Aliyekuwa Mkurugenzi wa Sheria TFF amaliza utata: Asema Fei Toto amekosea, mkataba hauvunjwi kienyeji vile

Aliyekuwa Mkurugenzi wa Sheria TFF amaliza utata: Asema Fei Toto amekosea, mkataba hauvunjwi kienyeji vile

Ila haya mambo bana.

Makolo leo wamegeuka mabush lawyers.
 
Mkuu kuna kitu unakisahau japokua umeandika maelezo mengi. Katika ile barua ya Yangu ilichapishwa imeeleza kuna sheria na taratibu za FIFA na TFF zimekiukwa.

Yes amevunja mkataba lakini kwa taratibu za FIFA ilipaswa timu inayomtaka hasa wakati wa dirisha ionane na timu inayommliki mchezaji wajadiliane kuvunja mkataba. Feisal amekidhi vigezo kuvunja mkataba na Yanga ila hajakidhi kulungana na taratibu za baba wa mpira wetu na ndicho anachozungumza huyo mwanasheria.

Tusikurupuke jamani tunaishia kujiaibisha kuandika vitu tusivyo na uelewa navyo
Hizo sheria na taratibu zilikuwepo kwenye vipengele walivyo saini Fei Toto na Yanga SC?

Haiwezekani nyie wenyewe mmempa mchezaji uhuru wa kuvunja mkataba atakapoweka pesa, halafu amewawekea pesa mnagoma kuipokea, inamaana mlikuwa hamjui mnachofanya wakati wa kusaini mkataba.
 
Hizo sheria na taratibu zilikuwepo kwenye vipengele walivyo saini Fei Toto na Yanga SC?

Haiwezekani nyie wenyewe mmempa mchezaji uhuru wa kuvunja mkataba atakapoweka pesa, halafu amewawekea pesa mnagoma kuipokea, inamaana mlikuwa hamjui mnachofanya wakati wa kusaini mkataba.
Mkataba mzima wa yanga na Feisal umesoma, unajua mkataba mostly ni page 50 na mingine mpaka page 200
 
Nimefwatilia hili jambo na kuja kugundua watu wengi wanakisema kipengele Cha kua anatakiwa a deposit signing fee na mishahara ya miezi mi 3
But kwa chini yake kuna sehemu pia inamtaka kabla hajafanya Hilo anatakiwa atoe notice ya miezi 6 na hapo ndo panapombana Fei .
Labda wewe ndie nakuelewa, hapo uliposema but kwa chini yake...... hicho kama kweli kipo, ndicho kitambana Fei, na sio mambo ya baba wa mpira na mengineyo.
 
Labda wewe ndie nakuelewa, hapo uliposema but kwa chini yake...... hicho kama kweli kipo, ndicho kitambana Fei, na sio mambo ya baba wa mpira na mengineyo.
Feisal alitakiwa akae na yanga, wakigoma aende TFF ili wampe go ahead sababu wao ndo wanamikataba, same arsenal walivyofanya kwa partey walienda kwa laliga wakapewa go ahead ya kutrigger release clause tatizo nchi hii watu wanapenda shortcut
 
- ww hujui sheria, hujui Legal principles zinazotumika, kwenye mikataba Kuna kitu kinaitwa Privity to contract, Feisal hawezi kujiondokea tu kienyeji, bila kukaa mezani na Klabu yake Ya Yanga na Club anayotaka kwenda, the undermining principle hapa ni kuwa mchezaji ni wa timu, Ile aliyoingia nayo mkataba tu i.eFeisal salum And Young Africans huwezi kuondoka, na kama mkataba una lugha tata/isiyoeleweka Mkataba huo utatafsiriwa against the Maker ni Sina uhakika kama mkataba ulikuwa haueleweki
Naona mnaingiza third parties kwenye mambo binafsi waliyokubaliana Fei na Yanga SC, tatizo lenu mnakariri sana.
 
Nadhani huyu hajamaliza utata bali katoa mawazo yake kulingana na uelewa wake. Kwani wewe huyu ndo unamuamini sana ktk sheria za mpira kuliko watu wote Tanzania au Duniani waliosomea sheria za mchezo huo. Au kuwa mkurugenzi wa sheria hiyo title ndio inakufanya kuamini kuwa anajua Kila kitu
 
Yote ni sawa, lqkini kama mchezaji hataki kuitumikia club yako huna mamna.

Yanga wamtafute FEI wayamalize ili FEI akachukue madolari kwa Mwarabu tena ya uhakika... watu walianza kwa Mshua zenji wakayamaliza sasa Uto mtahangaika saana.

Yaani kumbe uto mlikuwa mnampa mil 3 tu...looh. ..sasa Mzee Bakhresa kawapandia dau mara 5 dadec

Mwachieni HAWATAKI.. hakuna mkataba wowote duniani usionunulika...kanunuliwa Holland ilakuwq FEI... manara anawaingiza chaka Uto.

Kama ana miezi 16 imebakia haya pigeni kwa 3mil afu muweke na ausumbufu...mlipwe hela mwahi kutafuta wa mafungu muda wa usajili unakimbia
 
Hapa hakuna mwanasheria, ni kanjanja tu. Hajui hata zinazungumzia nini.

Kwa mfano.
Azam wanahusikaje katika hili la Feisal? Mpaka sasa hakuna mahali Feisal amesema anahamia Azam, na Azam wamekanusha kuhusika na chochote kuhusu Feisal. Sasa mwanasheria unajengaje hoja katika hilo?

Mchezaji akiwa huru (hana tena mkataba na klabu yake ya awali), ni vipi tena klabu zingine zikitaka kumsajili ziende kujadiliana na klabu yake ya awali?

Kama mkataba wa Feisal na Yanga unatoa nafasi kwa Feisal kuweza kuuvunja muda wowote kiwa atalipa fidia za kimkataba na Feisali anaona okay, nini mantiki ya kusema Feisal anapaswa kwanza kufanya majadiliano na Yanga? Ili iweje?
Wewe unamuita kanjanja mtu aliyekuwa mkurugenzi wa sheria TFF? Angekuwa kanjanja angeajiriwa na chombo kikubwa kama TFF kuwa mkurugenzi wake?
 
Nimefwatilia hili jambo na kuja kugundua watu wengi wanakisema kipengele Cha kua anatakiwa a deposit signing fee na mishahara ya miezi mi 3
But kwa chini yake kuna sehemu pia inamtaka kabla hajafanya Hilo anatakiwa atoe notice ya miezi 6 na hapo ndo panapombana Fei .
Unaweza kutuwekea hapa ili na sisi tujisomee Mkuu?
 
Mbona mnakitaja kipengele hiki tu ? Cha chini yake kinachomtaka kabla ya kufanya hili alitakiwa atoe notice ya miezi 6 mbona hamkitaji?
Tuletee hapa Mkuu,utakuws umetusaidia sana
 
Wewe unamuita kanjanja mtu aliyekuwa mkurugenzi wa sheria TFF? Angekuwa kanjanja angeajiriwa na chombo kikubwa kama TFF kuwa mkurugenzi wake?
Ni kanjanja kweli, nilitaka kuandika hivyo pia nikamuhurumia tu, amekariri tu sheria wakati mambo hubadilika kulingana na makubaliano ya pande mbili kimkataba.
 
Alinunua mkataba wake uwe na akili
We ndio huna akili, kununua kitu lazima muuzaje aridhie vinginevyo na vurugu. Ndio maana ya mkataba(pande mbili kukubaliana) na pia mnaweza kukubaliana kutokukubaliana(hii hutaelewa).

Kajifunze upya
 
Nyie nachoona sasa mnaishi kwa matumaini tu, mkiambiwa wekeni kipengele kinachombana Fei hamuweki, mnahisi tu.!!
Swala sio kipingele huwez vunja mkataba kihuni ndo maana ndege tatu za ATCL zimekamatwa kwa mambo haya haya ya kihuni, swala sio haki kwenye mkataba ufuate taratibu ndo kitu Cha muhimu
 
Back
Top Bottom