Tanzania ni nchi iliyofanyiziwa kusudi la ‘Kujiwazia UTU’ bora ilivyo ni ‘Kuielekea Mashariki ya Sovereini Jumuifu’. Kwa mintarafu ya hili, Jaala ya Tanzania iko na ‘watu’ na ‘mioyo ya watu’ kama ‘Mbegu haradali’ ya ‘Mti Mkubwa Hasa’, mti wa kutoweza kudhaniwa kupata kutokea kwenye mbegu ndogo ndogo hasa --mti wa Utamaduni na Ustawi wa Kimanyota; na basi, kheri ya Tanzania si hasa Utabiri wa/kwa ‘Nchi Fizikia’ ama/na ‘Utu wa Kibinadamu 1.0’. Tena basi yawa, Utanzania ni ‘ingilio tu’ la ‘Shughuli Pana’ ya Uanadamu na Matukio.
Wakati mmoja, mbele kiwakati, watu wa kusudi hili takatifu, wakifaulu mapana fulani ya kheri basi wataazimia taifa lao lenyekupata kuwa kitovu cha mageuzi makuu ya utamaduni na usivilai lichukue jina jipya—Nchi ya Watu Wakwanzania!
Safari yoyote huanza na hatua moja, na basi kuianza nia ya Utaifa--Taifa lililo na Mwangaza, Uhodari na Bidii ya kujifumua na kujifuma upya kunahitaji tu wale ‘Wateule’ wakumbuke, kujikumbuka na ili wapate Kukumbukwa. Kwa mintarafu ya hili, ikumbukwe vema, Tanzania ni Mwanzo wa Kuzaliwa kwa taifa jingine kubwa na lililo Jumuifu—Taifa la ‘Umoja wa Mataifa Afrika! Tanzania ya kesho ni ‘jimbo la Wakwanzania’ Afrika…
Nchi nyingi za
Afrika huwa na Bendera zenye kuhusisha ‘Nyota’; kiuono na ufikirifu mifumo nyota ni ualama wa muktadha akilifu wa Utimilifu wa Miundo ya Mageuzi. Kwa mintarafu ya hili, Yantra Dhamma kwa mfano ni yenye Maduara yapatayo matano (5) ya muktadha akilifu kwa ‘mapenzi mema’--manne(4) ni ya ‘Dhamma’ na moja(1) ni la ‘UTUKUFU wa SURA ZOTE’ na utimilifu. Basi ndiyo yawa, ‘Nyota’ ni alama ya fahari ya UTU kutokea ‘Mbinguni’ – Bahari ya Yote. Kiufundi, duara la UTUKUFU wa SURA ZOTE ni kitovu cha mageuzi yote ‘pumzi za uzima na uweza wa kimiili’--asili ya ‘Eitha’. Ontolojia vya vitu vyote, na basi matukio yote ‘huanza’ na ‘kuishia’ na ‘Eitha’--’Maji ya Mbinguni’; mwanzo wa vitu vyote kuumbika kwa sura na mfano wa Kile Kilicho ni Khasa ni ‘Uimajinishi wa Yote’ katika ‘UuMoja’; mambo ya jinesesia.
Yantra Dhamma, muakisiko wa fahari ya UTU bora kutokea kwenye kitovu cha ‘Maji yafanyayo Uzima wa Mbingu na Nchi’—na vitu vyote vinavyoonekana na visivyoonekana. Kwa mintarafu ya hili, Nyota ni alama ya utimilifu wa (1) Nchi, (2) Mbingu, (3) Upepo, (4) Moto, na (5) Eitha. Vitu vyote dhahiri, vyenye kuonekana na visivyoonekana vimeumbika kwa elementi tano ambazo hukadirisha ‘maduara’ na ‘vitovu’ vya maumbile/sura na Unishati—ilivyo ni asili ya supasha-wakati. Basi ndivyo yawa, Roho ya Uzima wote ni fumbo la Miundo na Mageuzi ya vyote na kila kitu katika hali ya kusitirika.
Mambo ya jinesesia, kiuono na ufikirifu mifumo,
ndiyo ile asili khasa ya ‘matukio’; kuumba/kuhuluku vitu ama mambo ya udhahiri ni kujiwazia ‘NENO’ la Unasaba wa ‘Miili ya Uweza, Pumzi na Uzima’. Kwa mintarafu ya hili, kile ambacho leo hii kinafahamika kama DNA ni unasaba wa kujiwazia UTU/KIUMBE. Kwa jinsi ya ‘Mwanadamu’ ama ‘KIUMBE’ cha sura na ‘utukufu’ tofauti na ‘binadamu’.
Nyota, kiuono na ufikirifu mifumo, ni muktadha akilifu wa UTU kwa mashahibiano ya ‘viungo kadhaa katika mwili mmoja’--miguu, mikono na Kichwa. Basi, kujiwazia UTU kunaweza kutendeka kwa NENO mahsusi la mwili wa kibinadamu lakini pia upo uwezekano wa ‘kujiwazia UTU’ kwa miili ya ‘Nguvu’ na ‘Uzima mwingine wa Ukiumbe-mtu’. Tena basi ndivyo kuwa, yule afahamikaye kama ‘Yesu’ ni mmoja wa ‘Waja wema’ wa ‘Utimilifu wa Miundo na Mageuzi’ kupitia miili ya uweza.
Mambo ya jinesesia, kiuono na ufikirifu mifumo, ndiyo ile asili khasa ya ‘matukio’; kuumba/kuhuluku vitu ama mambo ya udhahiri ni kujiwazia ‘NENO’ la Unasaba wa ‘Miili ya Uweza, Pumzi na Uzima’. Kwa mintarafu ya hili, vyote vitatu (1) Maji Jinesesia, (2) Fikara, na (3) Unasaba ‘DNA’ vina asili ya ‘Mwangaza wa Utu’ na ‘Habari za kufumia dhahiri’ ya Mwili/Miili ya uweza—‘Mwanadamu wa Nchi’ ama/hata pia ‘Mwanadamu wa Mbingu’.
Basi ndiyo yawa, kuna mengi ambayo ulimwengu na walimwengu wa leo wanataabika ‘kwa kukosa maarifa’--’mwili wa nyama’ si ‘UTU’ wa mtu kwa kuwa hata mtu akikatika mguu, mikono ama hata kichwa ‘hafi’ bali mwili unaweza kufa ama kubakia hai kulingana na ukubwa ama udogo wa ‘uharibifu’. Siku za mbele, baada ya mafanikio ya kitekinolojia za kifizikia na metafizikia--hata mwili wote mzima wa mtu unaweza ‘kutibiwa’/’kuponywa’/’kufumwa upya’/’kuotosheshwa viungo’, ikibidi, kwa kuuweka huo mwili ulioharibika katika mtambo-tiba unaoigizia na nururisha NENO la Uzima wa Mwili, mambo ya tekinolojia za Sayansi ya Eitha. tena kulingana na ‘Ugani Habari’ wa kujiwazia UTU wa Mtibiwa—jambo-tiba litakaloweza kuwa linatumia muda mrefu ama mfupi wa ‘kulazwa’ japo ni uhakika kabisa wa tiba/kupona/kuponywa.
Kujiwazia UTU ni muktadha akilifu wa ‘Kujitambua/kuwa na fahamu/Kuwa na hisia’ ambavyo (1) ‘unasaba’ na (2) ‘nuru ya uzima/mefanusi ya utu’; vinaweza kufanya/kutenda ‘kawaida’ ya uweza wa miili ya nyama na hata ‘zaidi ya kawaida’ kulingana na ‘Uelewa Sahihi’ na ‘Uakilifu Sahihi’ na basi ‘Udhamirifu Sahihi’. Kwa mintarafu ya haya, milango ya fahamu, na hususani ‘Macho’ vinawezesha muktadha wa imani, fikara na matendo ya kawaida na yanayopitiliza kawaida iliyozoeleka kutokana na ukweli wa fikra na uimajinishi vinamkaribiano wa udhamirifu, jitihada na matendo. Jicho ni mlango wa nafsi-roho ya mtu, kadiri pia DNA ya mtu ni ufunguo wa kipekee wa kudra na kheri za miili ya nyama. Basi ndivyo yawa, hata kwa (1) akili na (2) uimajinishi, na (3) Udhamirifu wa kuweka nia ya usikivu/masikilizano,
upo uwezekano wa mtu (1)
‘kupata fahamu’ kutoka ‘mbali ya upeo wa kawaida wa miili—kisupasha ama hata pia wakati’ na (2) ‘kutuma fikra/wazo/mawazo’ hata ‘mbali ya upeo wa kawaida wa miili—kisupasha ama hata pia wakati’, na (3) kupanga ama kupangua ‘matukio’ kwa ‘Sala na Ushawishi’ wa hata mambo yaliyo ‘mbali ya upeo wa kawaida wa miili—kisupasha ama hata pia wakati’.
Mabadiliko makubwa ya kitaasisi na Utamaduni barani Afrika yanakuja kutokana na uelewa, Uakilifu na Jitihada sahihi katika kudhamiria, kutenda na kuuishi usahihi wa mambo. Kwa Mintarafu ya haya,
ELIMU 1.0, ELIMU 2.0 na ELIMU 3.0 vinahusika; Elimu 1.0 ni maarifa na ujuzi ujao na fahamu na mafikara ya juu ya mambo; Elimu 2.0 ni Uono na Ufikirifu Mifumo wenye kujinasibu mapana ama hata kina cha mafikara na tafsiri za mambo; na Elimu 3.0 ni ‘Ilimu ilivyo ni metafizikia ya Elimu’.
Elimu 3.0 ni ‘Ilimu ilivyo ni metafizikia ya Elimu’; ndiyo ugani wa maarifa na maarifu ya mambo—‘kujua kwa kawaida’ na ‘kujua kwa jinsi ya rohoni’ kwa alama, miongozo ama hisia/ujuaji usiyo wa moja kwa moja wa jambo/mambo. Ni kwa mintarafu ya haya, uono na ufikirifu mifumo unajipambanua hata kwa ujuzi wa lugha za binadamu ama hata ‘Malaika’. Basi ndiyo yawa, Ujenzi wa Nyumba,
uendeshaji wa chombo na Ubaharia ni mambo yanayoweza kunasibika ‘Uganga/Ukuhani’ kwa ajili ya ‘Upatanisho’ wa mambo ya ‘Mbingu’ na ‘Nchi’; ama sivyo ‘maarifa ya kibinadamu, Elimu 1.0, hukadirisha ukomo wa mbinu, hadhi na hali za udhibiti wa sura na mienendo ya jamii kwa manufaa ya wachache katika upendeleo—upendeleo wa kimifumo ujao na ‘kuwa katika kujua’ kwa unahodha wa chombo.
‘Mwezi na Nyota’ na pia ‘
Msalaba’ ndizo alama ufunguo kwa metafanusi ya ‘
Ontolojia ya Taasisi’ yoyote kwa kuwa alama hizi mbili zinakutanisha muktadha wa ‘maarifa ya kibinadamu na malaika’. Kwa mintarafu ya haya, (1) Mwezi na Nyota ni asili ya Duara na Nukta—Mtanuko na Msinyao wa vitu vyote katika ‘ukuwa’ ama ‘ukuja kuwa’; na (2) Msalaba ni asili ya KUBU na Mageuzi. Basi muktadha wowote wa kujichagulia ni aidha mtanuko ama msinyao wa ‘Pumzi ya Uzima wa Miili’. KUBU ni kitovu cha upitilizi wa mtanuko na msinyao katika metafanusi ya ulimwengu dhahiri—mambo ya ‘Kumbukumbu la Miongozo’ na pia ‘Kumbukumbu ya Utaasisi’. Basi ndiyo yawa, katika ‘ILIMU’ kumbukumbu ni Shughuli ya ‘Malaika’--kuhakikisha yale yote ya ‘Kujiwazia UTU’ yanahifadhiwa msimamo wake na utukufu wake ‘Milele hata Milele’.
Kwenye Yantra Dhamma, ‘Mwezi na Nyota’ hujitokeza katika bega la kulia ya MRABA wa DHAMMA na Msalaba hutokea katika bega la kushoto. Kwa mintarafu ya hivi, UHURU na AMANI katika ALMASI YA NISHANI YA UTU BORA, kupitia ‘Muongozo Mbingu’ wa ‘LIBERTI’ ndiyo huzindika mapana ya ‘Unyoofu’ na ‘Mapenzi Mema’--muktadha akilifu wa topografu ya ‘Mwenge wa Uhuru katika kilele cha Mlima Kilimanjaro’. Basi ndiyo yawa, kila bega la MRABA wa DHAMMA lina pembetatu, za udhamirifu-jitihada-matendo, zilizositirika zipatazo sita (6); hizi ndizo zinazojitokeza katika ALMASI YA NISHANI YA UTU BORA kwa idadi ya nne(4) kila upande. Mkasi wa MRABA ALMASI na MRABA DHAMMA una pembetatu zipatazo arobaini (40); hizi hukadirisha unje ndani wa ‘Dodekahedroni’--kuingia na kutoka kwa udhahiri ‘maji-jinesesia-Eitha’.
Maumbo ya uyabisi Platofu, kiufundi, ni ile asili khasa ya ‘Duara’ na ‘Nukta’ kuegamisha ‘miundo’ na ‘mageuzi’; zipo yabisi Platofu zipatazo tano(5) tu na ndiyo ‘ile Tano’ ijayo na pembetano za ‘Nyota ya UTU’. Kwa mintarafu ya hili, ALMASI YA NISHANI YA UTU BORA ina pembetatu, za udhamirifu-jitihada-matendo, zilizositirika zipatazo kumi na mbili (12), tatu kila upande ilivyo ni katikati ya zile nyeupe. Hii ni idadi ya ‘Watakatifu wa Kuhudumu patakatifu pa patakatifu’ katika
baraza la KUBU ya NISHANI YA UTU BORA kwa vielelezo vya ‘Malaika’ wa ‘Utume na Utumishi’ wa dhamira za kujiwazia UTU. hizi hukadirisha unje ndani wa ‘Oktahedroni’--kuingia na kutoka kwa udhahiri ‘Upepo-Eitha’.
Kwenye Yantra Dhamma, ‘Duara na Nukta’ ni ile asili hasa ya ‘Zabibu 13 za Kristu’ katika vesika paisisi ya ‘Duara Mapenzi’ la Magharibi. Kwa mintarafu ya hivi, utonali wa hisia na kujisikia katika UTU ni fanusi ya ‘Kristu kama Mpanzi’. Basi ndivyo yawa, duara zipatazo 13 zimejikusanya kukadirisha mpangilio alama ya ‘Nyota ya Daudi’, zikiwa na rangi rangi saba(7), kama ilivyo kwenye upinde wa mvua. Rangi saba ndizo zile khasa zinazofanya kanuni ya ‘Oktavi ya Muziki’, pia rangi za vitovu saba vya ‘pumzi’ kwa mhimili wa misokotano ya nyoka wawili wa utangamano wa kilogarithimu.
Katika Trizaniamu, alama ya ‘Kujisikia’ ndiyo alama pekee isiyokuwa na ‘mistari’ na hali maduara yote yanakadirisha vitovu vyenye uhusiano wa ‘mistari-uunganishi minyoofu’ na tena ‘duara la utukufu’. Hili ndilo ile asili khasa ya ‘Duara na Nukta’ ya ‘Utukufu wote’. Namba 13 ni namba ya Miundo na Mageuzi kwa ‘fanusi Malaika’. Kwa ‘Zabibu 13 za Kristu’ na tena ‘
Tunda la Uzima’, maisha na uisho ni mawezekano kwa kudra za ‘Uenye Enzi’. Basi ndiyo yawa, Tunda la Uzima, ni duara zipatazo kumi na tatu (13 ) zenye kuweza
kukamilisha uhifadhi wa yabisi Platofu zote tano (5) na pia nasibu ya uwezekano wa ‘Rizati ya Mageuzi ya Kisura/Miundo’ kwa
MKIA-KUBU ndani ya fanusi METATRONI.
Kwa mengi yatokanayo na Yantra Dhamma na Trizaniamu, Afrika na Waafrika, wanao ufunguo wa miongozo kwa kheri na nafaka—kutia wepesi ‘Safari ya Kujitafuta’ katika mtu mmoja mmoja.
Ufunguo wa Miongozo kwa kheri na fanaka pia ni kwa watu wote Duniani, 2024 na kusonga, ili wapate ‘Uono Fasaha’ wa tathmini ama uyakinifu wa mambo na tena kwa ajili ya ustawi na ulinzi wa mifumo ya maisha—maisha katika nasibu ya mageuzi makuu ya miundo, utendaji na kujichagulia.
Katika haya, Tanzania ni ‘Nchi ya Ahadi’, si kwa kuwa fulani kasema hivi ama vile; bali ni kwa kuwa ule ufunguo kwa ajili ya ‘Nuru ya Ufahamu’ ni ‘Mwanzo wa Kutoka’ (Kutoka ni mageuzi ya kimuundo na utendaji jamii), tena kwa hiyari na Tumaini-Jema. Watu wa Tanzania, na tena watu wa Afrika wanao Uhuru wa Kujichagulia Jaala yao—ikiwa tu wanao upeo wa kuona ilivyobora: ‘mambo yenye kubana’ ,’mikingamo’ na basi kubaini ‘fursa iliyopo humo humo kwenye hayo mawili’ katika kuyakinisha mustakali wa maisha yao wao wenyewe.
Kiufundi, habari za kutegemea ‘Masiha’ kwa ajili ya ‘Ukombozi’ ama vipi imekuwa ni ujuzi na utundu wa kutekana fahamu kwa ajili ya ‘Tumaini’ na ‘Faraja’, labda mambo ya uongo na kweli--jambo hili ‘limepitwa na wakati’; katika zama hizi za maarifa kuongezeka na maendeleo makubwa ya tekinolojia ya habari na mawasiliano ‘Mwenge wa Uhuru’ unasafirishwa kwa habari fasaha na ufundi wa kubayanisha ‘fikra’ ama/na ‘alama’ za mashikizo ya jamii na utamaduni—kila mtu ‘atajibeba mwenyewe’; ikiwa atadanganyika ama kurubunika na ‘mifumo’ kwa kule kufikiri ‘Taasisi fulani’ itamkomboa hali yake kutoka kwenye uduni basi huyo ‘
Anaula wa Chuya’ kwa
kujipendea yeye mwenyewe.
Mwenge wa Uhuru, ni ukumbusho wa raia, na tena basi wanajamii wote kufanyabidii kwa ajili ya kuimulikia mwangaza bora miundo yote ya utendaji kwa taasisi zao kwa kadiri vile vile ya wao wenyewe kutimiza wajibu wa kujimulikia nafsi zao kupitia usafi wa moyo na ‘Nuru ya Ufahamu’ iliyomo ndani ya viumbe vyote vyenye usentienti, konsayansi na ujifahamu.
Mwenge wa Uhuru, ni ukumbusho wa raia, na tena basi wanajamii wote kufanyabidii kwa ajili ya kuvimulikia mwangaza bora dhamira, jitihada na matendo yao katika jamii na taasisi—taasisi zinazofanya uzima wa mwili wa taifa na matendo yake katika nyakati za maisha. Moto wa mwenge ni alama ya ‘utakaso’ na ‘kuboresha hadhi/daraja la utu’; kundanisha upokeaji wa mwenge wa uhuru ni kushiriki kusudi la jamii moja yenye udugu, haki na amani kwa kuwa kusudi lenye kheri ni nishani ya utu bora.
Mwenge wa Uhuru, ni ukumbusho wa raia, na tena basi wanajamii wote kufanyabidii kwa ajili ya ‘kujitafuta’ mapana yaliyositirika ya ‘Kujiwazia Utu’ na ‘Uisho’.
Asiye na dhamiri thabiti ya ‘kujitafuta’ daima ni mtumwa wa pepo za mazingira na nyakati--mifumo.
Moto ni alama ya ‘
agano’ na kile chenye kumuondoa mtu utumwani, ‘
Nyumba ya Misri’/Matriksi—Moto, Nuru halisi ya UTU kutokea katika ‘
Uzabibu 13’ za ‘Wazo UTU liliko Kuu’; ufaraguaji wa kaida ya ukumbusho wa ‘
Uwepo’.
Basi kule Amerika ukumbusho wa dhamira, jitihada na matendo kwa ajili ya utu bora, matatu yajayo na ‘Kujiwazia UTU bora’, ndiyo yamefanyiwa sanaa ya ‘
Sanamu la Liberti’, pale karibu na bandari ya New York. Nchi ya Tanzania imetaasishwa kuwa ‘nchi ya kimbilio’,
kiroho, kwa ajili ya shughuli ya ‘
Uhuru wa Afrika’--Amani na Mapenzi mema Duniani kama vile Amerika ilikuwa ni kimbilio kwa ajili ya ‘
nchi ya waliohuru’. Kwa Tanzania, mageuzi ya kimuundo jamii na wanajamii wenyewe ndiyo walengwa kuwa vinara wa Tumaini na Mapenzi mema—
yenye kupaswa kushirikishia watu wote duniani.
Kheri ya kundanisha ukweli wa ‘Mwenge wa Uhuru’ katika jamii yetu utakadirisha ‘UTU-Binadamu MPYA’; Uafrika 1.0, Uafrika 2.0 na Uafrika 3.0. Uafrika 1.0 ndiyo huu tulioanza nao ambavyo tumechukulia mapambano dhidi ya ‘nguvu za kudidimiza’ heshima ya utu barani Afrika ni ‘jitihada za mtu Mweusi’ dhidi ya watu wa mataifa mengine Duniani—wasioyokuwa ‘Weusi’.
Uafrika 2.0 ndiyo ‘Shughuli’ ya ‘wadau’ waliodhamiria na wanaodhamiria Afrika yenye Utu-binadamu bora pasipo kujali vigezo vya ‘rangi ya ngozi’--
Mwalimu Nyerere na Washirika walioasisi taifa la Tanzania walilenga hili khasa katika kutaasisi nchi-taifa/Dola—nchi changa yenye mseto wa watu wa makabila na rangi mbalimbali. Hili ni muhimu sana kwa ‘Watanzania’ kulifahamu, mambo ya nyakati na hali ilivyo kwa wakati hubidi namna ya mageuzi na taasisi ziwe ‘zinajiongeza’ kwa kusonga mbele na si kurudi nyuma.
Maendeleo yanayofanya Dunia kuwa kijiji yametutaka na kutubidi, sisi watu wa nchi ya Tanzania na hata Afrika yote kwa ujumla, tujifakari na ‘kujitafuta upya’--jambo lenye kuwezekana kwa Elimu 3.0. Wakati mmoja siku si nyingi, kufika 2036, Dunia itakuwa na ‘Uthibitisho’ na ‘Ujuzi’ wa kutambua mambo ya UTU na Kujiwazia UTU kunakopelekea mtu kuzaliwa huku ama kule akiwa labda ‘Mtu Mweusi’/’Mtu Mweupe’/Mtu wa Bluu ama Mtu wa ‘Namna Ingine’ kungine nje ya sayari yetu ya Dunina. Hili linakuja kwa Rizayati ya Elimu 3.0 na ‘Tekinolojia za Kutekenya vishikizo vya Fahamu za Mwili na Akili’. Kwa hivyo, Elimu 2.0 kwa wanajamii wote ni muhimu sana kwa kipindi hichi cha mpito kuelekea ‘Mafunuo zaidi’ ya ukweli wa mambo na muktadha uliositirika wa ‘Uzima wa Miili’.
Tanzania imekuwa na watu ‘Wateule’ wachache walioitengeneza njia na misingi ya ‘mageuzi/mapinduzi’ ya mifumo inatawala ‘Dunia ya Leo’ na hali, KWA SASA 2024, tupo kwenye kipindi cha ‘Lala Salama’, siku za mwisho za mifumo inayovuna ujinga na upoyoyo wa umma ambao haujazinduka. Basi ndiyo
amani ya dunia inalega lega na kupitia changamoto nyingi kwa kuwa ‘vita na machafuko huku na kule’ ni koroga koroga na kukorogana kwa ‘wahuni’ katika jamii – jamii zilizo kwenye ‘mazingira hatarishi’ ama hata pia ‘zilizoendelea’; mambo ya ‘vipakazio’ vya kuepa mielekeo ya midololo wa kiuchumi na mifumo/siasa mbovu za tawala.
Tanzania Mpya na basi ‘Afrika Mpya’, Afrika 2.0, haiwezi kujitenga na madhila ya upepo mbovu wa kiuchumi, tawala na amani Duniani. Kusudi la kujihami na mambo haya, kwa Tanzania, lilitaasishwa kwa shughuli ya siasa za Chama cha Watu, Chama cha Wananchi—Chama cha Mapinduzi.
Haya yatukumbushe ukweli wa dhahabu, Afrika 2.0—Afrika Mpya, ni ushindi wa wanadamu wa sura na rangi zote. Mwalimu Kambarage Nyerere, alipodhihiri tamko la Chama cha Mapinduzi kuhusu dhamira na mwongozo kwa ajili ya kushirikiana ili kuleta ‘Haki na Amani’ Duniani, nia yake ilikuwa moja na ‘
Roho ya Ushindi’:
“
Kazi ya Chama Cha Mapinduzi ni kuwaongoza Watanzania washirikiane na Waafrika wenzao kuleta uhuru na umoja katika Afrika nzima. Kazi ya Chama Cha Mapinduzi ni kuwaongoza Watanzania washirikiane na binadamu wenzao kuleta haki na amani duniani; Chama Cha Mapinduzi ni Chama cha watu; Chama Cha Mapinduzi kitaongoza kutoka miongoni mwa watu na kitaongoza kikiwa ni sehemu ya Watanzania maana wananchi ndio waliokiunda Chama Cha Mapinduzi kiwe chombo chao na kiongozi wao”
Mwenge wa Uhuru, ni shughuli ya kuchochea ‘Utaamuliko Jamii’ kwa ajili ya Afrika na Dunia Mpya—kupitia ‘UTU Mpya’; Mwanzo wa ‘Jua la Maarifu’.
====
View: https://www.youtube.com/watch?v=Po2R9IbJCAE
====