Ajira ni mtihani

Kuajiriwa na mtu aliyeishia la 5 haijawahi kuwa laana ila tunakumbushwa kuwa maishani usimdharau mtu huwezi jua atakae kufaa ni yupi kikubwa ni kuishi kwa usawa tuu
 
Bwamdogo anafikiria akipata kazi ndo dharau zitaisha! Dogo wenzio tumemaliza 2012 tukasota wee, tukajiongeza na mtaa, niliamua kuendeleza kipaji changu cha utoto cha ufundi, nikaingia gereji leo mi ni fundi wa umeme wa magari. Yan fresh tuu hakuna mtu anajua nina degree na nimesogea sehemu flani kimaisha. Weka degree pembeni afu tumia ulichonacho "kusavaivu" bwa mdogo. Nilikaa gereji mwaka tuu nikawa nimejifunza kazi kibishi sana, uzuri wa gereji hatubaniani kufundishana kazi madam uwe mtii, kujituma na kuheshimu watu wanaokufundisha. Alhamdulilah degree yao nishaisahau kabatini huko.
 
Habari wakuu natafuta kazi Nina certificate ya laboratory Nina experience ya laboratory technician, Quality control, microanalysis, blending oparetor.pia sichagui kazi .yeyote atakaye nisaidia yani anipe connection nipo tayri kuingia naye mkataba atakuwa anachukua asilimia 10% ya mshahala wangu ndani ya miezi 12.asanteni
 
Lete mchanganuo tufungue maabara huku mtaani!
 
 
Mtihani sana
Bro ila usjal utafanikiwa sana Cha msingi ni Dua tu, wengine bado tunasoma lkn hatujuw mbeleni tutavuna nn,...
Kuna wadau waliachaga shule kitambo lkn Wana maisha mazuri na wanaidhihaki elimu mno kama ivyo,,.nishawahi kusikia mtu anamwambia mwenzake "natafuta anayeweza kuchimba choo ila awe na cheti Cha form four" hii kauli ilisemwa na mtu ambaye ameishia darasa la Saba akimwambia ambaye amehitimu form six akisubir kwenda chuo,.. hizo dharau kwakweli sjuw zitaishaga lini
 
Dharau kila sehemu zipo ni kupotezea tu.life linabadilika.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…