Albert Msando: Wanahabari kuweni watetezi wa Haki za Binadamu, msiegemee upande mmoja

Albert Msando: Wanahabari kuweni watetezi wa Haki za Binadamu, msiegemee upande mmoja

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
525
Reaction score
1,257
Moja.JPG
Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Albert Msando amewataka wanahabari kuendelea kufanya kazi kwa bidii na ueledi zikiwemo za utetezi wa Haki za binadamu ili kuongeza tija katika kuwahabarisha wananchi taarifa zilizojitokeza na zitakazojitokeza.

Msando amesema hayo Mkoani Morogoro wakati akifungua Mafunzo ya siku mbili kwa wanahabari kuhusu namna Bora ya kutoa habari ambayo yameratibiwa na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania -THRDC, Julai 12, 2022

Aidha, Mkuu huyo Wilaya amewataka wanahabari kujitahidi kuwa watetezi wa Haki za Binadamu bila ya kuwa mashabiki wa kuegemea upande mmoja ili kuepukana na changamoto mbalimbali.

Amesema waandishi wa habari wanapozungumza Masuala ya Haki za Binadamu wasiwe wazito kwa kutozitoa badala yake waangalie mzani na ukweli katika kuhabarisha umma juu tukio wanalotaka kuliripoti.

Naye Jaji Mstaafu Robert Makaramba amewasilisha mada ya wanahabari namna ya kuandika na kuripoti habari za kwenye Mahakama kuwa ni vyema wakaepuka kutoa taarifa ambazo hazijatolewa mahakamani ili kuepusha sintofahamu kwenye jamii.
E86A0039.jpg

Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Albert Msando

Awali akizungumza Wakili Kutoka Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu – THRDC, Leopold Mosha amesema mafunzo hayo yamelenga kuwajengea uwezo waandishi wa habari namna ya kuandika ma kuripoti taarifa zinazohusiana na haki za Binadamu.

Wakili Mosha amesema kuwa Moja ya majukumu ya Asasi za Kiraia ni kufanya uchechemuzi wa kujua na kupata ufahamu wa Masuala mbalimbali yanayohusu Haki za Binadamu.
IMG_20220712_101718_848-scaled.jpg
Kwa upande wake Afisa Uchechemuzi -THRDC, Nuru Maro wakati aliwasilisha mada ya Umuhimu wa waandishi wa habari Katika kufanya uchechemuzi kuwa ni pamoja na kufahamu chanzo, ushahidi, kujua watu wengine wanavyofanya kazi hilo eneo husika.
E86A9950.jpg
"Ili kuwe na mabadiliko lazima umma uelewe hivyo ni vyema wanahabari mukaonyesha Umuhimu Katika kutoa elimu kuhusiana na Masuala ya Haki za Binadamu Pindi munapoona Kuna ukiukwaji," amesema Nuru

Hata katika mafunzo hayo ambayo yanatarajiwa kumalizika Julai 13, 2022 wanahabari wamesisitizwa kutumia fursa hiyo kujiongezea maarifa katika ufanyaji wao wa kazi.


Source: Torch
 
Back
Top Bottom