Alipokuja papa Paul wa pili nchini, aliiweka hii nchi chini ya Bikra Maria ndo maana nchi ina baraka tele

Huyo Bikra Maria ndiyo nani?
 
Mungu ndo alimfanya bikra siyo binadamu. Ukiwa na roho mtakatifu utajua hilo ila ukiongozwa na akina mwamposa kamwe hutafunuliwa fumbo hili
Wewe inahitaji msaada mkubwa Sana nikushaur kama unataka kufanikiwa katika ulimwengu wa roho katika ukristo wako acha kuomba kupitia Bikira Maria hakuna mahali Biblia imempa nafasi ya kuombwa chochote akusaidie kama unalo andiko liweke hapa namm nitakupa andiko linaloonyesha nani anapaswa kuombwa
 
Soma vizuri biblia. Biblia imeandikwa kwa mafumbo na mifano. Alipokuwa mjini kana watu walipitia kwa bikra maria ili kumfikia yesu ili awape pombe(divai)
 
Mungu ndo alimfanya bikra siyo binadamu. Ukiwa na roho mtakatifu utajua hilo ila ukiongozwa na akina mwamposa kamwe hutafunuliwa fumbo hili
Wewe si unafaham kiswahili ? Thibitisha kupitia Biblia kuwa yeye Bado ni bikra.
Kingine nakukumbusha Mungu hatetewi anajitetea Mwenyew ndio maana Kuna baadhi ya dini zinasemaga wanapigana kwaajili ya Mungu kana kwamba huyo Mungu mwenyew hawez kujitetea

Sasa weka andiko linaloonyesha kuwa Maria Bado ni bikra namm nitakupa andiko linaloonyesha yeye sio bikra
 
Huu utumbo una mchanga
 
Ni bikra kwa sababu mimba aliyoipata ni kwa uwezo wa Mungu siyo binadamu na hakuwahi kukutana na mwanamme yoyote na hajawahi mpaka anapalizwa mbinguni mwili na roho
 
Yule Papa alipokuja wapare wakamuomba akifika Mbinguni akafute amri ya kuzini.

Wachaga wakamwomba akafute amri ya kuiba.

Alikataa.

Nchi ina neema ni kwa vile lile sanduku la agano la Mungu lilifichwa humu.
 
Ni bikra kwa sababu mimba aliyoipata ni kwa uwezo wa Mungu siyo binadamu na hakuwahi kukutana na mwanamme yoyote na hajawahi mpaka anapalizwa mbinguni mwili na roho
Wewe unafahamu kama Maria alikuwa na watoto wengne? Ukiachana na Yesu nijibu Hilo swali kwanza na kama hujui basi tusibishane soma Biblia kwanza uimalize mwanzo Hadi ufunuo walau mara 3 ndio ulete hoja mezani

Bila shaka utakuwa ni roman mnakasumba Moja yakutotaka kujua ukweli mmebaki na habari mlizopewa na hamtak kujifunza

Leo nakupa swali fikirishi na usinijibu ila Lile la juu kuhus maria kuwa na watoto wengne nijibu

Swali: Kama Maria unafikiri anastahiri kuwaombea na ananafas kubwa kubwa mlizompa kilikuwa na haja gani ya kuzaliwa Yesu kwanini asingeachwa yeye maana Kwa Roman mambo yote yapo chini yake. ?
 
inafuatana na uelewa wako kuhusu Bikra .. Bikra ni nomino mkuu. ni kitu.. na siyo hali ya kuto ingiliwa.. kwa hiyo kile kitu "bikra" ambacho hata baisikeli tu inatoa.. hakikutoka ... kilibaki hata baada ya Yesu kuzaliwa... ni sawa na kusema mbona ukivaa miwani una ona mbele.. kwa hiyo miwani siyo kizuizi..
 
Hukuwa na sababu ya kuja na hii mada kama kweli wewe ni Mkatoliki kama nilivyo mimi. Maana utasababisha tu kejeli na matusi kutoka kwa watu wasioikiri imani ya Kanisa Katoliki.
 
Ni bikra kwa sababu mimba aliyoipata ni kwa uwezo wa Mungu siyo binadamu na hakuwahi kukutana na mwanamme yoyote na hajawahi mpaka anapalizwa mbinguni mwili na roho
Mathayo 13:
(Matthew)

55. Huyu si mwana wa seremala? Mamaye si yeye aitwaye Mariamu? Na nduguze si Yakobo, na Yusufu, na Simoni, na Yuda?
---------------
Is this not the carpenter's son? Is not His mother called Mary? And His brothers James, Joses, Simon, and Judas?


56. Na maumbu yake wote hawapo hapa petu? Basi huyu amepata wapi haya yote?
---------------
And His sisters, are they not all with us? Where then did this Man get all these things?"

Umesema Hadi anapalizwa hajawahi kukutana na mwanaume unawez ukaniambia Hawa kina yakobo na dada zake Yesu walizaliwa Kwa njia Gani?

Kaa chini soma Biblia acha kukariri vitu bila kujua ukweli, au unataka nkuulze pia ni wap huyo maria alipalizwa kwenye biblia maana waliopalizwa wameandikwa Eliya alipaa, henoko alipaa Yesu alipaa na maandiko yapo Wewe unalo andiko linaloonyesha alipokuwa anapaa?
 
Kweli ww ndio kabisa Bora Hata mleta mada soma comment zangu zote nmekupa Hadi watoto wengine ambao maria alizaa halaf unakuja kuniambia bikra ni kitu sio Hali may you define the term Virgin? Halaf Baki na majibu yako
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…