Ali Kamwe: Sababu 8 zilizoifanya GSM kuvunja mkataba na TFF

Kwani kutokuwekwa kwa mabango kulianza lini?

Kama mabango hayakuwekwa na simba basi hapo kumbe Simba ndo walitakiwa wawajibishwe kwa kunyimwa hizo pesa za udhamini na sio kuhusisha Club zingine zilizotii sheria

Unaposema ukikiuka kipengele cha mkataba hauwi halali unatakiwa ujue kuwa sheria yeyote iliyowekwa kama muongozo wa utaratibu fulani inapaswa kufuatwa kama ilivyoandikwa

Sasa kuna sheria ya 16 ya udhamini inasisitiza kua
Nembo ya mdhamini mkuu wa ligi kuu itawekwa kwa rangi zake halisi katika mkono wa kulia kwenye sare (jezi) za timu za kuchezea na timu zitalazimika kufanya hivyo kwa michezo yake yote ya Ligi Kuu.

1.7 Klabu inawajibika kuheshimu masharti ya udhamini wa ligi kuu kimkataba kwenye michezo yake kama navyoelekezwa na TFF/TPLB, timu itakayokiuka itatozwa faini ya shiingi milioni tatu (3,000,000/) kwa kila mchezo itakaokiuka na inaweza kuchukuliwa
hatua zaidi ikiwemo kushushwa daraja na/au kufungiwa.

Kwa maelezo hayo we unaona Yanga kavunja sheria au hajavunja sheria?
 
Katika kusajiiwa NBC nembo yao wameielezea kwa rangi miongoni mwake ni hiyo nyekundu (twiga mwekundu). Hiyo nyeusi mlioweka nyie ni fake. Hiyo nyeusi haitambuliki kisheria.
Wamelalamika?
 
Wamelalamika?
Sio wamelalamika jibu swali je yanga wamekiuka sheria ya mkataba kwakutovaa nembo yenye rangi harisi ( nyekundu) ya mzamini mkuu NBC. Alafu GSM inamana hakupitia sheria nakuona kwamba club itaokataa kuvaa logo ya mzamini itapigwa faini ya shs mil3 ?? Ambayo hio najuwa Simba walikua wanalipa Sasa kwanini yy akomae kwamba mkataba ni vilabu vyote 16 vivae nembo yake.bila Shaka walijua kua hio sheria ipo na iliwekwa kwa inawezekana club ikakataa kuvaa nembo ya mzamini ni endapo itakataa bac hatua itakaochukuliwa ni kupigwa fine ya shs mil3.je hiki kipengele wakati wanaingia mkataba kwann hawakumwambia TFF kua akibadilishe kwamba nilazima vilabu vyote vivae itaoe hicho kinachosema endapo kilabu kikikataa kuvae nembo bla bla.sasa nauliza swali hapo je sheria ingekua endapo timu itakataa kuvaa nembo inashushwa daraja yani hapo hapo hajavaa mechi moja tu shusha daraja huo zikabaki timu 15 je bado GSM asingelipa kwa kukaa kwamba tulikubaliana timu 16. Huu ni uonevu na GSM wanatikiwa walipe haki ya vilabu vilivyo vaa nembo yake myezi 3 Mana katika kufanya mkataba hakuna aliojua Kuna timu itagoma na bado hapo hapo GSM alijua sheria hio timu ikigoma itapigwa fine kwann aliendelea kusaini mkataba wakati anajua hicho kipengele kipo kwenye sheria za uzamini kua kwamba kwahio wao wanalazimisha kwa hakuna Cha kugomaa kuvaa logo Sasa sheria na zann Kama kutakua hakuna back laiti Kama sheria husika itakua imekiukwa
 
Wakati nbc wanaingia mkataba wa kudhamini ligi unafikiri hawakulijua ilo suala la rangi?
 
Huwa unatumia kichwa hata kwa mambo ya kawaida??, Mkataba ili ukamilike lazima terms and conditions Zote zitekelezwe. TFF kashindwa kutekeleza Aliyoyasema kwenye mkataba so far mwekezaji hawezi kuweka pesa. Mo amewahi kuweka ile 20B?
we kichwa mbese kweli bil 20 mbna ziliwekwa halafu kaulize makao makuu ya simba watakwambia ziko account ya benk gani
pia huo mkataba wa tff na gsm umeusoma hadi useme tff kashindwa kuutekeleza

 
we kichwa mbese kweli bil 20 mbna ziliwekwa halafu kaulize makao makuu ya simba watakwambia ziko account ya benk gani
pia huo mkataba wa tff na gsm umeusoma hadi useme tff kashindwa kuutekeleza

View attachment 2114256
Hivi una akili timamu?, Sasa hiki kipeperushi cha TFF ni cha nini? Tunapokwambia TFF anapaswa kujibu na kutoa ufafanuzi juu ya huu mkataba unaelewa maana yake? Au upo kushangilia upuuzi wakitanzania.
 
kwa pesa gani alioweka gsm?
hako ka milioni 3 kwa mwezi ndo tuvae jezi zenye logo ya gsm afu iyo mil3 ni mshahara wa mchezaji mmoja wa simba kwa mwezi utachukuaje hako ka hela hebu changamsha akili yako
Vijana mnaoishi sebuleni kwa mashemeji ZENU mna tabia ya kudharau pesa!!
 
Sema ujinga wako na siyo wetu. Mimi siyo mjinga kama wewe.
 
Simba ina mdhamini wake. Umefikiria hili la simba aitangaze GSM na MO kwa wakati mmoja inawezekana?

Sawa na wewe uambiwe mkeo kumtenbelea mzazi mwenzie nyumbani kwake bila wewe. Utakuwa tayari?
 
Hivi una akili timamu?, Sasa hiki kipeperushi cha TFF ni cha nini? Tunapokwambia TFF anapaswa kujibu na kutoa ufafanuzi juu ya huu mkataba unaelewa maana yake? Au upo kushangilia upuuzi wakitanzania.
huna hoja jamaa wenu chupli chupli utatokwa povu hadi ukome
sindano imekuingia

 
Simba ina mdhamini wake. Umefikiria hili la simba aitangaze GSM na MO kwa wakati mmoja inawezekana?

Sawa na wewe uambiwe mkeo kumtenbelea mzazi mwenzie nyumbani kwake bila wewe. Utakuwa tayari?
Huu ndio ujinga tunaousema.
 
Uhuni tu na kujitoa ufahamu Kama GSM alikuwa anajua simba amejitoa
 
Unahisi wewe upo tofauti na uliyemjibu[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Ama kweli si kila mwenye kichwa ana akili
 
[https://res]

MWENYEKITI wa Bodi ya Ligi Kuu Bara, Steven Mnguto, ameibuka na kusema licha ya wadhamini wenza Kampuni ya GSM kutangaza kujiondoa katika udhamini lakini hakuna klabu yoyote iliyolipwa.


Kauli hiyo imekuja ikiwa ni siku moja tangu GSM watangaze kujiondoa kudhamini klabu za ligi ambazo awali waliingia mkataba wa miaka miwili wenye thamani ya Sh 2.1Bil.


Akizungumza na Championi Jumatano, Mnguto alisema kuwa, hilo suala wamepanga kulizungumza hivi karibuni
mara baada ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) watakapokutana.


Mnguto alisema kuwa, wanasubiria wanasheria wao walipitie suala hilo na mwisho wa siku watalitolea ufafanuzi
kwa undani.


“Kiukweli tangu tuliposaini mkataba na GSM nikiri klabu hazijapata chochote. Klabu zimeitangaza GSM kwa muda wa miezi mitatu sasa, kwa hiyo tunasubiri wanasheria walipitie suala hilo tujue tunafanyaje.

“Hata suala la zile nembo kwenye mabega sijui kama zinaweza kutolewa haraka lakini hata hilo litafanyiwa
kazi kisheria,” alisema Mnguto.

Naye Mkurugenzi wa Habari na Masoko wa TFF, Boniface Wambura, akizungumzia hilo alisema: “Sisi
baada ya kupata barua kutoka GSM, suala la mkataba ni Bodi ya Ligi na ni vema akatafutwa Mnguto lakini
kwa upande wa sisi TFF hatuwezi kuzungumzia kila jambo.


“Tayari tumetoa tamko letu jana (juzi) kuhusiana na hilo baada ya kupata barua GSM.” Juzi TFF ilitoa taarifa
kuwa, Februari 7, mwaka huu walipokea barua ya kuvunja mkataba wa udhamini mwenza wa Ligi Kuu Bara
ya NBC kutoka Kampuni ya GSM, hivyo Shirikisho hilo linafanyia kazi barua hiyo na litatoa taarifa kwa wadau.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…