira" za kukosolewa na mimi na madereva wengine waliokuwa wanatupita kwa jinsi alivyokuwa anayumba njia nzima. Ila nashukuru Mungu alikubali kuwa hiyo kozi ya udereva aliyopitia ni ya kitapeli kabisa, na kukubali kuanza upya tena kozi ya udereva katka chuo cha shirika la elimu kibaha. Baada ya kumaliza hapo waliambiwa watakwenda kufaya mtihani wa road-test na nadharia Kituo cha Oysterbay kwa sababu kibaha walikuwa hawajaanza kutoa leseni mpya zinazotumika sasa. Waliambiwa licence mpya hazina forgeries wala upendeleo na "Competence " yako ndio itapelekea upate leseni. Walikwenda wakiwa sita na walipofika tu askari mmoja wa traffic akawauliza kama wana shida na leseni wakamjibu ndio. Basi akawaambia wajichangishe elfu ishirini kila mtu then mmoja wao akampelekea. Kilichofuata: hawakuulizwa hata walikosomea udereva wala kutakiwa kuonyesha udhibitisho wa kusomea udereva, walijaziwa makaratasi na kutumwa kwendaTRA kumwona mtu "Fulani" na kulipia benki then akaja na driving licence!!!! Nilijichokea tu!!! Huu ni mfano hai watu tunavyosababisha ajali kwa uzembe halafu tunaziita ajali!!

Kuna swala la Kilevi kwenye kusababisha ajali, nadhani wote tunalielewa na wadau mbalimbali wanajaribu kuzishauri mamlaka husika jinsi ya kutatua tatizo hili japo sioni bidii ya mamlaka husika kwenye hili zaidi kushupalia spidi kwa kamera na kujificha kwenye vichaka kuwaotea madereva walio kwenye speed. Swala la Ulevi uwe wa pombe, madawa nk ni swala la kuvalia njuga kwani kwa sasa hivi nasikia hata baadhi ya madereva wa masafa marefu hawapumziki njiani inavyoshauriwa na ni watumiaji wa vilevi wakiwa barabarani; sasa ukichanganya na uchovu wa hizo safari ndefu jibu unalo.


BODABODA: Huu ni ukiwa mwingine mkubwa tu. Nimeishi Douala Cameroon 2007, kule ni bodaboda na taxi tu hakuna daladala. Bodaboda ni nyingi ila ajali i nadra mno!! Kwanini? Douala dreva wa bodaboda na dreva wa gari wanasomea sheria za barabarani sawa na lazima wapate leseni kwa kufanya mtihani wa nadharia na road-test. Sasa hapa kwetu naona kidogo ni tofauti. Wanafundishana usiku na asubuhi yuko kituo cha basi anasubiri abiria ili hali haelewi hata alama moja ya barabarani! Kabla ya pikipiki kuanza kutumika kama taxi Tumbi ilikuwa inapokea ajali 2.1 kwa siku, baada ya bodaboda kuanza kutumika kama taxi ajali tumbi ziliongezeka na kufikia 4.9 kwa siku. Nadhani hii inatupa picha kamili ya mchango wa bodaboda kwenye ongezeko la ajali za barabarani. Pamoja na kutokujua sheria za barabarani bado speed zao ni za hatari nasikia vilevile wachache wao huanza kunywa viroba tangu asubuhi kwa hiyo wanaendesha wakiwa wamekunywa(DUI). Baada ya takwimu za Tumbi, shirika la elimu kibaha walianzisha kozi maalumu ya waendesha bodaboda ili kujaribu kupunguza ajali zinazosababishwa nao na athari zake.

Neno la mwisho: Unapomwambia bodaboda awashe taa mchana anapoingia barabarani ili aongeze "VISIBILTY" yake kwa magari yeye anakujibu kwa kejeli kuwa hawezi kuwasha taa kwasababu hajabeba maiti!! Inasikitisha :-(
 
Heshima kwenu Wakuu,

Hakika nimefurahishwa na hii mbunu mpya jeshi letu la Polisi ambayo wanaitumia.

Polisi katika kuwaelimisha Madereva, wameamua kuwafuata huko huko barabarani. Wamefunga Spika kubwa kwenye magari ya Patrol na kufungulia muziki mkubwa wenye kuelimisha.

Mkiwa kwenye foleni kwa upande wa Dar, Utasiki tangazo likihamasisha Usalama barabarani na kisha unawekwa ule muziki pendwa wa Walevi na Madereva.

Naomba mwinye kuujua huu wimbo atuwekee hapa.

Wimbo wenyewe unaimbwa hivi
"Dereva kalewa pombe sawa hiyo??...hata hiyo si sawa Dereva acha Vituko". Dereva kalewa pombe sawa hiyo??..mwanadada mwenye sauti nzuri anajibu..haataaa...hiyo si sawa Dereva acha vituko. Mia
 
utekelezaji mwema wa sheria za barabarani
 
Back
Top Bottom