Ajali ya Dr. Mwakyembe na yatokanayo

Good news: Kwa mujibu wa taarifa ya habari ya TBC, 30 minutes ago, Dr Mwakyembe ameruhusiwa kutoka hospitalini baada ya dakatari aliyekuwa anamtibu kuridhika kwamba anaendelea vizuri.
 
Wasi wasi wangy unakuwa kwa kauli ya polisi Nyombi, ina maana yeye wakati wa tukio alikuwepo? kwani alijuaje kama taili lilichomoka? alielezwa na habari hiyo na nani?
Eh Mungu mponye mtumwa wkoo haraka.
 

Shukran kwa taarifa Waga,inaweza ikawa ajali na pia inaweza ikawa ni mbinu za mafisadi,haiwezekani sisi tuseme moja kwa moja kuwa gari hilo jingine liliwagonga kwa bahati mbaya tu,maelezo ya dereva pamoja na mazingira ya ajali yenyewe yanaonyesha kuwa ni kama walikuwa wanafukuzwa na gari lililokuwa nyuma yao.
Kwa wale wanaojuwa utaalam wa polisi kwenye high speed chasing,utagunduwa kuwa huwa wanaligonga gari kwenye kona ya taa ya nyuma na gari hupoteza mwelkeo,wala huwa hawagongi kwa nguvu,kidogo tu na gari inaspin ama kupinduka...Who knows thats what happened? Anything is possible.
 
Je Mh Mwakyembe naye keshaongea? Aliyoyasema ni sawa na dereva? Tuwekee hapa maelezo ya alichosema kama ukiweza. Maana kama unafutilia mjadala huu utaweza kuona kuwa tunasubiri Mwakyembe apate nafuu ili na yeye aseme yaliyowasibu.
Mh. ameongea na driver wake ameeleza vizuri tu.
Wamesema bada yakupita Ifunda, kulikua na semi trailer inatembea polepole wakaomba kupita, driver akawaruhusu lakini waliposogea mbele driver akasogea kwao, driver wa Mh alibidi aongeze mwendo kukwepa wakagongwa kidogo taa ya nyuma. Wakati ameongeza mwendo ndio akaingia lile shimo aka lose mwelekeo wakapinduka.Mbele kwambali kuna coaster ilikua inakuja.
 
Ni muhimu tuendelee kupeana taarifa kuhusu hali ya huyu mpiganaji wetu. Pia tunahitaji kuhimiza na kufuatilia uchunguzi wa ajali yenyewe. Kwa mfano kuna taarifa (e.g. Mwananchi newspaper ya 22/5/2009) kuwa wakati gari ya Mwakyembe inaingia shimoni na kuanza kupinduka, kuna lori liliigonga kwa nyuma. Je, dereva wa lori hilo amefuatiliwa ili kusaidia kutoa taarifa za ajali? Ni muhimu kuondoa mashaka ya watu kuhusu uwezekano wa 'mkono wa mtu' katika ajali kama hii.
 


Hapo huamini?


hapa unaamini?
 

Hii habari ya gazeti la uhuru (gazeti la CCM) mbona ipo tofauti sana na magazeti mengine? Jamani mambo mengine yanasababisha tuanze kutilia shaka ajali hiyo.

ona Tanzania Daima

sasa unaona tofauti ilivyokubwa, inadaiwa kuwa wakati wa ajali kulikuwa na basi ambalo lililazimika kusimama vinginevyo lingegongana uso kwa uso na gari la Dr. Mwakyembe. Na kwamba ndani ya hilo basi kulikuwa na askari wawili wa usalama bara barani.

Kwamba hakuna mali au nyaraka zilizoibiwa, dereva alibaki na pistol yake, nyaraka za Richmond na Dowans pamoja na laptop zilichukuliwa na trafic police.

Lori lililohusika na ajali halikusimama, licha ya kushuhudiwa na watu wengi (waliokuwa kwenye basi) pamoja na traffic police wawili. mwee hapa lazima ufanyike uchunguzi.
 

inategemea ni nani wametoa conspiracy theories.. hadi sasa sijatoa commentary yangu kama ilivyokuwa kwenye suala la Wangwe. Siharakishi kusema kwenye mambo haya.
 

Hizi habari kweli zinachanganya! Kwasababu hatujui kama gari lilipinduka baada ya kulivaa shimo na kupoteza nati,ama lilipinduka baada ya kugongwa kwenye taa ya nyuma. Na je lilipinduka mara baada ya yeye kujaribu kulikwepa shimo ama gari analo li overtake? Before this story,dereva alisema kulikuwa na gari linawafuata nyuma kwa kasi,na kwamba gari hilo liliwagonga kwa nyuma.
Aaah! Pole Mwakyembe na ni furaha kuwa umepona na kwamba utaendelea na shughuli za ujenzi wa Taifa letu....Ni sawa tu ukimwachia Mungu,na pia mjue kuwa ufisadi unaosababisha tuwe na miundo mbinu mibovu ndo karibia upelekee kupoteza kwako maisha....Adui wa maisha,uzima na afya ni FISADI.....Warudishe mali za watanzania ili tusibakie kwenye jalala la soga,umasikini,maradhi,njaa na maafa yanavyoweza kuzuilika,madhara kama ajali uliyoipata(Ajali endapo kweli ni ajali)
 

Mh. ameongea na driver wake ameeleza vizuri tu. Wamesema....

No no no, dereva tulishamsikia. "Mheshimiwa" amesema nini?

TBC wamesema dakika 30 zilizopita Mkuu ndo katoka hospitali. Sasa ulimsikia on bed side interview hospitali?
 
Nimepata fununu kuwa ajali ya Mh Mwakyembe ilikuwa imepagwa kwa makusudi ya kumuondoa. Tz ni nchi yenye fununu nyingi na mwanzoni nilipomsikia RPC wa Iringa akizungumzia ajali hiyo kwenye vyombo vya habari niliamini ni ajali ya kawaida.

Jana, dereva wa Mwakyembe alikaririwa akidai kuwa aligongwa kwa nyuma na lori na kusababisha ajali tofauti na RPC wa Iringa. Kauli ya dereva wa Mwakyembe niliipuuza na kuona labda kachanganyikiwa au alikuwa anaona 'mauza-uza' ambayo baadhi ya madereva hydai kukutana nayo kabla ya ajali na badala yake nikamwamini RPC wa Irainga.

Leo Dk Mwakyembe kazungumza. Nimemsikia akisema kuwa walikuwa wakijaribu kumpita dereva wa lile lori lakini wakati dereva wa lori lile hakuwa anataka apitwe na gari ya Mwakyembe! Na walipokuwa wakimpita aliongeza mwendo na kusababisha kugongwa na lori kwa nyuma na hivyo kusukumwa na kupinduka. MAelezo ya Dk Mwakyembe yanashabihiana na maelezo ya Dereva wake ambyo niliyachukia kama ni kujitetea tu kwa uzembe wake.

Maelezo haya ya Mwakyembe ndiyo yananipelekea nianze kuchukulia kwa uzito tetesi za uwezekan wa kupangwa kwa ajaili hiyo. HAdi sasa sijasikia kukamatwa kwa dereva wa lori lile wa lori lenyewe azidi ya kusikia kuwa Dereva wa Mwakyembe aliwekwa chini ya ulinzi wa polisi! Je, dereva wa lori na lori lenyewe yuko wapi?

Mwaka jana ajali ya namna hiyo ilimpoteza Mbnge Salome Mbatia Iringa na tuliambiwa kuwa dereva wa lori alikamatwa (sijui kesi ilienda na kuisha vipi). LAkini baada a ajali hiyo tukasikia kuwa mlengwa alikuwa Mh. Zitto abaye ndiye aliyewasaidia majeruhi wa ajali hiyo Zito mwenyewe akathibitisha hayo.

Ni vema tusiichulie ajali hiyo kirahisi rahisi ikizingatia kuwa mwaka jana ilisemekana Mwakyembe alilishwa sumu (ingawa haikuthibitishwa na yeyote) na wazee wa Kyela wakasema watapambana na yeyote anayetishia uhai wa Mbunge wao kupitia njia za giza. Pia tukumbuke kauli ya Mengi kuwa Mafisadi wanamtishia kifo (tukumbuke pia kuwa Mengi na Mwakyembe na Selelii walikuwa mikoa ya Ziwa kwenye ziara ambazo walizungumzia sana mapambano dhidi ya ufisadi).

Wana JF ni vema tuchukulie tetesi hizi kwa uzito unaostahili,
 
inategemea ni nani wametoa conspiracy theories.. hadi sasa sijatoa commentary yangu kama ilivyokuwa kwenye suala la Wangwe. Siharakishi kusema kwenye mambo haya.


Nakuaminia mkuu, wengine twasubiri tamko lako kwa hamu kubwa
 
- Wakuu Nsaji, Engineer na Lazaro vipi jamani tupeni uptodates au? Mana naona maneno mengi sana hapa, damn hebu tupeni dataz huko wakuu!

- Nsaji Mpoki vipi mkuu hakuna habari za uhakika huko? Binafsi nitaanza kuzitafuta rasmi dataz kuanzia kesho, otherwise tupeni dataz wakuu!.

FMEs!
 


Mkuu hilo liko wazi, kale ka sjimo hakaingiii akilini kuweza kuchomoa gurudumu la VX neva, neva..jamani! unless hilo gudumu lilisha legezwa kabla ya safari!

Pia nilishangazwa na salamu za pole za harka haraka kutoka TBC? haija niingia hata kidogo!

Lakini swali linalo baki pia lile lori liko wapi? na dereva wake? Kweli siasa mchezo mchafu!
 
Kinacho nishangaza mimi ni kuwa wakati ajali inatokea, kulikuwa na basi (Dr. Mwakyembe ameita coaster, nadhani hakuona vizuri) ndani ya hilo basi kulikuwa na askari wa usalama bara barani wawili (Two Traffic Police). Hao askari ndo waliookoa mali na nyaraka za Dkt. Mshangao wangu ni kwanini hawakufanya jitihada za kuzuia lori linalohusika na ajali hata kwa kuwapigia simu askari wenzao? Kama dereva wa lori hatapatikana, nitaunga mkono shaka hii.
 
lets rule out foul play....ni barabara mbovu...,na uendeshaji mbaya wa madereva wetu ....hasa wa magari makubwa wana mioyo kutu,alichofanyiwa mwakyembe na truck drivers wetu wanakifanya kila siku na magari mengi yanayoanguka along the highways main reason ni irresponsible careless driving ya malori au wrong parking......

mara zote mimi nikiendesha along the highway zetu na avoid sana kuyafuata mabasi ya mikoani au malori nyuma,au yaje nyuma yangu ..njia nzuri ni kuondoka mapema sana .Moja ya tabia zao maarufu ni kukuruhusu uwapite kwenye kona au hata sehemu ikiwa nzuri anakuruhusu pale anapoona mbele kuna gari lingine linakuja kwa kasi.......wenyewe wanaita kupambanisha ,wanawaacha mnagongana uso kwa uso ...wanabakia wanacheka ndani!!!

misingi mibovu ya uendeshaji wa biashara za usafiri Tazania na imani za kishirikina zinapelekea kuamini kuwa hawa madereva na matajiri zao ni devil worshippers na unaweza kufikiri wakisababisha ajali damu ikimwagika ....wanatoa zaka ya kuteketeza ....na kuhisi wanapata bahati zaidi....
 
Ni mapenzi ya Mungu, tumuachie Mungu.


Huyu Mungu huyu? kuna siku ndimi za moto zitashuka na kutushuhudia kwamba ka! hili simo!

Make walo kufa kwa mabomu, mapenzi ya Mungu.., wanao kolimbwa wote mapenzi ya Mungu.. jamani Mungu gani huyo mwenye kupenda mabaya yatokee juu ya viumbe wake alio tuumba kwa mapenzi yake na kwa mfano wake?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…