Aliyefuta somo la kilimo shuleni achunguzwe uraia wake na kufunguliwa kesi ya uhujumu uchumi

Aliyefuta somo la kilimo shuleni achunguzwe uraia wake na kufunguliwa kesi ya uhujumu uchumi

The Phylosopher

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2015
Posts
1,968
Reaction score
2,957
Kwa nchi yetu kupuuza elimu inayohusiana na mambo ya kilimo lilikuwa kosa kubwa sana lisilosameheka.

Mikoa yote ya Tanzania ukiondoa dar salam msingi wao mkuu wa uchumi na ajira ni kilimo Kwa miaka yote.

Ukanda wetu wa majirani zetu na mataifa mengine duniani wanakabiliwa na changamoto za kiusalama, uhaba wa ardhi, ukame, hali mbaya ya hewa na kutokuwa eneo la kimkakati kama tulivyo sisi, yaani tupo mahali ambapo Kila njia ya usafiri ni rafiki.

Katika mazingira ya namna hiyo unashindwaje kukifanya kilimo kuwa ajenda kuu ya kujikomboa kiuchumi?

Ni kwa nini usikifanye kilimo kuwa ufumbuzi wa tatizo la ajira?

Ukishajijua hivyo unaondoaje somo la kilimo shuleni badala ya kuongeza uwekezaji huko ili lifundishwe kwa kina litengeneze wataalamu watakaoleta tija kwenye kilimo?

Mimi naamini katika nyakati hizi za changamoto za Russia vs Ukraine sisi tungepiga hela sana. Ni aibu sana kwa taifa kushindwa kustabilize kilimo ili kijibu maswali yote magumu ya kiuchumi.

Ndipo nadhani Iko haja ya kumtafuta mtu aliyeondoa somo la kilimo shuleni achunguzwe uraia wake na kufunguliwa kesi ya uhujumu uchumi.
 
Kwa nchi yetu kupuuza elimu inayohusiana na mambo ya kilimo lilikuwa kosa kubwa sana lisilosameheka.

Mikoa yote ya Tanzania ukiondoa dar salam msingi wao mkuu wa uchumi na ajira ni kilimo Kwa miaka yote.

Ukanda wetu wa majirani zetu na mataifa mengine duniani wanakabiliwa na changamoto za kiusalama, uhaba wa ardhi, ukame, hali mbaya ya hewa na kutokuwa eneo la kimkakati kama tulivyo sisi, yaani tupo mahali ambapo Kila njia ya usafiri ni rafiki.

Katika mazingira ya namna hiyo unashindwaje kukifanya kilimo kuwa ajenda kuu ya kujikomboa kiuchumi?

Ni kwa nini usikifanye kilimo kuwa ufumbuzi wa tatizo la ajira?
Ukishajijua hivyo unaondoaje somo la kilimo shuleni badala ya kuongeza uwekezaji huko ili lifundishwe kwa kina litengeneze wataalamu watakaoleta tija kwenye kilimo?

Mimi naamini katika nyakati hizi za changamoto za Russia vs Ukraine sisi tungepiga hela sana. Ni aibu sana kwa taifa kushindwa kustabilize kilimo ili kijibu maswali yote magumu ya kiuchumi.

Ndipo nadhani Iko haja ya kumtafuta mtu aliyeondoa somo la kilimo shuleni achunguzwe uraia wake na kufunguliwa kesi ya uhujumu uchumi.
Mkuu, hata hao wasomi wa SUA, wamesomea kilimo, lakkni wengi wao hawajui kilimo! Tatizo la Tanzania, watu wanasoma ili wasifanye kazi, ili wakaye ofisini! Hata maofisa ogani, hawana cha kumsaidia mkulima, kwa sababu wengi hawajui kilimo!
Hapa Tz, wakulima ni wale ambao hawakusoma na wanafanya kilimo, na waliosomea kilimo ni maafisa wa maofisini, wanaojua nadharia tu, lakini hawawezi kulima hata bustani!
 
Magufuli ndiye aliyepaswa kuwa mfungwa nambari 1 hapo.
1. Yeye katika miaka yake 6 ya utawala pesa alizozipeleka wizara ya kilimo ni ndogo kuliko alizowapatia TEMESA ambayo ni taasisi tu si wizara.
2. Magufuli hakuwahi kuajiri afisa kilimo au afisa ugani katika kipindi chake chote cha miaka 6, badala yake akaajiri maafisa usalama na kuwapandisha cheo wengine huku Taasisi zingine wakisugua benchi.
Magufuli was the baddest president ever
 
Ndio hilo ni sehemu ya tatizo lakini tatizo zaidi nadhani ni mfumo mzima wa nchi kukosa muelekeo.

Bado kuanzia kwa Viongozi wetu mpaka kwa Wananchi kuna imani ndogo sana juu ya kilimo na faida zake.

Ukienda maonesho ya Kilimo wamejaa wauza maplastiki ya kichina.
 
80% ya wanafunzi ni watoto wa wa kulima halafu hawafundishwi kilimo
Kwa sababu mazingira wazazi wao wanayo fanyia kilimo ni mateso, kuanzaia pembejeo, uhaba wa mvua hadi bei duni yq mazao! Wengi wanakulia kwenye mazingira ya kuchukia kilimo, na hata wanaosoma, lengo kubwa ni kuondokana na kazi hizo za ‘mateso’ za kilimo! Kwa hiyo hata wasomi wa kilimo, hawafanyi kilimo na hawajui kilimo!!
 
Nimesoma somo la kilimo lakini halikuwai kua msaada kwangu. Changamoto ya kilimo cha sasa ni fedha na soko.

Mtu unaweza lima sasa ata kwa kujifunza kuhusu kilimo fulani kupitia mtandao. Ata wafunzwe kwa viboko vingi hakutakua na tija yoyote kama hakuna uwekezaji stahiki.
 
Swala si kufuta somo la kilimo maana mpaka sasa zipo shule na vyuo bado zinafundisha somo hlo, swala ni je hao wasomi na wataalam wanatumiwa ilikuleta tija kwa taifa?
Lengo sio tu kuwatumia,tunahitaji watoto wetu wapate msingi imara wa kilimo waweze kujiajiri. Ujuzi walionao wakiutumia wao wenyewe kwanza taifa litasonga mbele
 
Back
Top Bottom