Akamatwa akiwa na mikoba/pochi 135 aliyokwapua sehemu mbalimbali

aleesha

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2016
Posts
798
Reaction score
1,178
Mnamo tarehe 05/03/2022 kuanzia majira ya saa 12 : 00hrs mpaka saa 12 : 00hrs a/insp Fadhil wa CID Madema akiongozana na makachero wa kituo hicho walifanya msako maalum wa kumtafuta mtuhumiwa anaejihusisha na vitendo vya wizi wa kukwapua vipochi pamoja na mikoba sehemu zenye msongamano wa watu hususan vituo vya daladala.

Katika msako huo ulifanikiwa kumkamata mtuhumiwa huyo aitwae Bahati Iddi Kimweli 32yrs Msambaa wa Jangombe na baada ya kupekuliwa chumbani kwake alipatikana na vipochi na mikoba 135 vya wanawake ambayo ameikwapua sehemu mbalimbali kwenye vituo vya daladala.

Mtuhumiwa huyo yupo kituo cha Polisi Madema akiendelea kuhojowa zaidi.




 
Nadhani amepata mafunzo mazuri kutoka kwenye dini ya hakhi..ameamua kurudi kitovuni kuja kui practice zaidi..hongera kwake mpeni ushirikiano ni ndugu yenu huyo kutoka bara.

#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Je ambavyo ameviuza?
 
Tutake radhi kina Kimweri. Hakuna Kimweri wa Jang'ombe hapa.
 
Angekuwa anahonga pisi hizo pochi za wizi asingekuwa na mzigo mkubwa hivyo.
Ajiandae kwenda kunyea ndoo kwa miaka 15 ijayo.
 
Sijui zitapigwa mnada au watapewa motisha watendaji wenyewe, hapo ukute zimekwapuliwa kila pembe ya jiji
 
Picha ya mwizi iko wapi tumuue mtandaoni
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…