Ajira za bara tunaomba wote, lakini za Zanzibar wanataka Mzanzibar pekee

Mingendeu

Senior Member
Joined
Aug 26, 2019
Posts
115
Reaction score
237
Serikali inapaswa kutafakari ni kwa namna gani wanaweka usawa kwenye hili.

Wahitimu kutoka bara wanalalamika sana. Ajira zinazotangazwa bara wanasailiwa hadi wazanzibar, lakini ajira zinazotangazwa Zanzibar, sifa moja wapo kubwa ya kusailiwa ni kuwa mzanzibar.

Mzanzibar anafaida mara 2, anaweza kupata ajira Zanzibar au Bara. Hii ipo tofauti kabisa kwa wahitimu wa bara.

Serikali wanaweza kuchukulia swala hili kama swala dogo sana, ila kiuhalisia linakuza chuki ndani ya muungano wetu. (Ajira ni moja ya changamoto kubwa tena inagusa kundi kubwa yaani vijana).

Serikali kupitia ofisi wa makamu wa Raisi, wizara ya kazi pamoja na utumishi wanatakiwa wakae na kuchukua hatua za haraka mapema. Baada ya miaka kadhaa hili swala litakuwa kubwa na halitaweza kutatulika kirahisi.
 
Kuwa tu mpole. Maana viongozi wetu wa Tanganyika, wakiwa na akili zao timamu wamekubali tuwe na Muungano wa hovyo kabisa wa changu changu, chako changu na hao Wazanzibari.
 
Inapotokea tangazo la kazi/ajira Nchini kwa maana ya huku bara tunafanya application ya tangazo husika kwa kuzingatia vigezo vya umri miaka 18 hadi 45 sifa nyingine ni kuwa mtanzania kuwa na vyeti na mambo kama hayo. So kwa kawaida watanzania wote wenye sifa na vigezo kulingana na tangazo husika tunaomba nafasi hizo.

Ila kumekuwa na utofauti zanzibar
Kwa maana linapotokea tangazo lakazi kina kuwa na vigezo vya ziada kama kitambulisho cha mkazi je hapa shida inakuwa ni nini ikiwa bara zikitangazwa nafasi za kaz tunaomba wote ikiwa tu ni watanzania na je shida ikowap upande wa zanzibar waombe wenye vitambulisho vya kule tu 🤔😭

Pia soma;

Ajira Zanzibar ni kwa Wazanzibar pekee?
 
Inapotokea tangazo la kazi/ajira Nchini kwa maana ya huku bara tunafanya application ya tangazo husika kwa kuzingatia vigezo vya umri miaka 18 hadi 45 sifa nyingine ni kuwa mtanzania kuwa na vyeti na mambo kama hayo. So kwa kawaida watanzania wote wenye sifa na vigezo kulingana na tangazo husika tunaomba nafasi hizo.

Ila kumekuwa na utofauti zanzibar
Kwa maana linapotokea tangazo lakazi kina kuwa na vigezo vya ziada kama kitambulisho cha mkazi je hapa shida inakuwa ni nini ikiwa bara zikitangazwa nafasi za kaz tunaomba wote ikiwa tu ni watanzania na je shida ikowap upande wa zanzibar waombe wenye vitambulisho vya kule tu 🤔😭
Muungano huu ni dhalimu
 
Muungano huu wanafaidika nao wanzazibari zaidi kuliko wabara ila kwa kulalamika wao utadhani ndio wananyanyasikaaaaa!
 
Tukiwa chuo fulani kule Dodoma miaka ya nyuma huko tulikuwa na Wazanzibar wanafanya kazi wizara nyeti huko kwao jamaa mmoja wa bara akawa anajaribu kutengeneza connection apate shavu kule Wazanzibar walimwambia waziwazi wewe wa Bara kule huwezi pata kazi kamwe. Hawa jamaa ni wabaguzi sana.
 
Mbona katika taasisi zinazohusu muungano wabara wapo wengi tu.
Tena ni zenye asali za nyuki wadogo kama BOT , TRA hata jeshini wapo wengi tu.

Hii wala sio ubaguzi ni ku balance tu, maana nchi ni ndogo sana so unaposema wabara wote wawe wanamiliki ardhi kule na watumishi kutoka bara waajiriwe kule kwa taasisi zisizohusu muungano kutakuwa hakuna wazanzibar tena.

Mbona mambo mengi bara wanafaidi huku tena uchumi mkubwa upo bara kuliko zanzibar.

Nikuulize unavijua viwango vya mishahara vya watumishi wa Zanzibar?

Ukiijua utaacha mdomo wazi.


Kiufupi Zanzibar hakuna uraia ni ukaazi tu wakati kabla ya Muungano Zanzibar kulikuwa na uraia wake mbona hamulitetei hilo na wakati ni nchi mbili zilizoungana?

Unapoleta mambo humu uwe unayapima kwa mizani ya uadilifu sio unaangalia upande mmoja tu.

Kwa ukweli wa mambo hata ajira zinazotoka kule sio nyingi kama za huku bara.
 
Inapotokea tangazo la kazi/ajira Nchini kwa maana ya huku bara tunafanya application ya tangazo husika kwa kuzingatia vigezo vya umri miaka 18 hadi 45 sifa nyingine ni kuwa mtanzania kuwa na vyeti na mambo kama hayo. So kwa kawaida watanzania wote wenye sifa na vigezo kulingana na tangazo husika tunaomba nafasi hizo.

Ila kumekuwa na utofauti zanzibar
Kwa maana linapotokea tangazo lakazi kina kuwa na vigezo vya ziada kama kitambulisho cha mkazi je hapa shida inakuwa ni nini ikiwa bara zikitangazwa nafasi za kaz tunaomba wote ikiwa tu ni watanzania na je shida ikowap upande wa zanzibar waombe wenye vitambulisho vya kule tu [emoji848][emoji24]
Muungano wa hovyo kabisa huu hata ardhi wao wanahaki ya kumiliki wakati sisi hatuna mamlaka hayo kwao
Tumewalea vyakutosha
 
Au hujuma kwa serikali ?
IMG-20240811-WA0004.jpg

Muwe na siku njema
 
Au hujuma kwa serikali ?
View attachment 3066683
Muwe na siku njema
Tuungane tudai serikali ya Tanganyika, ili vya Tanganyika vibaki kuwa vya watanganyika tuu, bila hivyo wazanzibari wataendelea kutumbua na vya watanganyika kupitia huu muondo wa muungano wa serikali mbili wakati vya Zanzibar wakila wao pekeyao
 
Back
Top Bottom