Aliyewaonyesha kazi wavulana kidato cha nne huyu hapa.........

Aliyewaonyesha kazi wavulana kidato cha nne huyu hapa.........

Hongera mwanangu Lucy..
nimefurahishwa na mafanikio yako..
Watanzania wenzangu, inabidi tuwe positive..let's support these talents.
Lucy amepania kuwa daktari..huwezi kujua atakuwa mtaalamu wa kitu gani.
Tumtie moyo, huenda akaokoa maisha yetu wengi hapo baadaye atakapotimiza ndoto (profession) yake.
 
Inanisikitisha sana kuona matokeo ya kidato cha nne yanazidi kushuka. Watoto sijui hawasomi au ni mfumo?
 
lucymallya.jpg

MWANAFUNZI aliyeongoza mtihani wa kidato cha nne kitaifa mwaka 2010, Lucylight Mallya (18), amebainika kuwa ni yatima ambaye wazazi wake wote walifariki dunia miaka minne iliyopita.

Hongera binti.
Marian wameanzisha Marian boys huenda ndo sasa ikaja ikawa kinara wa shule za sekondari hapa nchini
 
Hongera sana Lucy,am proud of you......May God guide you and may you grow up to serve him with all that you have......:clap2::clap2::clap2:
 
Hongera binti...umewapa hesima mama na dada zetu kwamba wakipewa fursa sawa wanaweza
 
Sikubaliani na title japo nampa hongera zake kwa kufanya vizuri, kwani alikuwa anapambana na wavulana au alikuwa akipigania maisha yake, familia yake na taifa lake?
Hata hoja ya udini iliibuka kama hii, kuweni makini bwana!
 
Binafsi nampongeza huyu Binti, kama kweli pamoja na kutokuwa na wazazi wake amefanya hivi basi iwe changamoto kwa Yatima wengine na wote, kufiwa na wazazi kuna huzunisha ila isiwe kigezo cha kutaka kuhurumiwa tu, juhudi ni kazi na kushirikiana na walezi wengine mtu yoyote atafanikiwa na Mungu ni mwema.

Hongera baby, keep it up!
 
Msimwage hongera tu, changieni fedha bint aende form five manake ni yatima na baba mkubwa huko mererani hana uwezo wakusomesha yeye na wadogo zake watatu.... Alietayari kuchangia ani PM nimpe maelekezo ya jinsi yakuchangia hizo fedha....
 
hongera sana dada, ila tatizo la kina dada zetu wengi wakifika hatua ya chuo wanapwaya....

PP, umeibua hoja nzuri pia, hii ya baadhi ya wanafunzi (wavulana na wasichana) kufanya vizuri shuleni (oleve & Alevel) lakini wakifika vyuoni shule inwatesa sana..wanastruggle kweli mpaka unashangaa hivi ni mtu yule yule ambaye cheti chake cha form six kinaonesha ametapa div 1 ya point 3!

Mimi nadhani ni baadhi ya shule/walimu kuwadekeza sana wanafunzi katika ufundishaji...kwa msemo kimombo tungesema 'spoon feeding'. Kwa mtizamo wangu, wanafunzi walipitia kwenye shule ambazo walikuwa wanakuwa spoon fed, wakifika vyuoni wanapata tabu.
 
Dada hongera.

Lakini mimi nimejifunza kitu hapa. Kila mtu anapenda kuji-associate na mtu mwenye success na mafanikio! Its natural. No body wants to associate himself/herself with failure. So that should be a challenge. Kesho na kesho kutwa mambo yakeinda kivingine..ujue kabisa post za kukuponda zitakuwa mara mbili ya hizi. The choise is yours!

Masanja
 
PP, umeibua hoja nzuri pia, hii ya baadhi ya wanafunzi (wavulana na wasichana) kufanya vizuri shuleni (oleve & Alevel) lakini wakifika vyuoni shule inwatesa sana..wanastruggle kweli mpaka unashangaa hivi ni mtu yule yule ambaye cheti chake cha form six kinaonesha ametapa div 1 ya point 3!

Mimi nadhani ni baadhi ya shule/walimu kuwadekeza sana wanafunzi katika ufundishaji...kwa msemo kimombo tungesema 'spoon feeding'. Kwa mtizamo wangu, wanafunzi walipitia kwenye shule ambazo walikuwa wanakuwa spoon fed, wakifika vyuoni wanapata tabu.


Mkuu point nzuri. Mimi I was the opposite. Shule ilipwaya huko O and A levels..nilivyofika college ndo mambo yakawa sawa sawa kabisa. Perhaps hata mazingira tunayosoma wengine yanatuathiri maana kama sisi watoto wa wakulima wengi tunasoma shule za sikinde. So, it happens both ways. I am a living example.
 
Back
Top Bottom