Aliyekuwa Mkurugenzi wa Sheria TFF amaliza utata: Asema Fei Toto amekosea, mkataba hauvunjwi kienyeji vile

Aliyekuwa Mkurugenzi wa Sheria TFF amaliza utata: Asema Fei Toto amekosea, mkataba hauvunjwi kienyeji vile

Huu ujinga wenu wa kuvunja mikataba kihuni ufanyeni huku ndani, Ila mkifanyia foreigner ndo yanatokea ya kukamatwa kwa ndege
Ndege huwa zinakamatwa kwa sababu watu hawajalipwa vyao, sio kama Yanga wamewekewa pesa walizotaka wakagoma kuzipokea, nyie hamjui kutofautisha mambo.
 
Hakuna mkamilifu hata wewe una mapungufu kibao watu wanaishi na wewe sababu wameamua kukuvumilia

Kwa kukusaidia hakuna mwanasheria ambaye hajawahi vunja sheria
Sasa hiyo haiwezi kuwa excuse kusema tumchukulie serious eti kwakua tu binadamu wana mapungufu

Tukisema kila mtu tumuangalie kwa kipimo hicho hicho cha udhaifu, tutashindwa hata kutoa hukumu kwenye makosa wanayofanya
 
Mazungumzo as if club ndo ina say ya mwisho kuhusu mchezaji
 
1: Mkataba huweza kuvujwa wakati wowote na bila kuhusisha pande zote.

Kilicho cha msingi ni: KUZINGATIA NAMNA/VIGEZO VILIYOTAJWA KWENYE MKATABA HUSIKA ILI KUUVUNJA KWA WAKATI HUSIKA.

Mkataba unajisimamia huitaji mazungumzo ya jinsi ya kuuvunja. Cha msingi ni kama mhusika katimiza masharti hayo?

2: Kama umetimiza masharti ya kuvunja mkataba, kesho yako au muda baada ya kuvunja mkataba u juu yako. Ukiumwa, kupata ajali au shida yoyote wewe uko nje ya utaratibu.

3: Ukivunja mkataba kwa kufuata utaratibu wa mkataba na wakati wake basi huitaji mwaka mzima kuendela na yako, unaweza kubaki nyumbani au kutafuta kazi mpya ndani au nje ya mwajiri wako. Labda tu kama uliingia mkataba kukiwa na maelezo ya ziada baada ya huo mkataba.

NB: Mwenye macho asome hapo 14.7: Real Extraordinary
20221225_155847.png
 
Fei Atacheza Wapi Ameshaonekana Mamluki Huko Yanga(Msaliti)
 
Ndio hapo point ya gu ilipo

Huyo mwanasheria aliyeshiriki kuhalalisha lile jambo anawezaje leo kusimama kutuambia habari za sheria ya mkataba ilihali hata yeye sheria zinamshinda?
Kwani mwanasheria ndio alihalalisha? Yale yalikuwa ni maagizo ya viongozi kutoka juu, hapo mwanasheria hana nguvu za kuzuia
 
1: Mkataba huweza kuvujwa wakati wowote na bila kuhusisha pande zote.

Kilicho cha msingi ni: KUZINGATIA NAMNA/VIGEZO VILIYOTAJWA KWENYE MKATABA HUSIKA ILI KUUVUNJA KWA WAKATI HUSIKA.

Mkataba unajisimamia huitaji mazungumzo ya jinsi ya kuuvunja. Cha msingi ni kama mhusika katimiza masharti hayo?

2: Kama umetimiza masharti ya kuvunja mkataba, kesho yako au muda baada ya kuvunja mkataba u juu yako. Ukiumwa, kupata ajali au shida yoyote wewe uko nje ya utaratibu.

3: Ukivunja mkataba kwa kufuata utaratibu wa mkataba na wakati wake basi huitaji mwaka mzima kuendela na yako, unaweza kubaki nyumbani au kutafuta kazi mpya ndani au nje ya mwajiri wako. Labda tu kama uliingia mkataba kukiwa na maelezo ya ziada baada ya huo mkataba.
Sawasawa
 
Mechi ganiya Derby ambayo Yanga ilisusa kucheza mpaka bodi ya ligi ikabidi wasogeze ratiba mbele?
Mechi miezi minne imepangwa ichezwe saa 11 jioni,siku ya mechi timu ipo kwenye basi inaelekea uwanjani unaleta taarifa mechi saa 12 sijui saa 1,yanga siyo timu ya ndondo,haichezi bonanza,kilichofanya muda ipelekwe mbele unakijua Hadi Leo!?..Sheria inasemaje kuhusu kubadili muda!?
 
Huyu mkurugenzi wa sheria asiyejua sheria anashangaza, unasema vipi suala la mkataba ni la kukaa pamoja walimalize wakati kuna kipengele kwenye mkataba kilimruhusu mchezaji kuvunja mkataba kama akiweka kiasi fulani cha pesa kwenye akaunti ya klabu?

Zaidi, anaposema mchezaji anapovunja mkataba hakai peke yake, lazima akae na klabu yake, napo anakosea, akumbuke pande zote kwenye mkataba kisheria huwa zipo sawa, hapa asilete ukubwa wa klabu akadhani ndio advantage kwa Yanga SC, hapa Yanga SC walijichanganya wenyewe kuweka kipengele kilichowabana kwenye mkataba.

Pia, klabu inayomhitaji mchezaji sio lazima iandike barua ikimhitaji mchezaji husika, kuna.mazingira yanayolazimisha kufanya hivyo hasa ikiwa mchezaji bado ana mkataba na timu yake, na mkataba wake unambana kwenda timu nyingine bila makubaliano ya timu mbili.

Lakini kwa Fei Toto hali haiko hivyo, yeye habanwi na mkataba kwasababu ameshatimiza takwa la kimkataba lililomtaka anunue sehemu ya mkataba wake kama akitaka kuondoka akiwa huru, huyu mwanasheria anaonekana mchanga halafu amekariri mambo ya usajili, hajui kutofautisha mazingira.
Unataka kusema kwamba mchezaji akiichoka timu anajiondokea tu kwa vile hela ya kununua mkataba anayo ? yaani hakuna utaratibu wa kufuatwa ?
 
Ila mwamba nilikua nakuonaga una akili Ila unatabia za upiga debe, mkataba hauvunjwi lazima pande mbili zikae zikubaliane sababu Feisal alikua Mali ya Yanga, anahaki ya kuondoka lakin alichofanya ni uhuni
Wakikaa wakazungumza ila Feisal akawa na msimamo kuwa yeye ameshaamua kuondoka na harudi nyuma hayo mazungumzo yatakuwa na faida ipi?
 
Unaniita mimi shabiki wakati kimsingi wewe ndie shabiki, unaposema "lazima Yanga washirikishwe" hapa unasukumwa na mahaba tu, sio logic.

Mtambue, mtu kutimiza sharti lake kimkataba haitaji ruhusa ya upande wa pili, ni uamuzi wake binafsi, kazi inabaki kwako wewe wa upande wa pili kufanya alichofanya mwenzio, ukigoma kama Yanga walivyofanya, Fei ana uwezo wa kwenda TFF kushtaki.

Sijui kwanini mnataka Yanga SC washirikishwe maamuzi binafsi ya Fei, sioni logic yako hapa.
Hata mimi najiuliza kwa hiyo Yanga wanataka waambiwe na Fei kuwa mimi navunja mkataba baina yetu kwa mujibu wa makubaliano then Yanga wakatae kivipi sasa watakataa wakati mtu kaamua kuvunja mkataba?
 
Unataka kusema kwamba mchezaji akiichoka timu anajiondokea tu kwa vile hela ya kununua mkataba anayo ? yaani hakuna utaratibu wa kufuatwa ?
Utaratibu wa kufuatwa ni Fei kuweka pesa zote Yanga SC walizohitaji kimkataba, sharti ambalo Fei alilitimiza, kama unalo sharti jingine ambalo lipo kimkataba Fei hakulitimiz weka hapa tulione.

Kulazimisha Fei akaongee na Yanga Sc, ikiwa tayari ameshafanya kile mkataba unachotaka ni sawa na kumshusha wakati pande zote kimkataba zipo sawa kisheria.

Huwezi kusema Fei amevunja masharti ya mkataba kwa kukiuka jambo ambalo halikuwepo ndani ya mkataba baina yao, Yanga wapokee pesa waache malumbano.
 
Back
Top Bottom