Katavi Mbuga ya wanyama wakali na hapo Mto Iku ndipo makutanyiko ya wanyama.
SATIVA (Sijui kama ndio jina lake halisi) akubali kwamba Mungu ameamua kubakiza maisha yake "spare his life" kwa namna ya ajabu sana. Nitachambua kidogo kwa uelewa wangu kidogo.
Wauwaji ni wazi walipompiga risasi walijua wamempiga kichwani kulenga ubongo na kama kawaida ya risasi ya kichwa lazima aanguke na apoteze fahamu hata kama ingepiga sikio tuu, hivyo kuwahadaa watekaji wake kama mamemuua.
Na lazima watekaji walikuwa na kiwewe na haraka ya kukutwa na askari wa wanyamapori waliopo hapo Iku maana ndipo kambi yao ilipo, kufuatia mlio wa bunduki hivyo waliondoka upesi eneo hilo wakijua wameua tayari na hasa ukizingatia ni usiku.
Hawakuwa na muda wa kumtizama walijua tayari kazi imekwisha na ndio kupona kwa huyu jamaa. Ni wazi walikuwa na nia ya kumuua sababu walichagua kumpiga kichwani kutoka nyuma, maana kikanuni ukitaka kumuua mtu akiwa amekupa mgongo unampiga kichwa kutoka nyuma, kulenga ubongo wote wa mbele, wa kati na wa nyuma. Ni ukitaka kumuua mtu amekugeukia (anakuangalia) unapiga eneo la moyo ukiwa mbele. Ni nadra kumuua mtu kwa bunduki ndogo kama bastola kutoka nyuma kulenga moyo, risasi maranyingi hujisokota kwenye uti wa mgongo au kuishia kwenye mapafu hivyo kushindwa kufikia vital organs za kumfanya afe maramoja. Hawa ni weledi watu wenye mafunzo maana bila shaka walimfunga pingu nyuma "Handcuffed" na walitaka asiwaone, kumvalisha kitambaa "Blindfolded" na kumpiga risasi ya kichwa wakilenga kumwaga ubongo afe maramoja "Instantly killing".
Kuna mtu nilimsikia anasema, wenda kulikuwa na kujifanya amekufa "Play dead" kuwahadaa watekaji. Sio kweli, bunduki inatabia ya kuvuruga fahamu kwa mlio, nguvu hofu na mstuko mkubwa anaoupata victim hasa kwenye ukaribu "close range", hivyo ilikuwa lazima apoteze fahamu na aanguke hata kama risasi haijamfanyia damage kubwa.
Huyu Bwana ameponea bahati tuu, ni mambo yanatokea marachache sana haya. Kupona risasi ya kichwa kwa muktadha kama huu ni nadra sana bila kujali umakini wa muuwaji wake alikuwa makini kiasi gani. Ni wazi Muuaji alikuwa confident kuwa ameshamuua, na hivi sasa anajiuliza imekuwaje huyu bwana yupo hai hapati pia majibu.
Inasikitisha sana watanzania tunafanyiana namna hii, wangeweza kutumia namna nyingine ya kumtisha huyu kijana mdogo wenda labda alikuwa aggressive sana kushambulia, ila bado walikuwa na option ya namna nyingine ya kumuonya na kumtisha.
Ni sisi tuu kwa karne hii ndio bado tuna mbinu za kizamani za kudeal na watu wetu namna hii, ni mbinu za kipuuzi hazina nafasi kwenye karne hii kwa watu wetu.
This is definitely barbaric, uncouthed and presumptuous way of dealing with our people.