Aliyemchoma Mwanamke visu 25 na kumsababisha Kifo afariki dunia akiwa chini ya ulinzi

Aliyemchoma Mwanamke visu 25 na kumsababisha Kifo afariki dunia akiwa chini ya ulinzi

View attachment 2859929
Mtuhumiwa anayedaiwa kusababisha kifo cha Beatrice Minja kwa kumchoma visu mara 25, Lucas Tarimo amafariki dunia akiwa chini ya ulinzi wa Jeshi la Polisi wakati akiendelea na matibabu katika hospitali ya Huruma iliyopo Wilaya ya Rombo, mkoani Kilimanjaro.

Daktari kiongozi wa Hospitali ya Huruma wilayani hapa, Daria Mushi amethibitisha kutokea kwa kifo chake ambapo amesema amefariki jana Jumatatu, Januari Mosi, 2024 saa nne na nusu usiku.
Watu mnatakiwa kujuwa,: ukisha mwaga damu ya binadamu mwezako, hata usipo kamatwa au kufahamika, azabu utakayo ipata ukiwa bado Hai ni kubwa kuliko uliye muuwaji. Kamwe usiuwe kwasababu yoyote ile. Ukiuwa maana yake na wewe uliye uwa unakuwa umeuwa nafusi yako mwenyewe kabla hujafa kimwili.
 
Kabisa mkuu, Shida huazia hapa, Kati yao mwingine kuingia mazima alafu anajisahau kama kuna kuachana kisha anawekeza vitu vingi kuliko hata kwa wazazi wake.
Sijui kwanini tunapenda kung'anganiana wakati hatupendani
 
View attachment 2859936
Pichani bw. Lucas Paul Tarimo anayetuhumiwa kusababisha umauti wa Beatrice Minja kwa kumchoma visu mara 25 mwilini. Naye inasemekana ameaga dunia leo alfajiri.

Sababu za kifo chake hazijawekwa wazi lakini inasemekana alipokuwa anakaribia kukamatwa alikunywa sumu. Inasemekana alipatiwa huduma ya kwanza kutapishwa sumu hiyo lakini amefariki baadaye.

Source: ndugu wa mtuhumiwa
Polisi aliempa tarimo chai ana huruma sana
 
Je, Amekufa kifo cha kawaida (natural death) au kuna mkono wa mtu??
Ni kwa nini siku zote hizo alikuwa bado yupo mahabusu ya Jeshi la Polisi badala ya kupekekwa katika Gereza la Mahabusu chini ya Jeshi la Magereza?????
Rudia kusoma. Amekufa akiwa hospitali ya Huruma akiwa akiwa chini ya ulinzi wa Polisi.
 
Polisi wamemkamata akiwa amekunywa sumu ili ajiue, wakawahi kumpeleka hospital,, nadhani hiyo ndiyo iliyomuathiri Hadi kupelekea kifo chake

Sent from my Infinix X6511B using JamiiForums mobile app

Kuna watu hawana cha kupoteza hawa wanauwezo wa kufanya chochote hata kujitoa uhai ili tu wawezi kujipa raha
 
Watu wa karibu kahakikisheni Kama kafa kweli na maiti muione.
Isije ikawa hao waliokua wanamlinda asikamatwe wakasingizia kifo ili Tarimo atoroke.
Hii point muhimu sana maana,amekamatwa baada ya kupigiwa kelele sana
 
View attachment 2859929
Mtuhumiwa anayedaiwa kusababisha kifo cha Beatrice Minja kwa kumchoma visu mara 25, Lucas Tarimo amafariki dunia akiwa chini ya ulinzi wa Jeshi la Polisi wakati akiendelea na matibabu katika hospitali ya Huruma iliyopo Wilaya ya Rombo, mkoani Kilimanjaro.

Daktari kiongozi wa Hospitali ya Huruma wilayani hapa, Daria Mushi amethibitisha kutokea kwa kifo chake ambapo amesema amefariki jana Jumatatu, Januari Mosi, 2024 saa nne na nusu usiku.
Si ndiyr yule alionja sumu baada ya kuona polisi?
Kuna comment ilisema kama mtu amekunywa sumu kwanini amalize dawa hospital maana hata akipona hukumu yake ni kunyongwa hadi kufa
 
View attachment 2859929
Mtuhumiwa anayedaiwa kusababisha kifo cha Beatrice Minja kwa kumchoma visu mara 25, Lucas Tarimo amafariki dunia akiwa chini ya ulinzi wa Jeshi la Polisi wakati akiendelea na matibabu katika hospitali ya Huruma iliyopo Wilaya ya Rombo, mkoani Kilimanjaro.

Daktari kiongozi wa Hospitali ya Huruma wilayani hapa, Daria Mushi amethibitisha kutokea kwa kifo chake ambapo amesema amefariki jana Jumatatu, Januari Mosi, 2024 saa nne na nusu usiku.
Duh!!!,Ngoja akashitakiane na mpenzi wake mbele ya Mungu.Huko hakuna Wakili wala rushwa.Hukumu ya Mungu ni very strait.Sheria yake ina Adili.

Sent from my V1901A using JamiiForums mobile app
 
Ukichaa wa akili ya binadamu ni ugonjwa mwingine ingawa hausemwisemwi sana....kuna jamaa huku anaanza mdogomdogo anasema huwa anajisikia kupiga kelele kali Kila anapokuwa peke yake au mahali penye utulivu.
 
Je, Amekufa kifo cha kawaida (natural death) au kuna mkono wa mtu??
Ni kwa nini siku zote hizo alikuwa bado yupo mahabusu ya Jeshi la Polisi badala ya kupekekwa katika Gereza la Mahabusu chini ya Jeshi la Magereza?????
Ali attempt kunywa sumu wakamuwahi nadhani sumu ilimzidiaaaa
 
Je, Amekufa kifo cha kawaida (natural death) au kuna mkono wa mtu??
Ni kwa nini siku zote hizo alikuwa bado yupo mahabusu ya Jeshi la Polisi badala ya kupekekwa katika Gereza la Mahabusu chini ya Jeshi la Magereza?????
Amekamatwa juzi ngorongoro na aoijarubu kunywa sumu kujiua ndo mana alikua bado hospitalized
 
Back
Top Bottom