MWISHO AKAJA KWENYE POINT
AKasema wamekuja na bidhaa ambayo ni package ya dawa lakini ni virutubisho. Wakasema wamefanya hivyo ili kuwasaidia watu hususani vijana watumie product hiyo kujikomboa kwenye umasikini.
Mchanganuo wa hiyo product sasa.
Ni kwamba kwanza unatakiwa uelewe kuwa hiyo product haitolewi bure. Ni package inayouzwa Shilingi 500,000.
Ndani yake kuna mchanganyiko wa dawa zenye kutibu magonjwa mengi ikiwemo kisukari, ugonjwa wa moyo, na Covid.
Lakini pia package hiyo unaweza kuitumia kama virutubisho tu hata kama sio mgonjwa.
Akatuwekea na picha ya mfumo wa ndani wa mwili wa binadamu ambao unatisha. Akatutajia jina la ugonjwa akisema ndio sababu iliyofanya mfumo wa ndani uwe na muonekano wa kutisha.
Baadaye akaweka picha nyingine inayoonesha mfumo wa ndani wa mwili wa binadamu upo clean.
Akatoa maelezo kuwa hapo ni baada ya mgonjwa kutumia product yao ndio ikaenda kufanya uponyaji.
Hivyo unachotakiwa kufanya ni kutengeneza pair. Ukinunua hiyo package utafunguliwa account na kiasi fulani cha pesa utawekewa kama kianzio ambacho ni 50,000.
Halafu ukimleta mtu mwingine hapa akanunua tena package yetu maana yake utapata shilingi 50,000 ambayo nayo itaingia kwenye account yako iliyotengenezwa.
KWa hiyo naye huyo mtu akileta mtu mwingine ndivyo utavyozidi kutengeneza hela kupitia pair.
MASWALI NILIYOWAULIZA
Niliponyoosha mkono kutaka kuuliza swali akaniruhusu.
SWali lilikuwa ni hili
Ikiwa kama kweli nyinyi mmeamua kumsaidia kijana ajitoe kwenye umasikini kwanini muweke gharama kubwa ya kununua hiyo bidhaa?
Je ni kweli mna amini mtu anayeweza kuwa na laki 5 ni mtu ambaye anahitaji kusaidiwa kuepukana na umasikini?
NImesikia kuna watu humu mnamiliki majumba na utajiri wa kifahari. Mwingine kasema ana
miliki 150M. Sasa akitoa 10M akatununulia hiyo product atakuwa amesaidia watu wangapi kuwainua kiuchumi?