Alichosimulia Edgar Mwakabela "Sativa" kuhusu waliomteka na kumpiga Risasi ya Kichwa

Alichosimulia Edgar Mwakabela "Sativa" kuhusu waliomteka na kumpiga Risasi ya Kichwa

Katavi Mbuga ya wanyama wakali na hapo Mto Iku ndipo makutanyiko ya wanyama.
SATIVA (Sijui kama ndio jina lake halisi) akubali kwamba Mungu ameamua kubakiza maisha yake "spare his life" kwa namna ya ajabu sana. Nitachambua kidogo kwa uelewa wangu kidogo.

Wauwaji ni wazi walipompiga risasi walijua wamempiga kichwani kulenga ubongo na kama kawaida ya risasi ya kichwa lazima aanguke na apoteze fahamu hata kama ingepiga sikio tuu, hivyo kuwahadaa watekaji wake kama mamemuua.
Na lazima watekaji walikuwa na kiwewe na haraka ya kukutwa na askari wa wanyamapori waliopo hapo Iku maana ndipo kambi yao ilipo, kufuatia mlio wa bunduki hivyo waliondoka upesi eneo hilo wakijua wameua tayari na hasa ukizingatia ni usiku.
Hawakuwa na muda wa kumtizama walijua tayari kazi imekwisha na ndio kupona kwa huyu jamaa. Ni wazi walikuwa na nia ya kumuua sababu walichagua kumpiga kichwani kutoka nyuma, maana kikanuni ukitaka kumuua mtu akiwa amekupa mgongo unampiga kichwa kutoka nyuma, kulenga ubongo wote wa mbele, wa kati na wa nyuma. Ni ukitaka kumuua mtu amekugeukia (anakuangalia) unapiga eneo la moyo ukiwa mbele. Ni nadra kumuua mtu kwa bunduki ndogo kama bastola kutoka nyuma kulenga moyo, risasi maranyingi hujisokota kwenye uti wa mgongo au kuishia kwenye mapafu hivyo kushindwa kufikia vital organs za kumfanya afe maramoja. Hawa ni weledi watu wenye mafunzo maana bila shaka walimfunga pingu nyuma "Handcuffed" na walitaka asiwaone, kumvalisha kitambaa "Blindfolded" na kumpiga risasi ya kichwa wakilenga kumwaga ubongo afe maramoja "Instantly killing".

Kuna mtu nilimsikia anasema, wenda kulikuwa na kujifanya amekufa "Play dead" kuwahadaa watekaji. Sio kweli, bunduki inatabia ya kuvuruga fahamu kwa mlio, nguvu hofu na mstuko mkubwa anaoupata victim hasa kwenye ukaribu "close range", hivyo ilikuwa lazima apoteze fahamu na aanguke hata kama risasi haijamfanyia damage kubwa.
Huyu Bwana ameponea bahati tuu, ni mambo yanatokea marachache sana haya. Kupona risasi ya kichwa kwa muktadha kama huu ni nadra sana bila kujali umakini wa muuwaji wake alikuwa makini kiasi gani. Ni wazi Muuaji alikuwa confident kuwa ameshamuua, na hivi sasa anajiuliza imekuwaje huyu bwana yupo hai hapati pia majibu.

Inasikitisha sana watanzania tunafanyiana namna hii, wangeweza kutumia namna nyingine ya kumtisha huyu kijana mdogo wenda labda alikuwa aggressive sana kushambulia, ila bado walikuwa na option ya namna nyingine ya kumuonya na kumtisha.

Ni sisi tuu kwa karne hii ndio bado tuna mbinu za kizamani za kudeal na watu wetu namna hii, ni mbinu za kipuuzi hazina nafasi kwenye karne hii kwa watu wetu.

This is definitely barbaric, uncouthed and presumptuous way of dealing with our people.
Jitafakarini sana kwenye system baadhi yenu mna roho mbaya sana. Tusiuane maana wote tutakufa tu kwa saa na wakati uliopangwa.

Tiss mnajiona mna mamlaka makubwa sana ya kutoa uhai wa watu acheni hizo bwana mida yetu ya kuishi hata kama utakaa sana ni ngumu kutoboa miaka 120.
Tuvumilianeni nchi yetu sote hii.
 
Kwanini polisi walisema hawajapokea mtu huyo kituoni na alifika kwenye karakana na kulala hapo?

Huyo kiongozi aliyefika na V8 na kupigiwa salute ndio mbeba maagizo ya huyu dogo kuuwawa au nae ni mleta maagizo? Na je ninani huyo?

Fanya yote ila kuwa makini na binadamu mwenzako ndio adui yako namba moja. Yan walimpeleka akwe kitoweo cha wanyamapori. SMH!! Gadamn
 
Eti MARANJA NA BONIPHACE wamekuwa tishio kwa watu flani ambao mimi ninawaona kuwa ni dhahifu.
Hizo posho na mafuta waliyotumia hao wa msafara si ni kodi zetu au ni ada za wanachama wao.
Watu ni waoga sana,hadi kina Maranja wanaogopwa kiasi hiki?
 
Tuliokuwa tunaona mbali tulikua tunasema anayofanya Jiwe kuteka teka watu madhara yake watu watakuja kujionea ni jambo la kawaida tu.
Sasa bibi Tukinao wa Kizimkazi anaona watu wake wanayoyafanya. Yeye anajifanyaga mama huruma, mboni hatumuoni kutoa tamko mgonjwa ahudumiwe kwa gharama zake?

Tukiwaambia tatizo kubwa la nchi hii ni CCM mnatuona mapoyoyo. Walaakini wanaopenda CCM ndio mapoyoyo.
Kuteswa imeenza tangu dunia imeumbwa ndio maana hata Yesu aliteswa. Usifikiri imeanza wakati wa Mwamba Magufuli utakuwa unajidanganya na itaendelea hata baada ya Mama kutoka ni mawazo finyu tu kufikiri utesaji umeanza wakati wa Magufuli. Wamarekani wanaendelea kutesa watu huko Gwantanamol mpaka leo. Kitu muhimu tuache kutukana watu ovyo la sivyo tukubaliane na matokeo yake!
 
Eti MARANJA NA BONIPHACE wamekuwa tishio kwa watu flani ambao mimi ninawaona kuwa ni dhahifu.
Hizo posho na mafuta waliyotumia hao wa msafara si ni kodi zetu au ni ada za wanachama wao.
Watu ni waoga sana,hadi kina Maranja wanaogopwa kiasi hiki?
Huwa nashangaa mno watu wazima wanapotumia gharama, raslimali watu na muda ku-deal na jambo dogo kama hili. Na ujue hii kodi yetu ambayo wanasema haitoshi na kukopa wanakopa. Naona huwa wanafanya hivyo ili kujilipa allowance ya ''kuteka na kuzunguka umbali mrefu ili kuua''.
 
Haya watu wenye ajira zenu mkuje hapa, muuaji kabolonga what next to him!? Atauwawa auu atahamishwa kitengo!! Najua baada ya kumuona sativa alivuta fegi nyingi saaaaana ,hajaamini!



Hata hivo nipende kuwapa pole watu wenye ajira za ajabuajabu,najua siyo mapenzi yenu ila mmejikuta ,na mnalazimika kufanya hivyo , rehema na huruma ya Mwenyezimungu iwe juu yenu na hasa nyie mliopo nchi masikini ambako Kuna viongozi ambao wanafikili wao ni miungu,wako juu ya Sheria,
Wauaji hamna furaha japo mnacheka, mna huzuni iliyofichika japo hamuombolezi, mmekuwa wapolee kwa hofu msiyoweza kuielezea, mnatamani kuanza upya maisha ili mchague kada nyingine,ila Tayari mna Siri za watu, mnapewa sifa mtaani,japo moyoni haziwapi amani(mnabaki kusema mngejua),, yote ya yote Mungu si mwanadamu, Bado mna nafasi , kwa namna Gani mnajua wenyewe, ,,,,ila Bado naamini nyie ni watu wenye moyo kama sisi civilians, mnapenda, mnaumia ,mnatamani na mnahurumia ila ndio mshakura kiapo, siwachukiii,

To sativa, wakati wa Mungu si wakati wa mwanadamu, still he has a mission kwa ajili ya Mungu, mwanadamu Hana nafasi kwenye mipango ya Mungu,ata aje na nuke just as what happened in Nagasaki, asante
 
Then what?...uliyeagiza uhai wa mtu utwaliwe sababu una mamlaka?
Kisasi juu yako tunamwachia Mungu, ukiwa umekaa na wanao unakula kunuwa na kusaza ujue kuna siku na wewe utakufa, na utayatolea hesabu yote uliyofanya!
 
Kuteswa imeenza tangu dunia imeumbwa ndio maana hata Yesu aliteswa. Usifikiri imeanza wakati wa Mwamba Magufuli utakuwa unajidanganya na itaendelea hata baada ya Mama kutoka ni mawazo finyu tu kufikiri utesaji umeanza wakati wa Magufuli. Wamarekani wanaendelea kutesa watu huko Gwantanamol mpaka leo. Kitu muhimu tuache kutukana watu ovyo la sivyo tukubaliane na matokeo yake!
Kulikua na haja gani ya kutumia gharama kubwa hivyo kushughulika na mtu kama Sativa ambaye ametekwa kirahisi kabisa?
Tunazungumzia masuala ya nchi. Hata waliomteka Yesu hawakutumia gharama zote hizo.
 
Assassination imefeli, kujisifu sana na kuanza kumuona/kuwaona hao wauaji ni dhaifu, wajinga.. hawana weledi ni mbaya..

Next time atakayetumwa Mission atahakikisha kichwa na mwili vimetengana.
 
Katavi Mbuga ya wanyama wakali na hapo Mto Iku ndipo makutanyiko ya wanyama.
SATIVA (Sijui kama ndio jina lake halisi) akubali kwamba Mungu ameamua kubakiza maisha yake "spare his life" kwa namna ya ajabu sana. Nitachambua kidogo kwa uelewa wangu kidogo.

Wauwaji ni wazi walipompiga risasi walijua wamempiga kichwani kulenga ubongo na kama kawaida ya risasi ya kichwa lazima aanguke na apoteze fahamu hata kama ingepiga sikio tuu, hivyo kuwahadaa watekaji wake kama mamemuua.
Na lazima watekaji walikuwa na kiwewe na haraka ya kukutwa na askari wa wanyamapori waliopo hapo Iku maana ndipo kambi yao ilipo, kufuatia mlio wa bunduki hivyo waliondoka upesi eneo hilo wakijua wameua tayari na hasa ukizingatia ni usiku.
Hawakuwa na muda wa kumtizama walijua tayari kazi imekwisha na ndio kupona kwa huyu jamaa. Ni wazi walikuwa na nia ya kumuua sababu walichagua kumpiga kichwani kutoka nyuma, maana kikanuni ukitaka kumuua mtu akiwa amekupa mgongo unampiga kichwa kutoka nyuma, kulenga ubongo wote wa mbele, wa kati na wa nyuma. Ni ukitaka kumuua mtu amekugeukia (anakuangalia) unapiga eneo la moyo ukiwa mbele. Ni nadra kumuua mtu kwa bunduki ndogo kama bastola kutoka nyuma kulenga moyo, risasi maranyingi hujisokota kwenye uti wa mgongo au kuishia kwenye mapafu hivyo kushindwa kufikia vital organs za kumfanya afe maramoja. Hawa ni weledi watu wenye mafunzo maana bila shaka walimfunga pingu nyuma "Handcuffed" na walitaka asiwaone, kumvalisha kitambaa "Blindfolded" na kumpiga risasi ya kichwa wakilenga kumwaga ubongo afe maramoja "Instantly killing".

Kuna mtu nilimsikia anasema, wenda kulikuwa na kujifanya amekufa "Play dead" kuwahadaa watekaji. Sio kweli, bunduki inatabia ya kuvuruga fahamu kwa mlio, nguvu hofu na mstuko mkubwa anaoupata victim hasa kwenye ukaribu "close range", hivyo ilikuwa lazima apoteze fahamu na aanguke hata kama risasi haijamfanyia damage kubwa.
Huyu Bwana ameponea bahati tuu, ni mambo yanatokea marachache sana haya. Kupona risasi ya kichwa kwa muktadha kama huu ni nadra sana bila kujali umakini wa muuwaji wake alikuwa makini kiasi gani. Ni wazi Muuaji alikuwa confident kuwa ameshamuua, na hivi sasa anajiuliza imekuwaje huyu bwana yupo hai hapati pia majibu.

Inasikitisha sana watanzania tunafanyiana namna hii, wangeweza kutumia namna nyingine ya kumtisha huyu kijana mdogo wenda labda alikuwa aggressive sana kushambulia, ila bado walikuwa na option ya namna nyingine ya kumuonya na kumtisha.

Ni sisi tuu kwa karne hii ndio bado tuna mbinu za kizamani za kudeal na watu wetu namna hii, ni mbinu za kipuuzi hazina nafasi kwenye karne hii kwa watu wetu.

This is definitely barbaric, uncouthed and presumptuous way of dealing with our people.
Huyu dogo ni mtukanaji tu, hakua na impact yoyote ya kusema wamuue, wametumia utamu tu wa madaraka kufanya hivyo.

Huyu cha kufanya ilikua kumchukua unamfungia kwenye chumba cha giza kimyaaa huku unaweka bastora kwenye friji. Ikipoa kabisa unaichukua kisha unawasha taa unamuwekea mkunduni kisha unampa onyo kwa ugali kisha unamuacha aendelee na safari zake.
 
Soma vizuri nilichoandika
Umeandika:
''Napinga kabisa watu kutumia mamlaka na silaha kunyamanzisha watu wanaopingana nao kiitikadi au kisiasa
Ila huyu dogo nae Hana adabu hata kidogo, nimepita page yake ya Twitter ni kichefuchefu kijana ana matusi ya nguoni mpaka kero''
Hii sehemu ya pili ndiyo yenye mushkeli. Maneno ''ila huyu dogo naye...'' yanaonyesha kuwa alichofanyiwa kinahalalishwa na matusi yake. Njia sahihi unaweza kuandika
''Pamoja na kuwa alikuwa anatukana sana.... lakini hii haihalashi kufanyiwa ....''
 
Umeandika:
''Napinga kabisa watu kutumia mamlaka na silaha kunyamanzisha watu wanaopingana nao kiitikadi au kisiasa
Ila huyu dogo nae Hana adabu hata kidogo, nimepita page yake ya Twitter ni kichefuchefu kijana ana matusi ya nguoni mpaka kero''
Hii sehemu ya pili ndiyo yenye mushkeli. Maneno ''ila huyu dogo naye...'' yanaonyesha kuwa alichofanyiwa kinahalalishwa na matusi yake. Njia sahihi unaweza kuandika
''Pamoja na kuwa alikuwa anatukana sana.... lakini hii haihalashi kufanyiwa ....''
Hio ni tafsiri yako
 
Back
Top Bottom