Aliyeng'atwa na Nyoka afia Kituo cha Afya kisa hana 150,000 Wilayani Babati

Kwa nini Dr. Ndunguru hakuongea mwenyewe na hao wataalamu?

Amandla...
 
Poor training, supervision na management ya afya.

Ndio kiini cha tatizo, sera na sheria zipo wazi.

Kwanza katiba airuhusu discrimination ya huduma afya, pili lazima kuna sheria kwa kanuni za WHO medics hawatakiwi kumuacha mteja anaehitaji huduma yao hasa kwenye kuokoa maisha yake kumuacha kisa hana hela.

Kuna mambo luluki ya ku-justify na kuweza kuhutimisha shida ni management.

Kama wewe ni consultant unatakiwa uelezee tatizo la hii case. Msingi wa tatizo ni training ye (below par), kuna skills nyingi medics wanatakiwa kuwa nazo top of the list ni empathy (it’s the top of five pillars za medical ethics) kwa sababu wanakutana na vulnerable people ambao only their intervention can change the outcome.

Mtu kufa kisa kukosa, hela maana yake hawana empathy (top of the hierarchy on five pillars of medical medical ethics.

Hadi medics kutokuwa na empathy maana yake ni poorly trained and supervised. Na kama case hiko public maana yake wizara nzima ya afya imeoza.

Embu nchi iweke watu wenye uwezo wa kusimamia hiyo sector.
 
Hakika ni wanastahili kushitakiwa, mtu katoa laki na thelathini ila still mkewe anakufa kweli?
 
Shida iliyopo sasa watu wengi hawana passion na kazi zao ila wanafanya ili tu waweze ku survive kimaisha. Yani mtu focus ni mshahara wake tu.

Hio hali imeenea sector zote ndio maana mtu ana hofu ya kupoteza kibarua chake kiasi kwamba hata humanity hakuna. Tendo la ubinadamu tu ni mpaka uwe na hela. Watu wametanguliza maslahi mbele sana ila kuna situations zinaumiza sana. Imagine unapoteza mke kwa sababu ya uzembe wa madaktari. Nilishampoteza kaka kisa sh.elfu 5 ya sindano ya kulegeza kifua cha pumu.
 
Hiyo ni kazi kama kazi zingine .Mnahimizwa sana muwe na bima ya afya ila hamzingatii.

Wewe hapo unapofanya kazi unaweza kumuhudumia mtu bure?
Huu ni upumbavu wa hali ya juu, huduma ya afya ni tofauti na biashara zingine.

Emergency ya mtu anayehitaji instant treatment haipaswi kusubiria malipo. Huyo mgonjwa angepewa huduma stahiki kwa sasa angekuwa hai. What is 150,000 compared na uhai wa mtu. Chukulia aliyeafanyiwa hivyo angekuwa mama yako mzazi still ungeropoka the same way?
 
Huko hospital wamejaa vilaza waliofeli form four wakakosa option nyingine,wao hutumia nguvu badala ya akili.
Alafu labda mi sielewi mgonjwa akilazwa si bill ni badae?
Wapumbavu sana tena nina hakika hao waliokuwa wanamkwepa ni wanawake wenzake kabisa😐. Sizungumzi kwa ubaya ila in case mtoto au mke wangu akifa kwa uzembe wa aina hio sitaacha hao watu waishi. Nipo tayari kwenda kufia jela.
 
Ulipata bahati ya kugongngwa na nyoka asiye na sumu kali.
Kuna nyoka wana sumu kali balaa huyoboi kwenye dawa za ujanja ujanja.
 
Hii point, watu hawana passion na kazi zao
 
Kabisa, wanashindwaje hata ikibidi walatwe kwenye salary zao, sijajua ni mazingira ya namna gani yaliwafanya wasiwe na huruma kwa kitu urgent?😭
Sasa kama hujajua mazingi ra kwa Nini unahukumu! Ungeuliza kwanza ,hii michakato na urasimu ilichukua muda gani, na je mgonjwa alipelekwa Kituoni muda gani baada ya kugongwa nyoka,na je sumu ya hiyo nyoka inaruhusu haya yote! RIP mama Laizer tuna mengi ya kujifunza!
 
Goli la mama ni milioni tano
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…