Alichoniambia mdogo wangu nawaza mpaka sasa nimekosa la kujibu, naombeni msaada wenu

Alichoniambia mdogo wangu nawaza mpaka sasa nimekosa la kujibu, naombeni msaada wenu

Muulize tatizo ni Nini anaweza kupewa dawa hapa hapa ila akupe vipimo tu vya sperm analysis

Ili kama ni ishu ya uzazi ntampa dawa Bure kabisa yaani Bure na ataweza kumpa mimba mke wake na hata hiyo dawa ntaelezea hapa hapa kwa faida ya wengi baada ya majibu ya vipimo ukileta kwahiyo sitaki mtu aje Dm ntaelezea hapa hapa kwa faida ya wengi
 
Mdogo wangu alinifuata wiki moja iliyopita akitaka nimsaidie jambo moja. Huyu mdogo wangu ameoa, ana mke kwa muda wa miaka 4. Anatafuta mtoto naye hawajapata ata kidogo, sasa amekuja kwangu wiki iliyopita anasema anaomba nitembee na mke wake apate mtoto.

Sikuamini macho yagu kabisa, nikaona kama naota vile! Kumuuuliza tena anasema ni kweli ameamua kabisa. Amuulize zile siku za kupata mimba kisha amueleweshe saana mimi nikalale naye apate mimba.

Nimewaza sana sijui nimsaidiaje huyu bwana mdogo, maana yupo na hakika kabisa kabisa. Nimemuuliza je, kwanini asimshirikishe mkewe hilo jambo? Akainijibu nikitaka anaweza muita waje wote tu. Hilo jambo sasa sielewi, je, kweli nimlale mke wa mdogo wangu ili apate mimba? Sielewi maana ni kama ndoto kabisa!

Na mke mwenyewe ni mzuri sana kabisa. Je, nimlale? Je, nifanyeje na mdogo wangu ananikumbusha kila mara kuwa kaka nisaidie jambo langu?


Wake zetu huko nyuma walikuwa na huu utaratibu, wakigundua tatizo ni mume, anamtafuta ndugu wa ukoo au wakuzaliwa tumbo moja anampa mbegu kimya kimya.

Actually mara nyingi walifanya bila hata wahusika kujua, mfano wewe hapo mke wa mdogo wake angekufata tu bila wewe kujua kinachoendelea wala mdogo wako kujua. Hii ilikuwa ni sehemu ya kupunguza tafrani na dharau baina ya ndugu endapo ingejulikana kwamba mmoja ndo amemsaidia mwenzake kuendeleza familia.

Ningekuwa wewe ningepima kwa swali moja tu? Ipi bora kati ya mke wa mdogo wako kuzalishwa na mtu asiyehusika na nyie kwa namna yeyote jambo ambalo linalidhalilisha familia kwani hapo siyo rahisi kutunza siri, na wewe kumzalisha mke wa mdogo wako watoto wakawa damu yenu. Ipi bora?

Hapa ndipo urithi wa wanawake ulipoanzia na hata kwenye Bibilia ambayo mimi siku hizi siamini, utaratibu wa ndugu kurithi mke upo.
 
Niliwahi kuona movie ya aina hii ya Nigeria lakini ilihusisha marafiki wawili. Yule muhusika alimlewesha mkewe na rafiki akafanya yake bila ya mke kutambua ule mpango.

Baada ya muda yule rafiki aliyebandika mimba kwa mke wa rafiki yake alipoteza mkewe halali na watoto wake wawili kwenye ajali na hapo ndipo soo lilipoanza. Kila akikaa alikuwa akimuwaza yule mtoto wa rafiki yake (ambaye ni wake kwa damu) na akaanza kumkera ampe mtoto wake. Ugomvi mkubwa ulizuka na mwisho rafiki akatoa siri kwa yule mwanamke jinsi mpango ulivyokwenda.

Sasa haya unayoongea hapa yamefanana kidogo na hiyo movie kwa hivyo jiwekee tahadhari usije kubadili mawazo baadae.
 
Zaa tu na shemeji yako. Ni bora mtoto awe damu yenu kuliko kuleta damu nyingine katika ukoo wenu. Damu zingine malaana
 
Mdogo wangu alinifuata wiki moja iliyopita akitaka nimsaidie jambo moja. Huyu mdogo wangu ameoa, ana mke kwa muda wa miaka 4. Anatafuta mtoto naye hawajapata ata kidogo, sasa amekuja kwangu wiki iliyopita anasema anaomba nitembee na mke wake apate mtoto.

Sikuamini macho yagu kabisa, nikaona kama naota vile! Kumuuuliza tena anasema ni kweli ameamua kabisa. Amuulize zile siku za kupata mimba kisha amueleweshe saana mimi nikalale naye apate mimba.

Nimewaza sana sijui nimsaidiaje huyu bwana mdogo, maana yupo na hakika kabisa kabisa. Nimemuuliza je, kwanini asimshirikishe mkewe hilo jambo? Akainijibu nikitaka anaweza muita waje wote tu. Hilo jambo sasa sielewi, je, kweli nimlale mke wa mdogo wangu ili apate mimba? Sielewi maana ni kama ndoto kabisa!

Na mke mwenyewe ni mzuri sana kabisa. Je, nimlale? Je, nifanyeje na mdogo wangu ananikumbusha kila mara kuwa kaka nisaidie jambo langu?
Z
 
Niliwahi kuona movie ya aina hii ya Nigeria lakini ilihusisha marafiki wawili. Yule muhusika alimlewesha mkewe na rafiki akafanya yake bila ya mke kutambua ule mpango.

Baada ya muda yule rafiki aliyebandika mimba kwa mke wa rafiki yake alipoteza mkewe halali na watoto wake wawili kwenye ajali na hapo ndipo soo lilipoanza. Kila akikaa alikuwa akimuwaza yule mtoto wa rafiki yake (ambaye ni wake kwa damu) na akaanza kumkera ampe mtoto wake. Ugomvi mkubwa ulizuka na mwisho rafiki akatoa siri kwa yule mwanamke jinsi mpango ulivyokwenda.

Sasa haya unayoongea hapa yamefanana kidogo na hiyo movie kwa hivyo jiwekee tahadhari usije kubadili mawazo baadae.
 
Back
Top Bottom