Aliyekubali Switch za bwawa la umeme la Rusumo Tanzania zikawekwe Rwanda ametumia akili zake ipasavyo?

Aliyekubali Switch za bwawa la umeme la Rusumo Tanzania zikawekwe Rwanda ametumia akili zake ipasavyo?

For what I know, huo mradi sio wetu kwa 100% bali Mabeberu ndio wana-finance huo mradi kwa ajili ya Rwanda, Burundi na Tanzania!!

So, mwenye pesa zake ndo kaamua hivyo, HUTAKI, jenga mwenyewe kwa pesa zako... nyie si dona kantri bhana!!! Ukifanya hayo, ndo utaamua kuweka swichi popote pale hata kama kwenye ofisi za Lumumba!!
Hebu ngoja, mbona huyo manager wa mradi anasema Tanzania tumetoa 100% ya fedha tunayopaswa kutoa, Rwanda 50% na Burundi ndio wamepewa hela na wafadhili? Au ndio mambo ya kuingizana town?
 
Ukisoma michango ya wachangiaji wengi utagundua wanatoka povu na hawajui chochote kuhusu huo mradi, wameona mada mezani mbio wamekimbilia kuchangia kwa mihemko...Huo mradi ni Joint project ya inchi 3, kila inchi imechangia na kila inchi itapata Megawatt 27...ss mlitaka kila kitu kiwe Tz na hao wengine, how will they protect their investment.?
 
Nimepata taarifa zisizo rasmi kwamba eti lile bwawa la umeme la Rusumo linalojengwa huko Ngara Tanzania, eti switch zake za kuwashia na kusambazi umeme zinafungwa Rwanda.

Maana yake ni kwamba Tanzania itakuwa ikizalisha umeme, halafu huo umeme utasafiri hadi Rwanda, halafu Rwanda ndio itakua inawasha hizo Switch ili kuruhusu umeme uje Tanzania.

Je, kuna mantiki yeyote juu ya maamuzi kama haya? , kwahiyo siku tukipandisha ushuru bandarini kwa mizigo inayoenda Rwanda na wao wanatuzimia switch za umeme hadi tushike adabu, na umeme tunauzalisha wenyewe? Sasa nashangaa, Tanzania tulikosa pesa ya kununulia switch hadi kwenda kuomba mchango wa Rwanda na tugawane nao umeme nusu kwa nusu eti?

Mi nadhani kuwe na haja ya kupimana magonjwa ya akili kabla ya kupeana hizi wizara nyeti hasa za Nishati na madini.., video ina maelezo ya ziada


Ukaambiwa hivyo na wewe ukakubali!?
 
Kuna hizi tetesi za Rwanda (Watusi) kutawala nchi zote za Mashariki na kati ya Afrika, ndio mkakati unaendelezwa nini?
 
Pasco,

Unachanganya madesa...

Tanzania kuna gas za "aina mbili"... aina ya kwanza ni ile ambayo iligunduliwa miaka ya 80 na aina ya pili ilianza kugunduliwa rasmi mwaka 2010.

Ile ya awamu ya kwanza, ilikuwa kiduchu tu; pale Songosongo na Mnazi Bay!! Hilo bomba unalosema wewe ni kwa ajili ya gas ya Mnazi Bay ambayo iligundulika back in 1980's!!

Kama utakumbuka, kabla ya suala la bomba, kule Mtwara kulikuwa na kampuni ya Artmas (am not sure with spellings) ambayo ilikuwa inazalisha umeme kwa kutumia gas ya Mnazi Bay a.k.a Msimbati lakini kwa bahati mbaya uchumi wa Lindi na Mtwara collectively haukuwa na uwezo wa ku-fully utilize umeme uliokuwa unazalishwa!!

Kutokana na uchumi wa Lindi na Mtwara kushindwa ku-utilize ule umeme at full capacity ndipo busara ikaonekana kusafirisha hiyo gas kutoka Mtwara to Dar es salaam ili umeme wake uingie kwenye grid ya taifa!!!

Hapa pia tukumbushane kejeli za Prof Sospeter Muhongo kwamba "Wafanyabiashara wa Tanzania hawana pesa ya kuwekeza kwenye gas industry"!! Muhongo hakuwa anamaanisha hiyo gas unayoisema wewe kwa sababu haikuwa nyingi kiasi cha kufikiria kuisafirisha na ndio maana ikatumika kuzalisha umeme tu!!

Gas aliyokuwa anaisema Muhongo ni hii ya awamu ya pili!!

Hii gas ya awamu ya pili, hadi in early 2000's ambacho tulikuwa nacho was just seismic data zikionesha UWEZEKANO wa uwepo wa mafuta na gas kwenye pwani ya Lindi na Mtwara lakini hatukufahamu hiyo gas exactly ilikuwa at which particular point na kwa kiasi gani!!!

It's like zile taarifa za TMA kwamba "Pwani ya kaskazini mashariki itanyesha mvua kubwa" lakini data hazisemi hiyo mvua itanyesha eneo gani hasa!!

So, kwenye gas industry unapokuwa na just seismic data, hatua inayofuata ni kuchimba visima vya UTAFUTAJI gas ili kufahamu hiyo gas exactly ipo point ipi hasa na kwa kiwango gani!!

Hapo sio kwamba unachimba gas bali unachimba kujiridhisha at which particular points ipo hiyo gas!! Na unapofanya hivyo, kuna 3 possible outcomes:-

1. No gas at all,
2. Gas ipo lakini but not economically viable kufanya extraction... meaning, hata kama ipo lakini ukiichimba hutaweza hata ku-cover extraction costs let alone kupata faida, na
3. Gas ipo ya kutosha and it's economically viable for further extraction!!

Outcome inapokuwa ama #1 or #2, hapo pesa mliyoingiza kufanya exploration inakuwa imeenda na maji, na kwa kawaida hiyo itakuwa zaidi ya 50 Billion kwa sababu hii gas ipo deep sea!!

Ukipata option #3, hapo eneo husika ndipo linakuwa declared kwamba ipo gas ya kutosha na kuingizwa kwenye takwimu, kisha mnahamia eneo lingine kuchimba kuangalia kama kuna gas (gas exploration) na sio kuchimba gas!!

Sasa basi, hilo zoezi lilianza mwaka 2000, na vitalu vya awali mnada wake ulifanyika Houston!! Again, huu haukuwa mnada wa kuuza vitalu vya kuchimba gas bali mnada wa kuuza vitalu vya kufanya exploration kutokana na available seisimic data!

Tangu mwaka 2000, declaration ya kwanza kwamba kweli gas ipo kwenye pwani ya Lindi na Mtwara ilikuwa mwaka 2010, na kama sikosei, ambao waliigundua ilikuwa kampuni ya Ophir!!!

That being said, hadi hiyo 2010 kulikuwa na kisima kimoja tu ambacho kili-confirm uwepo wa gas!!

More and more gas ilianza kugundulika from 2013, na kuanzia hapo ndipo takwimu zetu zikabadilika kutoka kwenye seismic data alone hadi kuwepo kwa at least 57 trillion cubic of feet of gas ambazo ziligundulika zaidi baada ya uuzaji wa vitalu back in 2012!!

Na baada ya kugundulika rasmi gas, ndipo 2015 bunge likapitisha zile sheria 3 ambazo upinzani walisusia kikao...

Na endapo utaratibu unafuatwa, sasa baada ya kupitishwa zile sheria ndipo lingefuata zoezi la uuzaji wa UCHIMBAJI GAS (sio utafutaji tena) kwa sababu hapo tayari mnakuwa mmeshafahamu ni wapi na wapi (particular area) kuna gas na kwa kiwango kipi!

Lakini kwa upande mwingine, punguzeni kusikiliza sana kauli za Wanasiasa bali tafuteni ukweli! In short, si kweli kwamba hakukuwa na sheria kwa sababu sheria iliwepo tangu mwaka 1980, tafuta "Petroleum (Exploration and Production) Act, 1980" ambayo ndiyo ilikuwa inatumika!!
Mkuu Chige , thanks very much for this, hii ndio faida halisi ya jf, sharing knowledge, kiukweli baada ya kukusoma hapa, nimeelimika na kujikuta kumbe kule mwanzo nilikuwa sijui kitu!. Thanks.
P
 
Ushafika kwenye huo mradi au unaanzisha Uzi kuidhihaki serikali na viongozi wake?!!
In hivi, huo mradi ni wa nchi tatu,Rwanda,Burundi na tz.
Therefore kuna kitu kinaitwa MoU ambapo ni kat ya Rwanda na tz kwa kuwa ndizo zimepakana katika mradi huo. Mitambo yote ya kufua umeme iko katika ardhi ya tz but switch ambapo ni kama supply station iko Rwanda ila palepale jirani na bwawa just like 2km juu ya kimlima.
Sasa nyie mkisikia switch ziko Rwanda mnashuka na Uzi kwa DHARAU mkijua labda walizipeleka KIGALI.
 
1.Kwanza ni mradi wa nchi 3 na Tanzania imewekeza zaidi ndio mana mitambo ipo kwetu.

2.Eneo lenyewe lilipo sio salama kufanya mradi mkubwa kama huo peke yako.

3.Ukiangalia faida ya usalama kwa jirani yako ni bora mushirikiane na mukubaliane ni aina gani ya ukuta utawafaa ujengwe kutenganisha nyumba/viwanja vyenu.

Nina imani na viongozi wetu waliyaweka maslahi mapana ya nchi yetu ndio mana wakakubali mradi wa ushirikiano.

Mungu Ibariki Afrika Mungu ibariki Tanzania.
 
Kwenye hoja hii
Ya 2012, nimesema tumesaini PSA 21 za gesi huku hatuna sera ya gesi wala sheria, nikauliza tuna haraka gani?.

Wewe ukanichallenge kuwa mwaka huo hatukuhitaji sera wala sheria kwasababu gesi ilikuwa haijaanza kuchimbwa!. Nikakuwekea mkataba wa bomba la gesi kuonyesha Tanzania tumeanza kuchimba gesi zamani tangu Songo Songo, hivyo there is no excuse kwanini tusiwe na sera ya gesi na sheria ya gesi ndipo kugawe vitalu na kusaini hizo PSA!.

All and all, I'm over 50, nina wajukuu 5!, kwa watoto wangu wa kuzaa mwenyewe, hivyo mimi ni babu!.

Na kwa vile pia niliwahi pata ajali iliyohusisha kichwa, pia you never know.
P
Duu, una wajukuu watano?! Hongera ndugu, hatua kubwa sana hiyo
 
Huo mradi umechangiwa na nchi tatu pia kumbuka mto Rusumo unapatikana katika nchi hizo tatu na wote wamechangia mradi huo hivyo switch room kuwa Rwanda ni sawa tu kama makubaliano yako hivyo!
Kama mto upo nchi zote tatu kila mtu ajenge bwawa kwake, ndio tutajua kama upo nchi zote au Tanzania
 
Look at you!! Eti kutia watu hasira!! Yaani hapo ndo unataka kujifanya Mzalendo sana, au?! Hivi mradi wenyewe unaujua au ndo kwanza leo umeusikia na hapo hapo ukakurupuka kuja JF?!!

Nimekuuliza, mradi upo mpakani, na unahudumia nchi 3 kwa usawa; sasa kwanini ulitaka switch iwe Tanzania na siop Rwanda au Burundi?

Mradi umeajiri Watanzania wengi kuliko Warundi na Wanyarwanda collectively; unataka kusema Rwanda na Burundi hawajali maslahi yao?!

Si bora ungehoji kwanini HQ iwe Rwanda ingawaje justification ipo kutokana na project proximity na Rusumo... lakini unahoji switch!!!
Na mimi nakauliza, Tanzania ilikosa pesa ya kununulia switch? Labda utuambie, mradi upo kwenye mpaka wa Tanzania na Rwanda au ni mpaka wa Tanzania na burundi?
 
Back
Top Bottom