Da Vinci XV
JF-Expert Member
- Dec 7, 2019
- 3,862
- 6,438
- Thread starter
- #21
Sawa sawa mkuu tutajitahidišLete story DaVinci,utupe nasiri km hii jamii yasiri ina usika na hii BITCOIN? Naona hiz coins zimekua habari ya dunia wkt huu
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Sawa sawa mkuu tutajitahidišLete story DaVinci,utupe nasiri km hii jamii yasiri ina usika na hii BITCOIN? Naona hiz coins zimekua habari ya dunia wkt huu
Mambo ya Babylon ya NabukadnezaALL SEEING EYE, EYE OF PROVIDENCE - 1
Wasalaam,
View attachment 1762279
Kila mmoja alama hii aliitafsiri vile ajuavyo yeye huku madaai ya kuhusishwa na vikundi vya Illuminant /Freemasonry yakishamiri zaidi.
Wengi wetu tumeichukulia kama alama ya mficho, kama zilivyo alama nyingi za kuficha na yenye ishara za siri.
'EYE OF PROVIDENCE' Alama ya jicho lililowekwa ndani ya pembetatu (pyramid) ni ishara ambayo imehusishwa na nadharia nyingi sana,
Alama ya jicho hilo sio tu linaonekana kwenye makanisa mengi na majengo ya Masons na vikundi vya siri ulimwenguni, pia inaoneka nyuma dola moja ya Marekani na vile vile kama Muhuri Mkubwa wa Marekani
Alama hii imesemwa kwenye nadharia nyingi za kushangaza na zisizo za kawaida
View attachment 1762302
Mfano
- kama upatikanaji wake kwenye nembo na vielelezo(dola) vya serikali ya Marekani,
- Alama na Ishara ipatikanayo kumwakilisha mungu katika dini (Ukristo)
- Upatikanaji wake katika vielelezo na nembo za Vikundi vya Siri (ilumminant)
- Kitambulisho cha Mungu wa Kipagani wa Misri ya kale, na Pia alama hii Uhusishwaji wake na Mpinga kristo (Anti christ)
Hizo ni miongoni mwa nadharia kuhusu Alama hiyo.
View attachment 1762298
Kwa hivyo, asili ya Jicho la Providence ni nini,??
kwa nini inatusugulisha sana???
na kwanini inaunganishwa mara kwa mara na ushetani na makundi ya (Freemason/Illuminati) na hizo nadharia nyinginezo????
Leo tutangalia japo kwa uchache miongoni mwa nadharia hizi kuhusu Alama ya Jicho hilo
TUENDELEE
JICHO KAMA ISHARA YA MUNGU KATIKA DINI (UKRISTO)
Hapo awali alama hii ya Jicho lilikuwa kama ishara ya Kikristo, na matumizi yake yanaweza kupatikana katika kazi nyingi za sanaa za kidini hasa katika kipindi cha Renaissance na alama hii ilikuwa ikiwakilisha Mungu. Mfano wa kazi ya sanaa ya kipindi hiko ni kama ile Tafrija ya Bwana YESU kazi ya mchoraji nguli wa kiitaliano Pontormo ya 1525 huko Emmaus.
Katika mchoro huo unaonyesha Alama ya Jicho hili na inaelezwa ikaangaza katika Tafrija ya mlo huo.
Ilibuniwa kama ishara ya uangalizi wa huruma ya Mungu juu ya binadamu.
View attachment 1762282
Chanzo kingine muhimu cha Alama hii kilikuwa katika kitabu cha nembo kiitwacho Iconologia, kilichochapishwa mwanzo mwaka 1593.
Katika matoleo ya baadaye, 'Jicho la Providence' lilionyeshwa kama sifa ya mfano wa 'Utoaji wa Kimungu', yaani wema wa Mungu kwa waadamu
Na ilibuniwa kama ishara ya uangalizi wa huruma ya Mungu juu ya binadamu.
Lakini kama ujuavyo alama ya jicho hili imeambatanishwa na Pembetatu (Pyramid) katika mingi kati ya mionekano yake.
Hakuna mtu anayejua ni nani aliyeibuni hivyo hapo awali, lakini ni nani aliyeiunda nje ya mipangilio ya kanuni za kidini zilizokuwepo hapo awali. ,,?
Inaelezwa pembetatu ilikuwa ni ishara ya utambulisho ya muda mrefu ya Utatu wa Kikristo ule wa Baba, Mwana na Roho Mtakatifu,
Miale ya mwangaza ambayo mara nyingi huonyeshwa ikitoka kwenye JICHO hilo, inaelezwa pia ni ishara iliyokuwepo hapo zamani ya mng'ao wa Mungu katika taswira ya Kikristo.
Lakini asili ya jicho hilo ni nini???
Huyo huyo Mungu alikuwa ameonyeshwa kwa njia nyingi za mficho hapo awali pia.
JICHO MOJA ISHARA NA ALAMA YA MUNGU WA KALE WA MISRI HORUS.
View attachment 1762292
Lakini walikuwa Wamisri wa zamani ambao inasemwa ndiyo walikuwa waanzilishi wa alama hiyo jicho Waliyoitengeza vyema karne nyingi nyuma.
kwa mfano, Alama za macho zillichorwa kwenye majeneza ya wafu ambayo kwao walikuwa na maana ishara hiyo iliruhusu wafu kuona kupata nuru ya muelekeo katika maisha yao ya baadaye.
View attachment 1762285
Na moja ya alama maarufu zaidi ya Misri ni Jicho la Horus.
Horus alikuwa mungu wa kale wa anga wa Misri ambaye kwa kawaida alionyeshwa kama Ndege(falcon) na mfanano pengine kama wa mbwa mwitu au peregrine.
Jicho lake la kulia lilihusishwa na mungu wa jua aitwaye Ra.
View attachment 1762290
Alama ya jicho hilo la Horus ipo katika muundo wa mchanganyiko wa jicho la mwanadamu na Ndege,,,na lina nyusi pamoja na alama ya shavu.
Kulingana na hadithi za zamani za Wamisri, Mungu-Mfalme Horus ,{mara nyingi huonyeshwa kama Ndege(falcon) au kichwa cha ndege( falcon)} alitolewa macho vitani na mjomba wake Set.
Kwa msaada wa Thoth, baadaye aliponya macho yake Horus.
Na Jicho la Horus, hivyo lilikuwa ishara ya kinga, mara nyingi pia kutumiwa kama hirizi, Watu walikuwa na vijisanamu vidogo vya Alama hiyo vya kutosha kwa mtu kubeba mfukoni mwake kama njia ya ulinzi.
View attachment 1762291
Hii na hieroglyphs zingine za Wamisri kuhusu Alama ya, ziliendelea kuathiri picha za Ulaya za wakati wa Renaissance na kufifisha Alama hiyo kama ishara ya Mungu. Na Wakati huo, wasomi na wasanii walipendezwa na maandishi ya Misri, kuhusu Alama hii nao waliamini kwamba yalitafsiri uwakilisho wa Mungu
View attachment 1762297
Na kuhusu Pyramids kwenye Nadharia hii ya jicho moja kuwakilisha jicho la Horus ikajibiwa ni utambulisho au uwakilisho wa Pyramids za huko misri ambazo zilikuwa ni desturi yao kujenga Pyramids na Kuzika humo miili ya viongozi wao , kuhifadhi vitu vya thamani na mambo mengine na shughuli nyingine nyingi nyingi.
ALAMA JICHO KATIKA VIELELEZO VYA TAIFA LA MAREKANI
Miaka michache mwanzo , mwaka 1782 Muhuri Mkubwa wa Marekani ulionyeshwa
(mfano kwenye fedha na kwingineko)
View attachment 1762294
Thomas Jefferson, Benjamin Franklin na John Adams walikuwa wamependekeza maoni yao juu ya muundo mihuri hio, lakini Charles Thomson, Katibu wa Baraza la Continental (congress), ambaye alikuja na Alama hiyo ya pyramidi na Jicho la Providence, katika ya mambo ya muhuri, kwa kushirikiana na mwanasheria mdogo na msanii anayeitwa William Barton.
View attachment 1762295
Piramidi hiyo katika mihuri hii ya marekani ni ile ambayo haijakamilika (Iliyokatwa juu) ilikusudiwa kuashiria "STRENGTH and DURATION", na Levels 13 za kuwakilisha majimbo 13 asilia ya Marekani.
Alama hiyo ya jicho , pia kama ilivyotumika kwingine kutoka kipindi kama hicho huko Uingereza na Ufaransa na inaelezwa ilikuwa ishara ya kawaida kwa uangalizi wa huruma wa Mungu kwaa mataifa hayo (wanadamu).
Katika moja ya mifano hiyo inaelezwa kulikuwa na Freemasonry/, Illuminanti iliyohusika na uchaguzi wa ishara hiyo na kuziingiza katika serikali hizo.
View attachment 1762299
ITAENDELEA
ALL SEEING EYE, EYE OF
ROVIDENCE - 2
ALAMA YA JICHO KATIKA JAMII ZA SIRI (FREEMASONRY/ILLUMINANT)
NA MAANA YAKE.
daVinci XV
View attachment 1762277
View attachment 1762280
Kabisaa mkuu,Mambo ya Babylon ya Nabukadneza
Kitabu cha Daniel kimeeleza kwa kina.
ReadKwa maneno yako yasiozidi 10 unakipi chakutuambia kuhusu ilo jicho la 3 kama ulivyoandika?
kareebutuko pamoja mkuu
Itabidi tushushe nyingine mkuu ,, ikihusisha vitabu vya ufunuo ,Daniel na MengineyoMambo ya Babylon ya Nabukadneza
Kitabu cha Daniel kimeeleza kwa kina.
Itabidi tushushe nyingine mkuu ,, ikihusisha vitabu vya ufunuo ,Daniel na Mengineyo
Shukraani mkuuWell said mkuu...
Nafukua mambo ya personal and physical presence of God Almighty. Acha tuone inakuwaje!
AiseeeMisri ya kale ndio chimbuko la dini ya kiislamu na kiyahudi na kikristu
Ndio hivyo amri kumi za Musa ni copy and paste ya amri 40 za miungu ya Misri ya kaleAiseee
Mwamba anataka tumpiganie Mungu wa Abraham, Isaac na Jacob. Hajui kwamba huyu Mungu anajipigania mwenyewe. Na hajawahi kushindwa jambo lake.Aiseee