Uchaguzi 2020 Aliyejipanga kupora uchaguzi tunamjua, Wananchi tukapige kura kwa wingi kumkataa!

Tuwe wakweli Watanzania wanahitaji heshima na kuthaminiwa.Haya mambo ya dharau na kiburi watawala yanachosha. Neno " Hamtashinda" baya sana halifai kwa taifa la kidemocrasia.
Kwahiyo yeye kama mgombea wa ccm ulitaka aseme kuwa upinzani mtashinda?
 
Wapinzani wanajua kabisa eneo wanalopigwa kila siku. It doesnt matter kura kiasi gani zimepigwa as long as NEC wana model yao ambayo tayari ipo calibrated na equations za kumpa ushindi mgombea wa CCM

VIONGOZI wa Upinzani wanalijua hili vyema but yet wanaingia kwenye uchaguzi ili kulinda matumbo yao (ruzuku etc). Kila mtu anajua kwamba bila Tume iliyo independent (bila mkono wa Rais), ni ndoto CCM kuachia Ikulu
 
Kama wananchi wakiamua kwa pamoja kuuondosha udhalimu huo umapindizu wakafanyie vyumbani mwao
 
Kwani hao wabunge waliopatikana waliopatikana kwa tume ipi.
Tume sio ishu
 
Kwani hao wabunge waliopatikana waliopatikana kwa tume ipi.
Tume sio ishu
Tume ni issue. Tume imepewa mamlaka ya mwisho ya kumtangaza Rais bila kupingwa popote. Why?

Atleast kwenye ubunge kuna chance ya kupinga matokeo mahakamani. Hata hao wabunge wachache waliotangazwa ni kwa kuwa either waliwachapa wapinzani wao kwa kura nyingi mnoo au walikomaa kwa jasho na damu mpaka watangazwe na DEDs.

Kuna watu walipata matokeo yao usiku saa mbili ila wakaja kutangazwa kesho yake saa 10 jioni baada ya figisu lakufa mtu. Haya yote ni kwa sababu tume ni tatizo na inapokea maelekezo kutoka nje ya mifumo yake
 
It is never too late in life
 
Uchaguzi ni wa Wananchi! Uchaguzi ukivurugwa, ni dharau kwa wananchi na si kwa wapinzani!
Heshima yetu kama watanzania ni kuheshimiwa maamuzi yetu kwenye chaguzi! Anayechakachua uchaguzi anatuona tuliopiga kura ni wapumbavu!
Ifike pahala viongozi wetu waache kudharau wananchi.
 
Mkuu, badala ya kulaumu ungeshauri cha kufanya.. Mwaka jana kwny serikali za mitaa umma uligomea uchaguzi, wezi wakajishindia kwa mbwembwe na tambo nyingi..!!! Unataka wagome tena, au??

Kama nyani wanakula mahindi shambani kwako, ukisusa wanamaliza yote.. hawana huruma
 
Ukijua thamani ya kura yako utapata ujasiri wa kwenda kupiga kura na kuilinda na itangazwe namna ulivyochagua!
Wacheni kutujaza ujinga,hivi kura wanaohesabu ni mawakala au wapiga kura.unaposema tulinde kura tunalindaje wakati haturuhusiwi kuingia ndani zinakohesabiwa kura?#sipigikura
 
Wacheni kutujaza ujinga,hivi kura wanaohesabu ni mawakala au wapiga kura.unaposema tulinde kura tunalindaje wakati haturuhusiwi kuingia ndani zinakohesabiwa kura?#sipigikura
Ujinga unakuwa nao mwenyewe na siyo dhambi!
Ukijielimisha utajua kivipi utalinda kura yako hata kama siyo wakala, pia utajua umuhimuwa kupiga kura badala ya kususia!
 
Tuwe wakweli Watanzania wanahitaji heshima na kuthaminiwa.Haya mambo ya dharau na kiburi watawala yanachosha. Neno " Hamtashinda" baya sana halifai kwa taifa la kidemocrasia.
Ni kweli hawatamshinda kwa sababu kazi alizozifanya siyo za kawaida kwa kipindi kifupi mno. Tutampatia tena kipindi cha miaka 5
 
Tumeporwa tokea one party system, mnashtuka leo?Vumilia hadi aje mkombozi.
 
Narudia tena kwako, hata kama Mbowe na Zito wangepewa ukuu wa Tume bado hamtashinda. Mwaka ule mlisaidiwa na mzee Lowassa na hayuko kwenu tena na wala msije jifariji. Hata kura millioni moja this time hamtopata. Mark my words. Na wala hamtaibiwa ila watu hawatawapa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…