Sesten Zakazaka
JF-Expert Member
- Sep 10, 2017
- 10,559
- 19,101
Jana saa tatu usiku katika kipindi cha Sports Roundup kinachorushwa na Clouds FM, mchezaji wa zamani wa vilabu vya Simba na Yanga ambaye siku hizi ni mchambuzi wa soka, Amri Kiemba alitoa madai mazito, ya kushtusha na yenye sura ya kijinai yanayoendelea kwenye soka letu
Kiemba alisema makocha wanaopewa kazi ya kusajili wachezaji kwenye vilabu vingi vya madaraja ya juu wanachukua kwa siri na kwa ubabe kinachoitwa commission kutoka kwenye ada za usajili za wachezaji wanaosajiliwa nao
Zaidi ya hapo alisema pia hata wachezaji husika wanapokua wamesajiliwa Makocha huchua asilimia fulani kutoka kwenye mshahara yao ili waendelee kubakia kwenye club vinginevyo wakikataa hufanyiwa zengwe na figisufigisu kwa kuwekwa bench, kufanyiwa kampeni za kuwachafua na hata kuachwa kwenye sajili zinazofuata
Muongoza kipindi Alex Luambano alipomuuliza labda pengine suala hilo lipo kwa baadhi ya vilabu, Kiemba alikataa na akasema kwamba club na waalimu wenye mtindo huo ndio wengi zaidi kuliko ambao hawafanyi hivyo!!!!
Amri Kiemba ni mdau wa michezo na alikua mchezaji wa ligi kuu na timu ya Taifa. Kwahiyo ana uhakika wa anachokisema hasa ukizingatia madai yake kayatoa hadharani kwenye chombo rasmi na kikubwa cha habari
Natoa wito kwa mamlaka husika za soka na za uchunguzi wa jinai nchini zifanyie kazi madai haya mazito ambayo kama ni ya kweli basi ni tatizo kubwa na ni uhalifu dhidi ya vijana wetu. Jambo hilo inawezekana likawa miongoni mwa vyanzo vya kufifisha juhudi za vijana kupata maendeleo kwenye soka na kuishia kucheza mpira mchangani tu na kurudisha nyuma maendeleo ya soka letu
Kiemba alisema makocha wanaopewa kazi ya kusajili wachezaji kwenye vilabu vingi vya madaraja ya juu wanachukua kwa siri na kwa ubabe kinachoitwa commission kutoka kwenye ada za usajili za wachezaji wanaosajiliwa nao
Zaidi ya hapo alisema pia hata wachezaji husika wanapokua wamesajiliwa Makocha huchua asilimia fulani kutoka kwenye mshahara yao ili waendelee kubakia kwenye club vinginevyo wakikataa hufanyiwa zengwe na figisufigisu kwa kuwekwa bench, kufanyiwa kampeni za kuwachafua na hata kuachwa kwenye sajili zinazofuata
Muongoza kipindi Alex Luambano alipomuuliza labda pengine suala hilo lipo kwa baadhi ya vilabu, Kiemba alikataa na akasema kwamba club na waalimu wenye mtindo huo ndio wengi zaidi kuliko ambao hawafanyi hivyo!!!!
Amri Kiemba ni mdau wa michezo na alikua mchezaji wa ligi kuu na timu ya Taifa. Kwahiyo ana uhakika wa anachokisema hasa ukizingatia madai yake kayatoa hadharani kwenye chombo rasmi na kikubwa cha habari
Natoa wito kwa mamlaka husika za soka na za uchunguzi wa jinai nchini zifanyie kazi madai haya mazito ambayo kama ni ya kweli basi ni tatizo kubwa na ni uhalifu dhidi ya vijana wetu. Jambo hilo inawezekana likawa miongoni mwa vyanzo vya kufifisha juhudi za vijana kupata maendeleo kwenye soka na kuishia kucheza mpira mchangani tu na kurudisha nyuma maendeleo ya soka letu