Kwenye hoja hii
Wanabodi, Nimekutana na hii kitu, nimeisoma, sio tuu nimeshangaa, bali nimechoka, imeniacha hoi, ukisoma ukaona jinsi tunavyoibiwa rasilimali zetu, na wanaofanya tuibiwe, ni wenzetu tuliowapa dhamana ya kutuongoza, mtu unaweza kupata wazimu, ukarukwa na akili, ukikamata SMG, unaweza...
Ya 2012, nimesema tumesaini PSA 21 za gesi huku hatuna sera ya gesi wala sheria, nikauliza tuna haraka gani?.
Wewe ukanichallenge kuwa mwaka huo hatukuhitaji sera wala sheria kwasababu gesi ilikuwa haijaanza kuchimbwa!. Nikakuwekea mkataba wa bomba la gesi kuonyesha Tanzania tumeanza kuchimba gesi zamani tangu Songo Songo, hivyo there is no excuse kwanini tusiwe na sera ya gesi na sheria ya gesi ndipo kugawe vitalu na kusaini hizo PSA!.
All and all, I'm over 50, nina wajukuu 5!, kwa watoto wangu wa kuzaa mwenyewe, hivyo mimi ni babu!.
Na kwa vile pia niliwahi pata ajali inayohisisha kichwa, pia you never know.
P
Pasco,
Unachanganya madesa...
Tanzania kuna gas za "aina mbili"... aina ya kwanza ni ile ambayo iligunduliwa miaka ya 80 na aina ya pili ilianza kugunduliwa rasmi mwaka 2010.
Ile ya awamu ya kwanza, ilikuwa kiduchu tu; pale Songosongo na Mnazi Bay!! Hilo bomba unalosema wewe ni kwa ajili ya gas ya Mnazi Bay ambayo iligundulika back in 1980's!!
Kama utakumbuka, kabla ya suala la bomba, kule Mtwara kulikuwa na kampuni ya Artmas (am not sure with spellings) ambayo ilikuwa inazalisha umeme kwa kutumia gas ya Mnazi Bay a.k.a Msimbati lakini kwa bahati mbaya uchumi wa Lindi na Mtwara collectively haukuwa na uwezo wa ku-fully utilize umeme uliokuwa unazalishwa!!
Kutokana na uchumi wa Lindi na Mtwara kushindwa ku-utilize ule umeme at full capacity ndipo busara ikaonekana kusafirisha hiyo gas kutoka Mtwara to Dar es salaam ili umeme wake uingie kwenye grid ya taifa!!!
Hapa pia tukumbushane kejeli za Prof Sospeter Muhongo kwamba "Wafanyabiashara wa Tanzania hawana pesa ya kuwekeza kwenye gas industry"!! Muhongo hakuwa anamaanisha hiyo gas unayoisema wewe kwa sababu haikuwa nyingi kiasi cha kufikiria kuisafirisha na ndio maana ikatumika kuzalisha umeme tu!!
Gas aliyokuwa anaisema Muhongo ni hii ya awamu ya pili!!
Hii gas ya awamu ya pili, hadi in early 2000's ambacho tulikuwa nacho was just seismic data zikionesha UWEZEKANO wa uwepo wa mafuta na gas kwenye pwani ya Lindi na Mtwara lakini hatukufahamu hiyo gas exactly ilikuwa at which particular point na kwa kiasi gani!!!
It's like zile taarifa za TMA kwamba "Pwani ya kaskazini mashariki itanyesha mvua kubwa" lakini data hazisemi hiyo mvua itanyesha eneo gani hasa!!
So, kwenye gas industry unapokuwa na just seismic data, hatua inayofuata ni kuchimba visima vya UTAFUTAJI gas ili kufahamu hiyo gas exactly ipo point ipi hasa na kwa kiwango gani!!
Hapo sio kwamba unachimba gas bali unachimba kujiridhisha at which particular points ipo hiyo gas!! Na unapofanya hivyo, kuna 3 possible outcomes:-
1. No gas at all,
2. Gas ipo lakini but not economically viable kufanya extraction... meaning, hata kama ipo lakini ukiichimba hutaweza hata ku-cover extraction costs let alone kupata faida, na
3. Gas ipo ya kutosha and it's economically viable for further extraction!!
Outcome inapokuwa ama #1 or #2, hapo pesa mliyoingiza kufanya exploration inakuwa imeenda na maji, na kwa kawaida hiyo itakuwa zaidi ya 50 Billion kwa sababu hii gas ipo deep sea!!
Ukipata option #3, hapo eneo husika ndipo linakuwa declared kwamba ipo gas ya kutosha na kuingizwa kwenye takwimu, kisha mnahamia eneo lingine kuchimba kuangalia kama kuna gas (gas exploration) na sio kuchimba gas!!
Sasa basi, hilo zoezi lilianza mwaka 2000, na vitalu vya awali mnada wake ulifanyika Houston!! Again, huu haukuwa mnada wa kuuza vitalu vya kuchimba gas bali mnada wa kuuza vitalu vya kufanya exploration kutokana na available seisimic data!
Tangu mwaka 2000, declaration ya kwanza kwamba kweli gas ipo kwenye pwani ya Lindi na Mtwara ilikuwa mwaka 2010, na kama sikosei, ambao waliigundua ilikuwa kampuni ya Ophir!!!
That being said, hadi hiyo 2010 kulikuwa na kisima kimoja tu ambacho kili-confirm uwepo wa gas!!
More and more gas ilianza kugundulika from 2013, na kuanzia hapo ndipo takwimu zetu zikabadilika kutoka kwenye seismic data alone hadi kuwepo kwa at least 57 trillion cubic of feet of gas ambazo ziligundulika zaidi baada ya uuzaji wa vitalu back in 2012!!
Na baada ya kugundulika rasmi gas, ndipo 2015 bunge likapitisha zile sheria 3 ambazo upinzani walisusia kikao...
Na endapo utaratibu unafuatwa, sasa baada ya kupitishwa zile sheria ndipo lingefuata zoezi la uuzaji wa UCHIMBAJI GAS (sio utafutaji tena) kwa sababu hapo tayari mnakuwa mmeshafahamu ni wapi na wapi (particular area) kuna gas na kwa kiwango kipi!
Lakini kwa upande mwingine, punguzeni kusikiliza sana kauli za Wanasiasa bali tafuteni ukweli! In short, si kweli kwamba hakukuwa na sheria kwa sababu sheria iliwepo tangu mwaka 1980, tafuta "Petroleum (Exploration and Production) Act, 1980" ambayo ndiyo ilikuwa inatumika!!