Alichofanyiwa Mrisho Ngassa ni uhuni, TFF, TPLB mnawajibika

Ngasa ana hela bado ana nyumba za biashara mwanza na dar anakosaje elfu kumi ya kiingilio,kongole kwa walinzi kazi nzuri wamefanya.
Alipe kiingilio kama wengine
 
Huyu boya alikataa kwenda Sudan acha umaskini umtese
 
Kwanini asilipe...au akitaka bure afuate utaratibu......waafrika tukishakuwa mastaa yaa it's like you have a tick to do whatever......huo Ni ujinga

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Mimi ni mwananchi, lakini pia mshabiki wa Mrisho Khalfan Ngasa. Sijajua chanzo hasa cha huo mzozo!
Ila kama ni kweli mchezaji wetu Mrisho Ngasa alitaka kuingia uwanjani kuangalia mpira, pasipo kufuata utaratibu; mfano kuwa na tiketi kama mashabiki wengine, au kitambulisho maalum! nadhani hapo atakuwa amekosea.

Siamini kama Mrisho Ngasa ni mchezaji wa kukosa hela ya kiingilio. Na kama alitaka kuingia uwanjani kupitia jina/umaarufu wake, hilo nalo ni tatizo. Maana kila mtu akiamua kutumia njia hiyo, nchi haiwezi kusonga mbele.
 
jamani mambo mengie bwana hivi ngasa nae alishindwa kua na kiasi cha pesa alipe tu aingie,mambo mengine jamani tuyaepuke
 
Hilo lapaswa kuwa somo kwa wachezaji woote wapuuuzi, wanaocheza mpira huku wakiendekeza ushabiki kwa timu zao, badala wacheze mpira kama ajira watengeneze kipato wao wanacheza kiushabiki, matokeo wastaaf tuu kipato hawana na club walizokuwa wakizichezea kiushabiki haziwathamini tena
Mfano makubwa ni huyu Ngasa,
Kwa herufi kubwa ALIPE KIINGILIO AKILI IMKAE SAWA NA LIWE FUNDISHO KWA WACHEZAJI WA SASAAA
 
Utaratibu upi, kuna Watu wanapewa Vitamburisho na kuingia bure wakiwa hawajafanya jambo lolote la Maana kwenye Mpira wetu.
Kwani uyo ngasa ili kuaje aende bila utambulisho na anajua una takiwa
 
Bongo mambwiga ni wengi,wakati hayo yanatokea hakukuwa na mashabiki kweli?
Kama kwenye level ndogo kama hii tunashindwa kuchukua hatua sishangai viongozi wa kisiasa kutufanyia utumbo na kupeta
Sisi wabongo tutanyasisika Hadi siku ya mwisho. Mamtu mengi ni zero brain.
 
Azipate kwako wewe unayelialia! Tunapenda vya bure mno
vya bure mwisho wake ndo huo sasa mabaunsa wa getini wanakubeba tupa kule alafu unakuja kulia lia hapa nani akusaidie sasa.lipa kiingilio akuna huruma pale mlangoni.
 
vya bure mwisho wake ndo huo sasa mabaunsa wa getini wanakubeba tupa kule alafu unakuja kulia lia hapa nani akusaidie sasa.lipa kiingilio akuna huruma pale mlangoni.
Kuna kitu huwa kinaniuma ni mentality ya sie! ati hiki kitu nilifanya mimi enzi hizo, tatizo unasahau ulipofanya ulipewa mshahara na mkamalizana na mwajiri. Unataka kuendelea kukamua kama ng'ombe? Mrisho wakati akicheza alikuwa analipwa. Baada ya kutoka uwanjani anakuwa mtazamaji, hivyo lazima alipe kiingilio ili anayecheza sasa apate mshahara. Ukitaka akina Kajole, Sunday Manara, Sunday Juma, Athumani Chama, Zamoyoni Mogella, Dilunga etc wote waingie bure mapato yatatoka wapi?
 
Walinzi wamefanya, wakulaumiwa ni Yanga, na iwe funzo pia kwa vilabu vingine vyote. Watoe at lease ticket za bure za home matches zote kwa legends wao kila msimu ukianza.
 
Dah! Kumbe kuna wakati huwa unakuwa na akili?

Sent from my Infinix X612 using JamiiForums mobile app
 
Uwanja wetu kuna upuuzi mwingi sana, ndiyo maana unaweza kuwa na ticket ya eneo fulani unafika hapo unakuta pamejaa na kwasababu kiwanja chetu hakina namba unaishia kukaa kwenye ngazi,moja ya upuuzi ni hawa wachezaji wa zamani kuingia free bila kadi wala eneo maalum wao wanaenda kukaa popote.Mfano wameingia 20 hiyo ni tatizo tayari.......wengi naona wanalaumu kuona Ngasa hajaheshimiwa ila kama vipi wapewe kadi maalum na eneo lao, tofauti na hapo ni fujo
 
Hakuwa na hela ya kununua tiketi? Utaratibu lazima ufuatwe.
 
Hivi Karia amewahi kucheza soka?timu ipi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…