Aliyekuwa Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari na Willy Qulwi Qambalo wa Karatu wajiunga CCM na kupokelewa na Mwenyekiti wa UVCCM Taifa


Kuna majimbo hata wasipoungana na ACT ,Chadema lazima ishinde Arusha,Hai,Mbeya Mjini,Tarime etc

Yes MEMBE ni Mtaji kwasasa!! Naunga mkono hoja.
 
Aliyekuwa Mbunge wa Arumeru ,Joshua Nasari(Chadema) na kung'olewa na Spika wa bunge la Jamhuri ya muungano Tanzania,Job Ndugai na kuzua utata mkubwa katika kuondolewa kwake,ametangaza kujiunga na chama cha mapinduzi na kupokelewa na mwenyekiti wa uvccm Taifa ,Kheri James.

Nasari amekishukuru chadema kwa kumlea tangia akiwa mdogo na sasa ameamua kutumikia nchi yake na sina nia ya kugombea nafasi yoyote,kilichopo mbele yake ni kumsaidoa rais John Magufuli.

 
Haya kumekucha, wafia chama pokeeni wageni wateule hao.....mshaambiwa ni marufuku kura za maoni katika majimbo yote ya walikotoka hawa wahamiaji...mpo???
 

Ametimiza Haki yake ya Kikatiba kama vile ambavyo hata Lazaro Nyalandu nae aliitimiza pale alipotoka CCM na Kutimkia zake pia huko CHADEMA.
 
Kila nikirudia kusoma ulichoandika kwenye para ya pili sikielewi, yaani kupona kwa CDM kunategemea kuungana na ACT?! how? hao ACT wana nguvu gani Tz Bara compare na Chadema? Na kama jamaa wamepanga kuwanyima wagombea wa Chadema ushindi kwa lazima, huo muunganiko wa CDM na ACT ndio utasaidia nini kwa CDM? Na huo uwepo wa Membe utasaidia nini kuondoa hiyo hali kama Lowassa na nguvu zake alishindwa?

Hebu wacha utani.
 
Hawa wote wanovihama vyama vyao dakika za mwisho, ilipaswa kutopewa kabisa fursa za kugombea...

Ni dalili kuwa ni wabinafsi na wapo kimadaraka tu zaidi
 
Umeandika point ambayo Chadema inabidi ikubali pia ,kiukweli Chadema imepoteza Wana mikakati imara na interejensia ndio maana wanayumba

Yote kwa yote , Zito ni mwanasiasa mwenye akili kwa kizazi hiki cha upinzani wa Sasa , Chadema walikosea Sana kumfukuza wangemvumilia Sasa hivi wangekuwa mbali sana
 
subiri waje wanataka tume huru wao hawataki wanachama
 
CDM kila siku watu muhimu wanaikimbia..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…