Aliondoka kwa First Class ila Karudi Kama Mzigo Kwenye Ndege

Siku yako ikifika basi imefika

Hata wewe waweza kwenda kwa miguu au kwa gari hospitali na ukarudi ukiwa kwenye boksi

Kufa ni lazima tutakufa
 
Hakuna cha kufikirishq hapa, ni sawa tu na binadamu yeyote akitoka nyumbani kwenye kazini akigongwa na gari! Atapikelewa nyumbani akiwa kama mwili/mzigo!

Tuache kukuza mambo.
 
Kuzaliwa ni njia ya kuingia duniani na kufa ni njia ya kutoka duniani.
 
Inashangaza sana binadamu wanapenda waende mbinguni ila wanaogopa kufa

Kwa suala la kufa; watu wanaogopa kwa sababu wanajua kabisa hawajafanya matendo mema kama yalivyo himizwa na Mungu kupitia mitume wake; sasa watapendaje kukutana naye wakati wanajua ni wakosefu?
wanasema ni bora hapa duniani unapajua tayari, huko kwa Mungu hakuna aliyerudi hivyo kunaogopesha sana!
 
We kijana wa Swissport badala ya kushughulika na kinachokupa chakula unaanza kupigapiga picha,kwani cha ajabu hapo ni nini,?kwenye kitabu cha muhubiri,mhubiri anasema anavyokufa mwerevu ndivyo anavyokufa mpumbavu, vivyo hivyo anavyokufa mtenda maovu ndivyo anavyokufa mtenda mema...So acha kutafakari jambo ambalo halikwepeki live your life kijana
 
Kwa suala la kufa; watu wanaogopa kwa sababu wanajua kabisa hawajafanya matendo mema kama yalivyo himizwa na Mungu kupitia mitume wake; sasa watapendaje kukutana naye wakati wanajua ni wakosefu?
We bwana acha zako,huyo Yesu mwenyewe mtenda mema mashuhuri aliogopa kifo,kumbuka pale Gathemane mpaka alitoka jasho la damu,mpaka aliwaomba wanafunzi wake kesheni muombe pamoja nami, mpaka ali confess "roho i radhi lakini mwili ni dhaifu"hii kauli ilionyesha uoga wa kukikabili kifo
 
Hapo kilichokushangaza ni hiyo ndege kubeba mzigo mbona watu wengi wanakufa kwenye hizi hospital zetu au kifo kinakua kinashangaza kikipata aina fulani ya madaraja...
 
mama mchungajiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii nakuja unitoe mapepo ya kuwawazia kifo watu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…