Ajira za Walimu: Kigezo cha kujitolea ni kichaka cha rushwa, upendeleo na udanganyifu. Rais Samia kimulike

Ajira za Walimu: Kigezo cha kujitolea ni kichaka cha rushwa, upendeleo na udanganyifu. Rais Samia kimulike

mbingunikwetu

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2015
Posts
13,897
Reaction score
18,477
Kumekuwa na upendeleo wa dhahiri katika ajira za ualimu kwa siku za hivi karibuni. Utakuta imetangazwa ajira ya waalimu wa hesabu na fizikia lakini majina yakitoka unakuta wa Biology wamo!

Utakuta imetangazwa waalimu wanaotakiwa ni wale waliomaliza masomo mwisho 2017, lakini unakuta waliomaliza hadi 2018 wamo!! Sasa hayo ni makosa ya upendeleo ya dhahiri na yakilalamikiwa wakubwa wanakosa mahali pa kuficha nyuso zao!! Unakuta jina moja limetoka zaidi ya m,ara moja, hapo ujue nafasi imetunzwa kinyemela ya mtu fulani

Sasa imebuniwa njia rahisi ya kupendelea ambayo mtu hatalazimika kuficha uso wake!! Kwanza huwezi kuweka sheria ya mchezo wakati wa mchezo ukiwa umeshafika.

Ilipaswa itangazwe mapema baada tu ya ajira zilizopita kuwa safari ijayo tutatumia kigezo cha kujitolea kama sharti mojawapo la kupata ajira ya ualimu.

Inawezekana walioandaliwa kupendelewa walipewa siri hii mapema na wakatafuta hizo nafasi za kujitolea ili tu waje wawe na sifa ya ziada kuliko wenzao. Lakini pia hapa utafunguka mlango mkubwa wa rushwa. Watu watapata barua za kujitolea wakati siyo.

Ushauri wangu: Kigezo hiki cha kujitolea KISITUMIKE awamu hii maana wengi walikuwa hawakijui. Ila kama itaonekana ni cha muhimu, basi itangazwe SASA kuwa safari IJAYO zikitokea nafasi za ualimu, kigezo hicho kitatumika.

Halafu uwekwe utaratibu wa wazi na Tamisemi wa kuomba hizo nafasi za kujitolea kama nafasi za ajira zinavyoombwa na majina yatoke kwa wazi na shule walizopangiwa kujitolea ziwe wazi. Hii itapunguza rushwa na udanganyifu.

Utaratibu mzuri wa kugawa ajira utumike ule ule uliokuwa unatumika. Aliyehitimu kwanza anafikiriwa kwanza. Haiingii akilini mtu aliyehitimu 2019 akapata ajira na mtu aliyehitimu mapema zaidi kama 2017 au 2018 akakosa kwa masomo yale yale.

Rais wetu tunakuomba ulifuatilie hilo maana hao uliowapa dhamana wamekuja na vigezo ambavyo wengine waliandaliwa navyo kwa siri!
 
Safari hii tusione mtu aliyehitimu 2020 amepata ajira kama ambavyo imekuwa inatokea. Mtu aliyehitimu mapema anakosa na mtu aliyehitimu jana tu anapata tena kwa masomo yale yale.
 
Ni rushwa na uonevu maana it is not statutory kuwa mpaka kuajiliwa lazima uwe umejitolea. Mtu anajitolea kwa utashi wake, kwanini iwe condition moja ya kuajiliwa. Kuajiliwa ni haki ya kila mtanzania regardless kujitolea. Merit ni academic performance yake as exemplified by his credentials

Samia ondoa haya majitu ya Jiwe, yameshakuwa na mind set ya uonevu.
 
Serikali wao wenyewe ndo wametengeneza huo mwanya wa rushwa , kama mliwarundika tuu toka 2015 huku mmekomaa na ujenzi sjui wa mji mkuu wa Dodoma na ununuzi wa Madege na ma SGR hayo , na wote Wana sifa , sasa mnawafungulia na vi ajira viduchu unategemea nn na wote Wana sifa ...lazima rushwa itembee tuu na waliopo kwenye udahili lazima watajirike
 
Dah kuna meng sn kweny kada ya ualimu hasa kuchangua watu weny sifa moja labda wamepishana miaka ya kumaliza.

Kada zingne ukienda kweny interview unapigwa maswali ukitoka unajua kabisa nimekunya au bahati kutoka kwa Mungu.
 
Ni rushwa na uonevu maana it is not statutory kuwa mpaka kuajiliwa lazima uwe umejitolea. Mtu anajitolea kwa utashi wake, kwanini iwe condition moja ya kuajiliwa. Kuajiliwa ni haki ya kila mtanzania regardless kujitolea. Merit ni academic performance yake as exemplified by his credentials

Samia ondoa haya majitu ya Jiwe, yameshakuwa na mind set ya uonevu.
Waseme ukweli kuwa hawana uwezo wa kuajiri. Over
 
Serikali wao wenyewe ndo wametengeneza huo mwanya wa rushwa, kama mliwarundika tuu toka 2015 huku mmekomaa na ujenzi sjui wa mji mkuu wa Dodoma na ununuzi wa Madege na ma SGR hayo, na wote Wana sifa, sasa mnawafungulia na vi ajira viduchu unategemea nn na wote Wana sifa lazima rushwa itembee tuu na waliopo kwenye udahili lazima watajirike.
Ndiyo hicho kina watesa sana
 
Samia ondoa haya majitu ya Jiwe, yameshakuwa na mind set ya uonevu.
Yale yale! Kwani wakati huyo Jiwe akiwa Rais, huyo Samia alikuwa wapi? Na unadhani chanzo cha haya yote ni hayo majituu, au ni Hayati?

Mimi naunga mkono kutumika kwa hiki kigezo cha kujitolea. Walau hao vijana na wenyewe wataona Serikali imetambua mchango wao. Na uzuri karibia wote wanatokea familia maskini! Hivyo wakipata hizo ajira, familia zao zitapata ahueni ya kimaisha.
 
Yale yale! Kwani wakati huyo Jiwe akiwa Rais, huyo Samia alikuwa wapi? Na unadhani chanzo cha haya yote ni hayo majituu, au ni Hayati?

Mimi naunga mkono kutumika kwa hiki kigezo cha kujitolea. Walau hao vijana na wenyewe wataona Serikali imetambua mchango wao. Na uzuri karibia wote wanatokea familia maskini! Hivyo wakipata hizo ajira, familia zao zitapata ahueni ya kimaisha.
Wakishatoa hizi kidogo mpk 2023 tena
 
Imekaaje pale Serikali inapojinasibu kutumia kigezo cha kuajiri waliojitolea alafu huyohuyo mwalimu anaweza kwenda shule mpaka nne na akaambiwa hakuna nafasi za kujitolea.

Kwamba: Wizara Vs Shule zina maono tofauti.
 
Back
Top Bottom