Aliyekuwa mbabe wa kivita Liberia, Prince Johnson afariki dunia akiwa na miaka 72

Aliyekuwa mbabe wa kivita Liberia, Prince Johnson afariki dunia akiwa na miaka 72

BabaMia

JF-Expert Member
Joined
Jan 7, 2024
Posts
270
Reaction score
554
Aliyekuwa mbabe wa kivita wa Liberia Prince Johnson, ambaye alisimamia mauaji ya kikatili ya aliyekuwa Rais Samuel Doe wakati vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyotikisa nchi hiyo, kabla ya kuwa Seneta na Mfalme wa kisiasa, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 72.

Msemaji wa familia Wilfred Bangura amethibitisha kuwa Johnson, alikuwa na shinikizo la damu kabla ya kufariki Dunia.

Zaidi ya watu 200,000 waliuawa, maelfu zaidi wakipata ulemavu na kubakwa na zaidi ya Milioni Moja walikimbia makazi yao wakati wa vita vya kikatili vya wenyewe kwa wenyewe nchini Liberia kati ya 1989 na 2003, ambapo Johnson alihusika.

Johnson alipata umaarufu baada ya watu wake kumkamata, kumtesa, na kumkata viungo vya mwili Rais wa zamani Doe kabla ya kumuua.
1732821362891.jpg

#KitengeUpdates
 
TOKA MAKTABA :

13 Juni 2022

Prince Johnson- Nimetubu, Nilimrejea mwenyezi Mungu

Prince Johnson Wa Kaunti Ya Nimba, Liberia Aeleza Jinsi Alivyoipata Dini Baada Ya Kifo Cha Samuel Doe

View: https://m.youtube.com/watch?v=3xD4pc8Mht8
Prince Yormie Johnson ni mwanasiasa wa Liberia na Seneta Mkuu wa sasa kutoka Kaunti ya Nimba nchini Liberia. Aliyekuwa mbabe wa kivita na kiongozi wa waasi, Johnson alichukua nafasi kubwa katika Vita vya Kwanza vya wenyewe kwa wenyewe vya Liberia ambapo alimkamata, kumtesa, kumkata viungo na kumuua Rais Samuel Doe, ambaye yeye mwenyewe alipinduliwa na kumuua rais aliyepita William R. Tolbert Jr. +
 
TOKA MAKTABA :

09 Agosti 2023

NDANI YA HEKALU / KASRI ALIYEKUWA RAIS WA ALIBERIA SAMUEL K. DOE HOUSE miaka 33 baada ya kifo chake.

View: https://m.youtube.com/watch?v=gtRIAP0YWIk

Katika video ya leo, nitakupitisha kwenye jumba la Rais wa zamani wa Liberia Samuel K. Doe, kasri hilo lililokatiwa jina Doe Palace. Samuel K. Doe alikuwa Rais wa 21 wa Liberia.
 
Toka maktaba :

14 June 2023

NDANI YA KASRI LA MBABE WA KIVITA NA ALIYEKUWA RAISI WA LIBERIA CHARLES G TAYLOR HOUSE


View: https://m.youtube.com/watch?v=8inadNWPsUY
katika video ya leo nimetembelea jumba kubwa mfano wa hekalu / kasri lililojengwa na Rais wa Zamani wa Liberia mbabe wa kivita Charles G. Taylor House katika mji aliozaliwa wa Arthington Liberia. Charles G. Taylor alikuwa Rais wa 22 wa Jamhuri ya Liberia.
 
TOKA MAKTABA:
23 Juni 2023

MJI ULIOTELEKEZWA WA KIJIJINI KWA MKUU WA NCHI ! WA ALIYEKUWA MBABE WA KIVITA NA RAIS WA LIBERIA CHARLES G TAYLOR


View: https://m.youtube.com/watch?v=83vGWieTias

Katika video hii tunatembelea mjini wa nyumbani kwao KIJIJINI kwa aliyekuwa Rais wa Liberia Charles G TAYLOR nyumbani kwa Town Arthington nchini Liberia...

Mji umebaki magofu baada ya aliyekuwa akipeleka maendeleo kuondoka madarakani na kukimbia uhamishoni kisha kufunguliwa mashtaka the Hague Uholanzi kwa ukiukwaji wa haki ya kuiishi, utekaji na mauaji vitani ...
 
Back
Top Bottom