Aliyefuta somo la kilimo shuleni achunguzwe uraia wake na kufunguliwa kesi ya uhujumu uchumi

Aliyefuta somo la kilimo shuleni achunguzwe uraia wake na kufunguliwa kesi ya uhujumu uchumi

Na lengo la elimu ni kujibu changamoto za wakati husika. Kwa taifa kama letu tulipaswa kuwa na maendeleo makubwa sana kwenye mambo ya kilimo ikiwa tungekuwa serious na kilimo.

Tulipaswa kufundisha kilamo na liwe somo la lazima kwa kila mwanafunzi tangia nursery hadi chuo kikuu tulipaswa watanzania wakisome kilimo kwa vitendo Tanzania ilipaswa agricultural transmissional center kwa subsahara region and the rest of the world.

Tuzalishe watafiti na wataalamu wa kutosha wa udongo, mbegu Bora, pembejeo, masoko ya ndani na nje, miundo mbinu ya kilimo cha kisasa na cha umwagiliaji, uhandisi wa mitambo na viwanda vya zana za kilimo nk. Haya yote yanatakiwa kufundishwa kwenye shule zetu zote.

Sio hivyo tu lakni serikali itenge fedha za kutosha kuifanya hii elimu kuwa ya vitendo zaidi badala ya nadharia.
Na ndivyo inavyotakiwa lakini fuatilia huko kite tunakopaongelea leo kwamba ndio leaders WA hii industry katika kuzalisha pembejeo , mazao ya kilimo , vifaa kama tractors ,planters &harvesters , mitambo ya usindikaji WA mazao , tafiti za madawa , mbolea NK , kote huko initiatives zimesupportiwa Kwa kiasi kikubwa na serikali zao .
 
Ndo madhara ya kuwapa uongozi mamluki toka nchi jirani, hapa vetting ilifail
 
Utamfungulia kesi hali ni marehemu kwa sasa.
Joseph Mungai mbunge ambae alikuwa Mkenya mamluki ndie aliyeua elimu kwa interest ya Kenya kuteka soko la ajira nchini.
Alifutaga pia michezo ya umiseta

Mkuu unajua sababu ni nini yeye kufuta

Ova
 
Alifutaga pia michezo ya umiseta

Mkuu unajua sababu ni nini yeye kufuta

Ova
Ili kupata kizazi cha wakata viuoni,huoni Kazi ya kina dada ni kubinua vigodoro kwenye instagram huko
 
Walioitwa kazini ila yakafanyika magumashi.
Wengi wakadhulumiwa ajira zao
Acha uongo na ujinga
2016 tangazo la kazi la maaafisa kilo, alafu kwenye kuajiriwa wakadhulumiwa?
2017 tangazo tena la kazi la maafisa kilimo, alafu kweye kuitwa kazini wakadhulumiwa?
2018 tangazo tena la kazi la maafisa kilimo, alafu kwenye kuitwa kazini wakadhulumiwa?
2019 tangazo tena la kazi alafu kwenye kuitwa kazini wakadhulumiwa?
2020 tangazo tena la kazi alafu kwenye kuitwa kazini wakadhulumiwa?
2021 February tangazo tena la kazi alaafu kwenye kuitwa kazini wakadhulumiwa?
 
Nimesoma somo la kilimo lakini halikuwai kua msaada kwangu. Changamoto ya kilimo cha sasa ni fedha na soko.

Mtu unaweza lima sasa ata kwa kujifunza kuhusu kilimo fulani kupitia mtandao. Ata wafunzwe kwa viboko vingi hakutakua na tija yoyote kama hakuna uwekezaji stahiki.

Tatizo hata wanafunzi wakiwa shule hawapendi haswa kipindi cha kufanya practical
Wanafunzi kutopenda kufanya practical haiondoi ukweli kuwa kilimo kinapaswa kuwa ajenda kubwa sana kwenye taifa letu
 
Utamfungulia kesi hali ni marehemu kwa sasa.
Joseph Mungai mbunge ambae alikuwa Mkenya mamluki ndie aliyeua elimu kwa interest ya Kenya kuteka soko la ajira nchini.
Ikiwa tuna uhakika ni yeye basi kesi ianze mara moja maana huyu atakuwa na mchango mkubwa sana kwenye tatizo kubwa la ajira na uchumi tunalopitia sasa
 
Agriculture mbna ni somo kwa level ya advance, labda ungesema lirudishwe O level.
Hapana kwa O level lilikuwepo tangu muda,kaka na dada yangu wamesoma shule ya Kilimo na somo la kilimo lilikuwepo
 
Ndio hilo ni sehemu ya tatizo lakini tatizo zaidi nadhani ni mfumo mzima wa nchi kukosa muelekeo.

Bado kuanzia kwa Viongozi wetu mpaka kwa Wananchi kuna imani ndogo sana juu ya kilimo na faida zake.

Ukienda maonesho ya Kilimo wamejaa wauza maplastiki ya kichina.
Ukweli mfumo ni mbaya sn
 
Ukweli mfumo ni mbaya sn
Hicho kinachoitwa mfumo nini suluhisho lake maana taifa linateketea.

Lakini nadhani zaidi ya hicho tunachoita mfumo kuna watu wako accountable kufanya maamuzi ambao bila ridhaa yake mambo hayaendi ama yanaenda.

Chukulia mfano kwamba chini ya uongozi wa mtu fulani mnaweza kuwa na mambo moja mbili tatu kama alama ya mafanikio chini ya uongozi wake.

Mfano chadema imekua sana chini ya uenyekiti wa mbowe kiasi kwamba hata wanachadema hawako tayari kumtoa kwenye hicho kiti.

Hivyo naamini hata hili la kuchezea masomo nyeti Kwa taifa Kuna kiongozi ambaye Kwa makusudi mazima aliamua kuidumaza nchi Kwa sababu anazozijua mwenyewe huyu lazima tumtafute ili awajibike Kwa kulihujumu taifa.
 
CCM ni hatari sn
Nadhani pamoja na kuendelea kuilaumu CCM Kwa uharamia huu ni lazima tuinuke Kwa pamoja kupambana na huu uhalifu usiokubalika hata kidogo!

Haiwezekani ukaenda Kwa watu wanaoishi baharini na kwenye maziwa na mito mikubwa alafu ukaondoa study za kukabiliana na mazingira ya maji alafu tudhani ulikuwa na nia njema na watu hao
 
Nimesoma Agriculture Olevel bado sijaona faida yake,zaidi ya kutesa tu watoto mara kuchunga ng'ombe,bustani jembe la mkono na ujinga mwingine mwingi.
 
Back
Top Bottom