Ajali ya basi la Ester, Rav4 yaua watatu Kilimanjaro

Ajali ya basi la Ester, Rav4 yaua watatu Kilimanjaro

Malizia au andika ushauri kwa serikali yetu,,,
Wazipanue barabara za kuingilia manispaa mbalimbali , kutenga sehemu maalum kwa watembea kwa miguu hasa kwenye free way, alama za barabarani ziboreshwe .

Kuwe na Traffic lights kwenye kila makutano ya barabara.

Elimu za sheria za barabarani zitolewe kwa raia na madereva .

Vyombo vibovu vipingwe marufuku hata kunusa pua zao barabarani .

Madereva walevi watengenezewe sheria kali na faini za kutisha.

Boda boda wote wapate mafunzo maalumu ikibidi wapate na vyeti na watumia mihadarati wazibitiwe.

Rushwa zizibitiwe vikali kabisa na abiria watoe ushirikiano kuhusu kuzizibiti ...

Mwisho kabisa abiria wafundishe haki zao wanaponda usafiri wa umma , pia wawe macho kuzibiti uzembe na mwendo kasi wa madereva.
 
Hii familia naifahamu.
Mke aliztaafu na khpata mafao wakaamua wakanunue gari Dar.
wakati wa kurudi wakaamua kukodi dereva awarudishe Arusha, ndio hivyo tena
Watu watatu wamefariki dunia papo hapo baada ya gari aina ya Toyota Rav4 waliokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na basi la abiria la Kampuni ya Ester Kuxury, mkoani Kilimanjaro leo Jumamosi Februari mosi, 2025.

Kaimu Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na uokoaji mkoani Kilimanjaro, Jeremiah Mkomagi amesema ajali hiyo imetokea eneo la Mdawi, Wilaya ya Moshi.

"Ajali imetokea leo asubuhi eneo la Mdawi, watu watatu waliokuwa kwenye gari dogo aina ya Toyota Rav4 wamefariki dunia baada ya gari hilo kugongana uso kwa uso na basi la kampuni ya Ester Luxury lililokuwa likitokea Moshi kwenda Dar es Salaam," amesema Mkomagi.

Amesema chanzo cha ajali ni baada ya dereva wa gari dogo kuyapita magari mengine bila kuchukua tahadhari na kwenda kugongana uso kwa uso na basi hilo.

Hata hivyo, Kamanda Mkomagi amesema hakuna majeruhi kwenye basi hilo, na miili ya marehemu waliokuwa kwenye gari dogo imehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kilimanjaro, Mawenzi.

 
Sijui huwa ni shetani gani huwaingia Mtu anatamani ku overtake tu kwenye mazingira yoyote yale.Upo kwenye Basi wakati mwingine unashangaa Dereva analazimisha ku overtake kwenye mlima na alama za onyo zipo zinazokataza kufanya hivyo,Mtu yupo tayari kubahatisha kubaki hai au kufa.Ubinaadamu kazi.
 
Sijui huwa ni shetani gani huwaingia Mtu anatamani ku overtake tu kwenye mazingira yoyote yale.Upo kwenye Basi wakati mwingine unashangaa Dereva analazimisha ku overtake kwenye mlima na alama za onyo zipo zinazokataza kufanya hivyo,Mtu yupo tayari kubahatisha kubaki hai au kufa.Ubinaadamu kazi.
sure
 
EKU gari bado mpyaa

Poleni sana aisee
IIlikatiwa Bima tarehe 30 Januari na kupata ajali mbaya tarehe 1 Februari
Screenshot_20250203_050300_Tiramis.jpg
 
Mama mwalimu kapokea pension kamchukuwa kijana wake twende dar tukachukuwe gari
Kufika wakamlipa dereva awapeleke Arusha na chuma mpya, familia imempoteza kijana na mama yake mzazi na dereva waliyemkodi. Inasikitisha sana
Kuna mwenye miaka 65 na 61, yupi hapo ni mama na yupi hapo ni kijana wa huyo mama?

Mwenye miaka 25 alikuwa dereva dereva.
20250203_050250.jpg
 
Ukiendesha njia kuu utaona hawa wapumbavu wengi sana. Mmoja akiovateki nao wanafuata nyuma kama nyumbu kumbe mwenzao kakadiria gap lake dogo matokeo yake ndio haya.
Wengi wako hivi. Basi akitoa na wao wanatoa. Basi linawaziba field of vision yao kabisa hawaoni mbele kuna nini, wanalifuata tu basi nyuma.
 
Wengi wako hivi. Basi akitoa na wao wanatoa. Basi linawaziba field of vision yao kabisa hawaoni mbele kuna nini, wanalifuata tu basi nyuma.
Upumbavu wanaoendekeza huko mitaani wanaingia nao njia kuu, wacha wanyooshwe tu.
 
Back
Top Bottom