Al-Shabab walitumia dola milioni 24 kununua silaha mwaka jana

Al-Shabab walitumia dola milioni 24 kununua silaha mwaka jana

John Haramba

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2022
Posts
365
Reaction score
1,374
1645609131242.png

Kundi la Al-Shabab nchini Somalia lilitumia dola milioni 24 mwaka 2021 kununua silaha, kulingana ripoti ya Taasisi ya Hiraal lenye makao yake Mjini Mogadishu.

Ripoti hiyo pia inadai kuwa Al-Shabab ambao wana ufungamano na Al-Qaeda, ina kusanya mapato ya karibu dola milioni 180 kila mwaka.

Ripoti hiyo iliyopewa jina la Al-Shabab’s Arsenal - From Taxes to Terror inasema kundi hilo linatumia mbinu mbalimbali kupata silaha, ikiwa ni pamoja na ununuzi wa moja kwa moja kutoka soko la ndani, na kutoka kwa wafanyabiashara wa silaha walio na kandarasi ya kununua na kusambaza silaha kutoka nje ya nchi, hasa Yemen.

Taasisi ya Hiraal pia inasema kwamba waasi wanadhibiti sehemu kubwa ya Somalia na kudumisha kiwango cha ushawishi kwa raia kupitia mchanganyiko wa ushawishi, utawala na kulazimisha.


Source: bbc
 
............Ukisikia wanasema hivyo ujue ndio wale wale kwani magaidi nia na lengo lao linajulikana.......... wanasema wao wanampigania allah na sio Marekani ambaye wao wanamtambua kama kafiri sasa muislam na kafiri wapi na wapi.
 
Back
Top Bottom