Ajali ya Ndege ya Precision Air imetuvua nguo wazi wazi

Ajali ya Ndege ya Precision Air imetuvua nguo wazi wazi

It's as if we are GOOD FOR NOTHING !!!
 
Polisi wa doria ziwa Victoria kazi yao ni nini sasa

Jwtz - Navy kazi yao ni nini sasa

Tanzania yangu ina safari ndefu sana haki tena [emoji174][emoji174][emoji706][emoji706]
Majeshi yetu ni ya kupita mbele ya rais na kumfanyia michezo ya kuigiza kama vile walivyokuwa porini wiki iliyopita. Ila katika uhalisia wa matukio, ni watupu.
 
View attachment 2408785
Wakuu kwa mara nyingine tena nitoe pole sana kwa waliopatwa na ajali ya Ndege leo huko Bukoba baada ndege ya Shirika la Precision Air kupata hitilafu wakati wa kutua na kuingia Victoria pia wale waliopoteza maisha basi Mwenyezi Mungu awarehemu na kuzipumzisha nafsi zao pema peponi.

Kusema ukweli nashindwa kuelewa ni jambo lipi sisi kama taifa tunaweza kujivunia kulifanya kwa ukamilifu, nakosa majibu jamani. Hivi uwezo wetu wa kukabili majanga uko kwa namna ipi? hakuna siku limetokea janga nchi hii vyombo byetu vikafanikiwa kudhibiti kwa 100%. Kila wakati lazima madhara makubwa yatokee.

Leo tumeshuhudia mambo ya ajabu sana kama nchi utadhani tuko miaka 40 huko, Ndege imekaa kwenye maji zaidi ya lisaa hakuna hata helicopter ya uokoaji au boti za kuvuta ndege za kisasa zilizofika eneo la tukio matokeo yake ndege inavutwa kwa kamba na wananchi, mambo ya ajabu kuwahi kutokea.

Nashindwa kuelewa serikali inajali kweli maisha ya wananchi wake? ni mpaka afe nani ndio nchi hii itashtuka kuwa tunatakiwa kuwa tayari kukabili majanga badala ya kuripoti madhara? Inakera na inaumiza sana, narejea kukumbusha matukio makubwa ya yaliyochukua maisha ya watu wetu wengi, ni watu tu hawakuwajibika ipasavyo na kusababisha maisha ya watu kupotea.

Hii nchi inahitaji mageuzi makubwa sana ya kimfumo, viongozi wetu hawajali maisha ya wananchi, wamekuwa wabinafsi na wasio wabunifu kukabiliana na matatizo.

Leo tumeonesha dunia ni kiasi gani hatuna uwezo wowote wa kujiokoa wenyewe, hatuna vifaa, hatuna wataalamu mpaka napata shida kuwaza ni kiasi gani hii nchi iko salama kiulinzi? mbona kama siku tukikumbwa na mafuriko ya mwezi mmoja watu wote tutaelea kwenye maji jamani?

Hwa watu hawatujali jamani, hawana muda na sisi.
Toka enzi za MV Bukoba hatujawahi kua na boti/meli ya uokoaji kweli? Labda hii kitu itabadilisha mtazamo wa umuhimu wakua nayo maana dah aise hapana. Mungu atupe busara kama nchi kuzingatia hivi vitu kabla hayajatokea.

Ingekuwa nchi ya wenzetu kuna kiongozi angejiuzulu kutokana na maafa ya aina hii.
 
Hakuna helicopter ya kunyenyua tani 20 Tanzania, Eastna Central Afrika

Hakuna tugboat ingesaidia kwenye kile kina kifupi.
Pia watu walikuwa washakufa tayari kabla hawajaokolewa, na hii ni kutokana na impact ya ndege kupiga maji
 
Kwa ufupi hamna wizara hata Moja yenye mikakati yakudumu na yenye kuendana na maisha ya Sasa tuliyonayo, mambo yanafanywa kwa matukio ya dharura ila hatuna mipango Wala njia yakutukomboa ni kitu chakushangaza watu wanaangalia matumbo yao tuu,swala la moto kule Kilimanjaro na hili la precision linanifanya kuishangaa hii nchi kwa siku hizi chache Bado umeme na maji ni mambo ya ajabu
 
View attachment 2408785
Wakuu kwa mara nyingine tena nitoe pole sana kwa waliopatwa na ajali ya Ndege leo huko Bukoba baada ndege ya Shirika la Precision Air kupata hitilafu wakati wa kutua na kuingia Victoria pia wale waliopoteza maisha basi Mwenyezi Mungu awarehemu na kuzipumzisha nafsi zao pema peponi.

Kusema ukweli nashindwa kuelewa ni jambo lipi sisi kama taifa tunaweza kujivunia kulifanya kwa ukamilifu, nakosa majibu jamani. Hivi uwezo wetu wa kukabili majanga uko kwa namna ipi? hakuna siku limetokea janga nchi hii vyombo byetu vikafanikiwa kudhibiti kwa 100%. Kila wakati lazima madhara makubwa yatokee.

Leo tumeshuhudia mambo ya ajabu sana kama nchi utadhani tuko miaka 40 huko, Ndege imekaa kwenye maji zaidi ya lisaa hakuna hata helicopter ya uokoaji au boti za kuvuta ndege za kisasa zilizofika eneo la tukio matokeo yake ndege inavutwa kwa kamba na wananchi, mambo ya ajabu kuwahi kutokea.

Nashindwa kuelewa serikali inajali kweli maisha ya wananchi wake? ni mpaka afe nani ndio nchi hii itashtuka kuwa tunatakiwa kuwa tayari kukabili majanga badala ya kuripoti madhara? Inakera na inaumiza sana, narejea kukumbusha matukio makubwa ya yaliyochukua maisha ya watu wetu wengi, ni watu tu hawakuwajibika ipasavyo na kusababisha maisha ya watu kupotea.

Hii nchi inahitaji mageuzi makubwa sana ya kimfumo, viongozi wetu hawajali maisha ya wananchi, wamekuwa wabinafsi na wasio wabunifu kukabiliana na matatizo.

Leo tumeonesha dunia ni kiasi gani hatuna uwezo wowote wa kujiokoa wenyewe, hatuna vifaa, hatuna wataalamu mpaka napata shida kuwaza ni kiasi gani hii nchi iko salama kiulinzi? mbona kama siku tukikumbwa na mafuriko ya mwezi mmoja watu wote tutaelea kwenye maji jamani?

Hwa watu hawatujali jamani, hawana muda na sisi.
Nashindwa kuelewa serikali inajali kweli maisha ya wananchi wake? ni mpaka afe nani ndio nchi hii itashtuka kuwa tunatakiwa kuwa tayari kukabili majanga badala ya kuripoti madhara? Inakera na inaumiza sana, narejea kukumbusha matukio makubwa ya yaliyochukua maisha ya watu wetu wengi, ni watu tu hawakuwajibika ipasavyo na kusababisha maisha ya watu kupotea.
 
Polisi wa doria ziwa Victoria kazi yao ni nini sasa

Jwtz - Navy kazi yao ni nini sasa

Tanzania yangu ina safari ndefu sana haki tena [emoji174][emoji174][emoji706][emoji706]
Navy wapo busy kgamboni uko wanasimamia LONGONI BEACH
 
Sasa yale mazoezi ambayo vyombo vya usalama hufanya kuonesha utayari wa kukabiliana na dharula yana maana gani ikiwa hayana msaada kwenye kukabili majanga ya ndani zikiwemo ajali?
Ili kumfurahisha mgeni rasmi, wageni na wananchi waliojitokeza. Ili kijiweni wanapopata kahawa, mihogo na chai wakasema Tz ina makomando wengi sana ipo vizuri ni ya 3 kwa ujasusi duniani.
 
Usitegemee jambo jipya toka kwenye serikali ya chama cha mapnduzi.Walipindua mambo mengi ndo maana vitu vingi viko kichwa chini miguu juu.Ni vile tu vichwa vyetu vizito kuelewa ila hawa watu walishashindwa toka kitambo.Ndo maana wanalamba asali tu sasa mambo mengine ya wananchi yatajiset yenyewe yatakavyojua.Ndo maana tumewekeza zaidi kwenye kupongezana na kusifiana badala ya kukosoana wakati kimsingi hakuna lolote kubwa tuliloliweza.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom