ALLIANCE GLOBAL: Kampuni ya kitapeli inayoendelea kuliza wasomi wengi nchini

ALLIANCE GLOBAL: Kampuni ya kitapeli inayoendelea kuliza wasomi wengi nchini

MWISHO AKAJA KWENYE POINT


AKasema wamekuja na bidhaa ambayo ni package ya dawa lakini ni virutubisho. Wakasema wamefanya hivyo ili kuwasaidia watu hususani vijana watumie product hiyo kujikomboa kwenye umasikini.


Mchanganuo wa hiyo product sasa.

Ni kwamba kwanza unatakiwa uelewe kuwa hiyo product haitolewi bure. Ni package inayouzwa Shilingi 500,000.

Ndani yake kuna mchanganyiko wa dawa zenye kutibu magonjwa mengi ikiwemo kisukari, ugonjwa wa moyo, na Covid.

Lakini pia package hiyo unaweza kuitumia kama virutubisho tu hata kama sio mgonjwa.

Akatuwekea na picha ya mfumo wa ndani wa mwili wa binadamu ambao unatisha. Akatutajia jina la ugonjwa akisema ndio sababu iliyofanya mfumo wa ndani uwe na muonekano wa kutisha.

Baadaye akaweka picha nyingine inayoonesha mfumo wa ndani wa mwili wa binadamu upo clean.

Akatoa maelezo kuwa hapo ni baada ya mgonjwa kutumia product yao ndio ikaenda kufanya uponyaji.

Hivyo unachotakiwa kufanya ni kutengeneza pair. Ukinunua hiyo package utafunguliwa account na kiasi fulani cha pesa utawekewa kama kianzio ambacho ni 50,000.

Halafu ukimleta mtu mwingine hapa akanunua tena package yetu maana yake utapata shilingi 50,000 ambayo nayo itaingia kwenye account yako iliyotengenezwa.

KWa hiyo naye huyo mtu akileta mtu mwingine ndivyo utavyozidi kutengeneza hela kupitia pair.

MASWALI NILIYOWAULIZA

Niliponyoosha mkono kutaka kuuliza swali akaniruhusu.

SWali lilikuwa ni hili

Ikiwa kama kweli nyinyi mmeamua kumsaidia kijana ajitoe kwenye umasikini kwanini muweke gharama kubwa ya kununua hiyo bidhaa?

Je ni kweli mna amini mtu anayeweza kuwa na laki 5 ni mtu ambaye anahitaji kusaidiwa kuepukana na umasikini?

NImesikia kuna watu humu mnamiliki majumba na utajiri wa kifahari. Mwingine kasema ana
miliki 150M. Sasa akitoa 10M akatununulia hiyo product atakuwa amesaidia watu wangapi kuwainua kiuchumi?
Safi boss,tutoe tongotongo
 
Wakuu,kuna hii inaitwa NEO LIFE,naomba mnaoifahamu mtupe ABC zake.
Kuna mwana ananishawishi kujiunga ili niuze dawa zao
 
Ukilizwa basi wewe jione bado ni mjinga na sio msomi kama heading ya maada isemavyo
 
Saiz imepanda mana ilikuaga500000
Ndiyo, imepanda hadi 600k na unahimizwa pia kwenye fomu yao ya kujiunga ni vyema zaidi ukiwekeza zaidi ya hiyo hili upate zaidi.

NB: Wanajibatiza majina mengi hili wasifahamike kiurahisi na hutumia technique hiyo kupoteza wafuasi wao, hivi sasa wanajiita EMPOWERED ENSURING lakini deep down ni ALLIANCE GLOBAL iliyochangamka ukiwa makini utabaini hilo kupitia fomu zao za makubaliano batili.
1857996339.jpg
876537872.jpg
1039635287.jpg
 
Back
Top Bottom