Aliyekuwa Rais wa Tanzania, Hayati Dkt. John Magufuli azikwa Chato mkoani Geita

Aliyekuwa Rais wa Tanzania, Hayati Dkt. John Magufuli azikwa Chato mkoani Geita

Ulikuja chanika juzi imenyesha sanaa tu

Ili iwe ajabu unyeshe eneo la tukio tu
 
mtoto.png

Pole sana Suzan Magufuli
 
Nakumbuka 2012 huko Mbarali Mbeya alififariki nguli mmoja Na mchawi mkubwa wa usangu nzima. Ilikuwa ni mwezi wa 8 kipindi cha kiangazi. Muda wa kumzika mida ya saa 8 mchana ilinyesha mvua isio ya kawaida. Toka nizaliwe sikuwahi kuona mvua ikinyesha msimu kama ule.
 
Habari za muda huu.Kwanza nitoe pole kwa msiba huu mzito uliotukumba taifa letu na mpaka sasa tupo katika hatua za mwisho za kumpumzisha mpendwa wetu JPM katika makazi yake ya milele....
Tuendelee mkuu kumshukuru Mh. Hayati Rais wetu mpendwa kwa kutuletea hali ya mawingu na mvua. Daima tutaendelea kumkumbuka.
 
Hahaa hii ndiyo mtakuja Street jf. Karibu saana baby ntakutafuta baada ya maziko maana nimwkuona uko unachat
Dah unafanya tucheke kwenye msiba.🤣🤣🤣🤣

Mtu ashatwishwa na cheo cha baby fasta
 
Fuatilia mbashara hapa



RAIS Samia Suluhu Hassan leo ataongoza waombolezaji kumzika Rais wa Serikali ya Awamu ya Tano, John Magufuli.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu, Bunge, Vijana na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama atamkaribisha Mwenyekiti wa Kamati ya Mazishi ya Kitaifa, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa atoe neno la utangulizi likifuatiwa na salamu.

Salamu hizo zitatolewa wawakilishi wa makundi wakiwemo wazee wa Chato, vyama vya siasa, na viongozi wa nchi za nje. Salamu nyingine ni kutoka kwa vyombo vya ulinzi na usalama, Mahakama ya Tanzania, Bunge la Jamhuri ya Muungano, Rais mstaafu Jakaya Kikwete, Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi, na Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Mwinyi.

Baada ya salamu, Rais Samia atahutubia waombolezaji na kisha ataongoza wananchi na wageni kutoka nje ya nchi kutoa heshima za mwisho kumuaga Rais Magufuli.

Baada ya tukio hilo, familia ya Magufuli ikiongozwa na mkewe Janet Magufuli, Rais Samia na viongozi watakwenda eneo la maziko nyumbani kwa Magufuli.

Saa 8:00 mchana mwili wa Rais Magufuli utaondolewa uwanjani na kupelekwa mazikoni ambako itafanyika ibada itakayoongozwa na Askofu wa Jimbo la Rulenge wilayani Ngara Mkoa wa Kagera, Severine Niwemugizi na kisha yatafanyika mazishi ya kijeshi.

Mazishi hayo ya kijeshi yatahusisha gwaride la mazishi na upigwaji wa mizinga 21 kutoa heshima kwa aliyekuwa Amiri Jeshi Mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama.

Tukio hilo litahitimisha safari ya mwisho ya maisha ya Rais Magufuli aliyefariki dunia Machi 17, katika Hospitali ya Mzena, Dar es Salaam alikokuwa akitibiwa ugonjwa wa umeme wa moyo uliomsumbua kwa zaidi ya miaka 10.

Pia soma>> Askofu Niwemugizi: Rais Magufuli aliagiza nirejeshewe Passport yangu na alisema 'Wewe ni Askofu wangu utanizika'

Ibada za wafu, hizo sifa zoe angepewa tu Mungu na si mwanadamu.
Kuna watu wanamsifia na kumtukuza kuliko wamsifiavyo Mungu na wake zao.
 
BURIANI MAGUFULI: Ibada bado inaendelea uwanja wa Magufuli, Chato ambako kuna Kanisa la muda lililoandaaliwa kwaajili ya ibada ya mwisho ya Hayati Dkt. John Magufuli
azamtvtz_164151312140215658024818411515791340482920n.jpg


Baadhi ya waombolezaji waliopo hapa uwanja wa Magufuli, Chato ambapo itafanyika ibada ya mwisho ya kuaga mwili wa Hayati Dkt. John Magufuli.
Tayari viongozi mbalimbali akiwemo Waziri Mkuu Kassim Majaliwa wameshawasili katika eneo hili.
4.jpg
3-1.jpg
2-1.jpg
1-1.jpg


azamtvtz_16449698316452373590202414114400398866815395n.jpg


 
Aidha pia alisuggest mwili wa JPM usizikwe Bali ukaushwe na kwekwa kumbukumbu kwa vizazi vijavyo. Amesema siku ya maziko kutanyesha mvua kubwa sana iliyoambatana na radi nchi nzima ikiwa watamzika.

Na hiyo ni ishara ya ardhi kulaaniwa kwani jpm hajafa kifo naturally kama inavyosemekana Bali kuna watu wamehusika.
Pia kutatokea misiba mfululizo ikiwa wafanya hivo

Moderator msiifute hii thread.let's keep it tuone.huwezi jua.
Pasipo maono taifa huangamia.

Screenshot_20210326-121533.jpg
Screenshot_20210326-121457.jpg
Screenshot_20210326-121239.jpg
Screenshot_20210326-121230.jpg
 
Back
Top Bottom