Ali Kiba Fans' Special Thread...

Nimekumbuka kitu,kuna comment nimeona Mdakuzi kasema Kiba hajamshirikisha Fally Ipupa kwenye remix ya mwana...please nieleweshe vizuri sijaelewa hapo

Wakati Mwana inaanza harakati za kurekodiwa, ilipangwa Fally Ipupa ashirikishwe ili apige verse moja na Kiba apige mbili. Hivyo akasikilizishwa beat na kupewa maudhui ya wimbo wenyewe, mwisho wakakubaliana kwamba Kiba aimbe sehemu yake kisha Fally angekuja kumalizia kutokana na ratiba yake.
Sasa baada ya Kiba kuingiza vocal kwenye sehemu yake ikaonekana kwamba wimbo umesimama sana bila hata Fally Ipupa kuingiza vocal, kwa hiyo ikaonekana kwamba kulazimisha Fally aingize inaweza kuharibu wimbo endapo itatokea bahati mbaya.
Hivyo, Kiba akaamua kufuta mpango wa Fally kuingiza vocal kwenye Mwana na badala yake akatayarisha wimbo mwingine na kumjulisha Fally Ipupa ambaye bila kinyongo akakubali, na moja kwa moja wakashirikiana kwenye wimbo mwingine ambao tayari umesharekodiwa na umetoka mkali ile kinoma.
Ukiisikiliza Mwana ikifika kwenye dakika 2 na sekunde kama 16 hivi, utaona kama kulikuwa na mtu anasubiriwa aingize, drums zinagongwa kwa pamoja na kinanda, kisha Kiba akamtaja Man Water, ambaye akaingiza ile vocal nzito nzito hivi ya 'Umeleta Lawama', sasa sehemu hiyo alikuwa anakaa mtu mzima Fally.
Kwa hiyo huo wimbo ni mwingine kabisa, wala sio Remix ya Mwana, ni wimbo mzuri sana. Fally katenda haki na Kiba ndio usiseme. Beat ni ya Man Water kama kawaida.
Ova
 

Watu kwa kulazimisha kiki. Anajaza watu ujinga wakiamini anadate naye, sasa mwenyewe huyu hapa amekana. Yaani muziki tu ndio utupeleke huku kwenye uzushi na uongo? Hii haiko sawa bwana kuna umuhimu wa kulinda heshima zetu na wengine, imba muziki mzuri watu wataupenda tu, sio lazima ujitangaze kuwa wewe ni malaya.
Ova
 
Diamond platnamz ndani ya mjengo wa big brother right now
Kumbe yupo fit kiingereza,
Fally ipupa kachemka kiingereza anatema kifaransa
 
Huu uzi unakimbiza kuliko maelezo, sasa nataka kufanya christmass bonanza tupendekeze zawadi kwa walioshiriki vyema kwenye thread hii wadada wawili na wakiumeni mmoja.

vp hangover imekwisha?
 

Kabisa,nangoja nione huo mwisho wa drama zake ni upi....
Na hivi wema keshambwaga tena,sina wasiwasi naye tena maana mashabiki maandazi wa wema walikua wananitesa sana....
 
Huu uzi unakimbiza kuliko maelezo, sasa nataka kufanya christmass bonanza tupendekeze zawadi kwa walioshiriki vyema kwenye thread hii wadada wawili na wakiumeni mmoja.
nifah na @ Ms.Lincoln
wa kiume Mdakuzi ndio namkumbuka wengine cna hakika km ni me
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…