AKILI ZA MTU MWEUSI: Kuchangishana sherehe (kadi za mwaliko na magroup )

AKILI ZA MTU MWEUSI: Kuchangishana sherehe (kadi za mwaliko na magroup )

Niseme ukweli tu, kuna wakati niliteuliwa kuwa mwenyekiti wa kamati ya harusi, nilimuuliza mwenye harusi unataka kufanya harusi ya bajeti kiasi gani? Alijibu nataka kufanya harusi simple tu ya bajeti ya laki nane, wajumbe walimuuliza we una kiasi gani? Alijibu ana laki moja. Mwisho wa michango zilipatikana laki tatu pamoja na yake. Nilipangia bajeti hizohizo zilizopatikana, wali maharage bila nyama wala soda, maji ya kisima ikatoka hiyo. Ifike muda viongozi wa dini wawaache huru waumini kufunga ndoa kimtindo kulingana na bajeti zao, kuoa hata bila kufanya sherehe, inatosha kusainishwa cheti cha ndoa, jioni wanandoa watajua wale nini wenyewe
 
Ukitaka kuoa inabidi 100% uwe na mpunga wako ,kama bajeti ni 10m basi inabidi uwe na 10m kwa mfuko ,kama mtu anatataka kukuchangia iwe option na si lazima.
kabisa. Zamani muoji ndiye alijigharamia kulisha wahudhuriaji wa harusi yake bila kujali watahudhuria wangapi, upuuzi fulani ukaingia wa kuchangia, imeenda hivyo mpaka ikafikia kwenye madaraja ya kutoa kulingana na uwezo wako. Ni ufahari na anasa tu zimetawala harusi hizi zisizo na maadili ya kindoa na hazidumu ni show off tu huku watu wamekamuliwa vya kutosha japo ni hiari kutoa. Harusi zenyewe ni za kichoyo, wanaingia waliotoa mchango tu. Tena umezuka uvaaji wa wahudhuriaji wa kihuni na ukahaba ukumbini huku harusi ikifanyika usiku wa manane. Mambo ni mengi ya kukera kuhusiana na harusi hizi za kuchangia.
 
Niseme ukweli tu, kuna wakati niliteuliwa kuwa mwenyekiti wa kamati ya harusi, nilimuuliza mwenye harusi unataka kufanya harusi ya bajeti kiasi gani? Alijibu nataka kufanya harusi simple tu ya bajeti ya laki nane, wajumbe walimuuliza we una kiasi gani? Alijibu ana laki moja. Mwisho wa michango zilipatikana laki tatu pamoja na yake. Nilipangia bajeti hizohizo zilizopatikana, wali maharage bila nyama wala soda, maji ya kisima ikatoka hiyo. Ifike muda viongozi wa dini wawaache huru waumini kufunga ndoa kimtindo kulingana na bajeti zao, kuoa hata bila kufanya sherehe, inatosha kusainishwa cheti cha ndoa, jioni wanandoa watajua wale nini wenyewe
Hapo kwa viongozi wa dini hawahusiki na hii kadhia. Ndoa mfano ya kikatoliki gharama unayotakiwa kulipa kanisani hazidi elfu 50. Hapo ikijumuisha hela ya mafundisho ya ndoa na cheti. Sijajua madhehebu mengine kama kuna gharama yoyote.

Kwa waislamu najua ndio almost zero cost
 
Hapo kwa viongozi wa dini hawahusiki na hii kadhia. Ndoa mfano ya kikatoliki gharama unayotakiwa kulipa kanisani hazidi elfu 50. Hapo ikijumuisha hela ya mafundisho ya ndoa na cheti. Sijajua madhehebu mengine kama kuna gharama yoyote.

Kwa waislamu najua ndio almost zero cost
Makanisa mengine inategemea na maono ya mchungaji wa mahali hapo. Wengine huchangisha mchango mdogo wa fedha kununua mchele, maharage, nyama, soda, matunda, maji na viungo bila kujali mwenye harusi kajiandaaje kwa bajeti yake na harusi huliwa hapohapo kanisani au ukumbini kutegemea na kamati imechangaje michango. Washirika humbeba muumini mwenzao kumfanyia harusi bila mchango mzito. Unakuta mchango ni mdogo elfu moja, mbili, haizidi elfu tano, mtu anakabidhiwa mke wakaanze maisha ya ndoa
 
Sure..umesema ukweli ila sasa mfumo ndo umetushape hivo mkuu.. hivi nimeungwa kwenye magrupu manne ya michango ya harusi na wato jamaa zangu.. wao ni employees ila mimi jobless..natafuta namba nileft.!
 
Hizi ni nyuzi special kuelezea akili za mtu mweusi, naanzia hapa.
Akili za mtu mweusi season1.
ep 01 :
Kuchangishana pesa kwenye raha binafsi za watu( hizi wanaita sherehe za harusi, ubatizo, birthday n.k )

* Kuna huu ujinga unaoendelea kwenye jamii zetu wa kuchangishana kwenye furaha binafsi za watu pesa kwa ajili ya kuendeshea shughuli zao.

* Imefika hatua wajinga wanakusanya michango kama vile ana kudai, ni mwendo wa kukufuatilia kila uchwao ili tu umsaidie pesa ya kuendeshea huo upuuzi wake sijui ndoa, birthday na ujinga mwengine.

* Kuna watu wanavuka mstari mwekundu mpaka anakuunganisha kwenye magroup ya WhatsApp ili mpige zogo humo za namna gani mtapush upuuzi wake anao panga kuufanya.

* Kadi sasa hapa ndio kuna ujinga mwingi sana imekuwa kama kitambulisho cha taifa kwamba lazima uchukue na utie kiasi tajwa huu ni ufala wa level ya juu sana.

* Sherehe za harusi, ubatizo, birthday, vipaimara n.k hizi zote ni raha binafsi sio mchongo kutaka marafiki, ndugu, watu wa karibu, watu unao juana nao, majirani kukuchangia kwenye raha zako binafsi unazo taka fanya.

* Fanya vitu kwa uwezo wako usiwape shida jamii kuuwazia upuuzi wako namna gani ya kuupush.

NB: Hizi akili za namna hii kwa watu weusi inabidi zikome mara moja na najua kuna majitu humu huu uzi umewagusa kwa sababu ndizo akili hizi zimejaa vichwani mwao.
Nakazia, Huo Upumguani Ukome.
 
hivi 𝘂𝗹𝗮𝘆𝗮 𝗸𝘄𝗲𝘁𝘂 𝗸𝘂𝗻𝗮 𝘂𝗷𝗶𝗻𝗴𝗮 𝗵𝘂𝘂 𝗮𝘂 𝘂𝗹𝗶𝘀𝗵𝗮𝘄𝗮𝗵𝗶 𝗸𝘂𝗼𝗻𝗮 𝗸𝘄𝗮 𝗺𝗮𝘁𝗮𝗷𝗶𝗿𝗶
 
Nimetoka kulambwa km dola 100 mda si mrefu inauma balaa,sema tu namuheshimu huyo demu na mwanae anaeolewa ni mchepuko so nabembelezea niendelee kutafuna tu.
Wengine sitoi senti kumi na hata unialike bure siji vilevile
hata akiolewa potelea pwete😁.
Huna pesa wewe maskini ndio maana unalalamikia tumichango twa 20,000 hadi 50,000. 😆😆😆
 
Back
Top Bottom