ALLIANCE GLOBAL: Kampuni ya kitapeli inayoendelea kuliza wasomi wengi nchini

ALLIANCE GLOBAL: Kampuni ya kitapeli inayoendelea kuliza wasomi wengi nchini

Katika simulizi yake; yeye ni graduate na hana kazi, sasa katika pilika pilika za kutafuta job akaambiwa na baba yake ambaye ni msataafu kuwa kuna kijana wa mzee fulani anayefahamiana naye toka kijiji X kwa sasa kafanikiwa huko jijini Mwanza kimaisha baada ya kuajiriwa kwenye kampuni fulani inayodili na biashara ya online marketing.

Pia kijana huyo alimwahidi baba yake kuwa atamuunganisha binti yake aajiriwe halipo yeye, kikubwa huyo baba (mstaafu anajulikana siku zote pensheni inasoma) awe tiyari kuchangia bidhaa zao za virutubisho kwani nje na kumtibia BP pia itamwongezea (bintiye) sifa za ziada kwa mabosi wake kumkubalia kirahisi kuungana nao kwenye biashara hiyo, bila hiyana mzee wa watu kwa ajili ya bintiye kupata kazi akaona isiwe tabu akakubali kupigwa kwa kununua kwanza bidhaa hizo za virutubisho (kwa Tsh.200,000)na akasafirishiwa kwa njia ya basi hadi huko kijijini kwao.

Baada ya hapo ni zoezi la kuja mjini ambapo mzee akahakikishiwa kuwa binti yake aje tu kwanza na kiasi cha shilingi 30,000 ambazo ni kwa ajili ya kitambulisho na kujiandikisha, ila asiofie pakufikia mwanaye kwani huko kazini wanahosteli nzuri na salama kwa ajili ya kufikia wafanyakazi wao waliotoka mbali, mpaka pale watakapozoea mazingira ya kazi wanaeza enda kupanga kikubwa aje na pesa ya kula tu (kwa kuwa kijana anahaminika kwa wazee na pale kijijini ni mtu mwenye heshima yake mzee akamruhusu binti achangamkie fursa)

Binti anaeleza kuwa mojawapo ya kitu kilichomvutia kuhusu kazi husika ni pamoja na kuambiwa kuwa atafanya kazi katika kampuni nzuri, yenye ofisi kubwa na makompyuta ya kutosha kinachotakiwa ni yeye tu kuja kuripoti na kuelekezwa mara moja namna ya kuuza bidhaa mtandaoni kisha aanze kuvuta mshahara wa bila jasho kwa kuwa wao hawatembezi bidhaa juani kama machinga, wao shughuli zao zote huishia mtandaoni na unalipwa vizuri kila sekunde unapofanya mihamala hawasubiri tu hadi mwisho wa mwezi (japo mshahara mwisho wa mwezi pia upo palepale)

Sasa binti anakwambia kuwa alikuwa akiwasiliana na huyo tapeli X kwa njia ya simu tokea ameondoka kwao mpaka anafika stendi ya mabasi Nyamhongolo kila mara alikuwa anapewa maelekezo ya namna ya kufanya, sasa siku ile anakuja kwa bahati mbaya gari alilopanda (binti) lilipata hitilafu likaharibikia njiani hivyo akafika Mwanza mida ya jioni kabisa, alivyowasiliana na tapeli X akamwambia kama vipi tafuta lodge yeyote iliyokaribu nawe ulale mpaka kesho ndiyo uje ofisini kwa maana sisi shughuli zetu mwisho saa 9:30 mchana hivyo hatuna namna ya kukusaidia.

Binti japo Mwanza hapajui ila alikuwa akipita maramoja moja akielekea huko chuoni kwao Morogoro kuna mtaa alikuwa ana-idea nao (Igoma) hivyo akaendazake kutafuta malazi hapo hadi kesho yake ambapo ndipo siku nilipokutana nae akiwa anaelekea kwa wazee wa kazi kupigwa....

"Tunaendelea sasa na pale tulipoishia...baada ya kugundua ni mgeni na kisha kunieleza vile kuwa kuna kampuni hapo mitaa ya CCM Kirumba sijuhi ameitishiwa kazi mara imepanda mara imeshuka mmh! nikawa na mashaka ndipo ikabidi nianze kumdodosa kiundani kuhusiana na kampuni husika.

Kumhoji dada wa watu kwani Kampuni yenyewe inaitwaje? Akaniambia hata na yeye hajui bado maana kila alipojaribu kumhoji jamaa ni kama alikuwa anamumunya maneno na hasikiki vizuri, kama utani nikamwambia wasije kuwa ni matapeli hao! Dada wa watu akashtuka ila kwa ujasiri akanijibu haiwezekani yule kaka hawezi kufanya hivyo tunaheshimiana sana, nikamuuliza kwani ndiye huyo muda wote mlikuwa mkizungumza nae, akanijibu hapana huyu ni mwingine kaniambia anaitwa X naye anafanya kazi kampuni hiyohiyo kapewa namba zangu na yule mtu aitwaye X hili aje anipokee, sasa ndiye mara kwa mara nawasiliana nae (hapa kwa uzoefu tu nikawa nishausoma mchezo unaoendelea siyo mzuri wenda kuna shida mahali)

Hapo hapo nikauvaa moyo wa huruma nakadhamira kale ka kusaidia jambo lisilonihusu ikawa inaniijia akilini ila najaribu kuyashinda majaribu, hatimaye tukafika Natta japo sikuwa na mpango wa kushuka ila nikajikuta nashukia pale kumsaidia binti wa watu na kazini nikapiga simu ya hudhuru ya kuchelewa kidogo (sijui kwa kuwa ni mrembo ndiyo maana
najikuta mwana wa Zebedayo[emoji23])

Nikamsindikiza mpaka stendi ya daladala ya makoroboi, palepale akapigiwa simu kuulizwa alipo (nikamwambia ajibu vipi) hapohapo jamaa akatuma meseji kuwa kuanzia hapo wawasiliane kwa meseji kwani yupo ofisini, basi tokea hapo chating zikawa ni zile za namna ile nilishazizungumzia mwanzoni hatimaye tukafika kituo cha daladala cha misheni jirani na rock city mall mahali tuliposhukia,

Wakati tunatembea kuitafuta furahisha kwa mujibu wa maelekezo ya tapeli nambari mbili, ikanibidi nitafute jambo la kupotezea ka muda hili nimchane binti hatari inayomkabili na nimpange cha kufanya kwa kuwa muda sasa ni karibia saa nne asubuhi najua tumbo linadai nikampitisha mgahawa mmoja jirani na hapo uwanja wa furahisha kupata kifungua kinywa (ambao ulikuwa hauna wateja wengi nyakati hizo) nikamfungukia wasiwasi wangu wote kuhusiana na kampuni hiyo X ninayohisi ni ya kitapeli na nikampanga cha kwenda kufanya akifika huko (mwanzoni alionesha kutoniamini kabisa tena kuna kale kamtizamo ka dharau fulani hivi machoni mtu akiwa anakueleza jambo usilokubaliana nalo alikuwa nako, ila akazidi kunihakikishia kuwa anajua hamna shida anaamini hizo ni hisia zangu tu ila hamna inshu)

Baada ya chai mie nikampa assignment ya kuniripotia kila kinachoendelea kwa SMS na aende ila asitoe pesa wala chochote kile hata begi lake ikitokea ameombwa lipelekwe mahali popote pale asikubali, nikamwacha mie nikaenda zangu kazini,

Sasa yaliyoendelea huko seminani ndiyo hayo nilishayaelezea yote, baada ya kutoka job ikabidi nimpitie binti wa watu hapo VILLA PARK (mahali walikokita kambi-matapeli) nikampeleka kwenye restaurant za jirani kula huku ananisimulia kila kilichojiri tokea tumeachana mpaka muda huo, nikamwambia sasa si unaona nilichokueleza tokea mwanzo,

Palepale binti bila kujizuia akaanza kuangua kilio akifikiria alivyodanganywa na uhalisia ulivyo, pili akinishukuru kwa wema niliomwonesha, kama gentleman nikajiongeza na leso mkononi hili binti afute machozi huku nikimfariji kwa kuishinda mitihani ya utapeli na punde mipango ya kurejea alikotoka ikafanyika nami sikuwa na la ziada tena katika simulizi hii nikawa sina budi kuishusha kalamu yangu chini kufikia hitimisho.
Dah! Mkuu ahsante sana kwa simulizi yenye kufundisha.

Mara nyingi utapeli unaonasa na kukumata ni ule utapeli unaounganishwa kwa kupitia jamaa yako wa karibu ama ndugu ili kukutoa wasiwasi wa kupeleka shingo kibra!

Na mtu akiisha ingia kwenye target ya kupigwa huwaga ni vigumu sana kumnasua kutokana na namna ambavyo matapeli wanajua sana namna ya kuinterrupt saikolojia ya mhanga.
 
Dah! Mkuu ahsante sana kwa simulizi yenye kufundisha.

Mara nyingi utapeli unaonasa na kukumata ni ule utapeli unaounganishwa kwa kupitia jamaa yako wa karibu ama ndugu ili kukutoa wasiwasi wa kupeleka shingo kibra!

Na mtu akiisha ingia kwenye target ya kupigwa huwaga ni vigumu sana kumnasua kutokana na namna ambavyo matapeli wanajua sana namna ya kuinterrupt saikolojia ya mhanga.
Ni kweli kabisa mkuu, mtu akishakuwahi akakuteka akili na kuiharibu saikolojia yako kujinasua ni mbinde mno, uwezi amini kuna ng'ombe iko busy sasa hivi na mafundisho ya Alliance global licha ya kusoma uzi huu lakini inaingia kibla na haitaki kukubaliana na ukweli kuwa inachokifanya si sahihi.
 
Huwa wanasikia basi?wanaona kama unawazibia riziki,kuna kakijana ka huko singida basi kalifika mjini mwanza sasa kutokana na kalivyonichukulia kama dada yake basi nikakauliza kamekuja kufanya nini mjini ndo kaanza kunielezea nikajua ni wale wa ajira!ajira nikakaelekeza vizuri,nikaona hakajaridhika sa ngapi hakajapigwa na kitu kizito mpaka nilikaonea huruma nikakakatia tiketi karudi kwao

Sent from my HUAWEI MLA-AL10 using JamiiForums mobile app
 
MWISHO AKAJA KWENYE POINT


AKasema wamekuja na bidhaa ambayo ni package ya dawa lakini ni virutubisho. Wakasema wamefanya hivyo ili kuwasaidia watu hususani vijana watumie product hiyo kujikomboa kwenye umasikini.


Mchanganuo wa hiyo product sasa.

Ni kwamba kwanza unatakiwa uelewe kuwa hiyo product haitolewi bure. Ni package inayouzwa Shilingi 500,000.

Ndani yake kuna mchanganyiko wa dawa zenye kutibu magonjwa mengi ikiwemo kisukari, ugonjwa wa moyo, na Covid.

Lakini pia package hiyo unaweza kuitumia kama virutubisho tu hata kama sio mgonjwa.

Akatuwekea na picha ya mfumo wa ndani wa mwili wa binadamu ambao unatisha. Akatutajia jina la ugonjwa akisema ndio sababu iliyofanya mfumo wa ndani uwe na muonekano wa kutisha.

Baadaye akaweka picha nyingine inayoonesha mfumo wa ndani wa mwili wa binadamu upo clean.

Akatoa maelezo kuwa hapo ni baada ya mgonjwa kutumia product yao ndio ikaenda kufanya uponyaji.

Hivyo unachotakiwa kufanya ni kutengeneza pair. Ukinunua hiyo package utafunguliwa account na kiasi fulani cha pesa utawekewa kama kianzio ambacho ni 50,000.

Halafu ukimleta mtu mwingine hapa akanunua tena package yetu maana yake utapata shilingi 50,000 ambayo nayo itaingia kwenye account yako iliyotengenezwa.

KWa hiyo naye huyo mtu akileta mtu mwingine ndivyo utavyozidi kutengeneza hela kupitia pair.

MASWALI NILIYOWAULIZA

Niliponyoosha mkono kutaka kuuliza swali akaniruhusu.

SWali lilikuwa ni hili

Ikiwa kama kweli nyinyi mmeamua kumsaidia kijana ajitoe kwenye umasikini kwanini muweke gharama kubwa ya kununua hiyo bidhaa?

Je ni kweli mna amini mtu anayeweza kuwa na laki 5 ni mtu ambaye anahitaji kusaidiwa kuepukana na umasikini?

NImesikia kuna watu humu mnamiliki majumba na utajiri wa kifahari. Mwingine kasema ana
miliki 150M. Sasa akitoa 10M akatununulia hiyo product atakuwa amesaidia watu wangapi kuwainua kiuchumi?
Bora hata sasa hivi kiasi imepungua,anko na kijana wake walipigwa 5M,binamu alikuwa chuo ghafla nikaanza kuona status akipost mambo,mara quotes za matajiri mara gari za ndoto zake,badae nikaona hapost tena kumbe ashapigwa na kitu kizito

Sent from my HUAWEI MLA-AL10 using JamiiForums mobile app
 
Huwa wanasikia basi?wanaona kama unawazibia riziki,kuna kakijana ka huko singida basi kalifika mjini mwanza sasa kutokana na kalivyonichukulia kama dada yake basi nikakauliza kamekuja kufanya nini mjini ndo kaanza kunielezea nikajua ni wale wa ajira!ajira nikakaelekeza vizuri,nikaona hakajaridhika sa ngapi hakajapigwa na kitu kizito mpaka nilikaonea huruma nikakakatia tiketi karudi kwao

Sent from my HUAWEI MLA-AL10 using JamiiForums mobile app

Hii generation inakabiliwa na mitihani migumu sana, vijana wanaumizwa mno na hawa matapeli na elimu hii kwa jamii haitolewi kwa mapana yake nadhani kwa kuwa vyombo husika na vile vya kusimamia haki navyo itakuwa kuna namna wananufaika katika mnyororo huu wa dhuluma lasivyo vitendo kama hivi visingeachwa viendelee katika jamii zetu pasipo kukemewa wala kukomeshwa.
 
Bora hata sasa hivi kiasi imepungua,anko na kijana wake walipigwa 5M,binamu alikuwa chuo ghafla nikaanza kuona status akipost mambo,mara quotes za matajiri mara gari za ndoto zake,badae nikaona hapost tena kumbe ashapigwa na kitu kizito

Sent from my HUAWEI MLA-AL10 using JamiiForums mobile app
Dah inauzunisha sana 5M huo ni mtaji ambao ungemtoa kabisa kimasomaso, ila kwa ujinga wake akaenda kuwakabidhi matapeli na yeye kurudia msemo wa ng'ombe wa maskini.
 
Hata hawa wazee wa Forever Living.
Ni hayo hayo, wazee wa pyramid schemes unafanya kazi kwa kushirikishwa nawe unashirikisha wengine, kisha unamuuzia mtu bidhaa zake kwa kuforce market, unapambana vilivyo ku-push mzigo uende hata kama soko ni gumu kiasi gani huko radhi hata kumdhulumu mteja kwa bei isiyo halali, mwisho unachoambulia ni kiduchu ukilinganisha na efforts pamoja na fedha ulizowekeza, kama ni mjanja na una-wish kufanya wanachofanya basi jifunze kuhusu mfumo wao unavyofanya kazi nawe anzisha wakwako otherwise achana na hizi mambo zimejaa utapeli na ubabaishaji mno.
 
huu ujinga niliukataa sana licha ya kuwa na marafiki wa karibu waliojiunga baadae walilia vilio vya mbwa mwizi
 
Dah inauzunisha sana 5M huo ni mtaji ambao ungemtoa kabisa kimasomaso, ila kwa ujinga wake akaenda kuwakabidhi matapeli na yeye kurudia msemo wa ng'ombe wa maskini.
Nadhani hawatosahau mpaka wanaenda kaburini,make anko aliugua pressure 5M ya kijijini sio mchezo

Sent from my HUAWEI MLA-AL10 using JamiiForums mobile app
 
Nadhani hawatosahau mpaka wanaenda kaburini,make anko aliugua pressure 5M ya kijijini sio mchezo

Sent from my HUAWEI MLA-AL10 using JamiiForums mobile app
Dah pole yake maisha haya sometimes yana ukatili mno, imagine umetendewa hivyo afu unakutana na washenzi hao hao mahali pengine kwenye miangaiko yako eti bado wanaendelea na dhuluma za kuwapotosha wengine waingie mkenge na uruhusiwi kuwaghasi kisa wapo kisheria.
 
huu ujinga niliukataa sana licha ya kuwa na marafiki wa karibu waliojiunga baadae walilia vilio vya mbwa mwizi
Utapeli ni laana kubwa mno maana licha ya kunufaika na jasho la mtu visivyo halali moyoni unajibebea msalaba wa manung'uniko, simanzi na majonzi ya wale unaowatapeli. Kimwili unaonekana ni tajiri lakini kiroho umedhoofu na wala amani haipo nafsini mwako, kwani matendo yako maovu uendelea kukuwinda milele.
 
Utapeli ni laana kubwa mno maana licha ya kunufaika na jasho la mtu visivyo halali moyoni unajibebea msalaba wa manung'uniko, simanzi na majonzi ya wale unaowatapeli. Kimwili unaonekana ni tajiri lakini kiroho umedhoofu na wala amani haipo nafsini mwako, kwani matendo yako maovu uendelea kukuwinda milele.
ni kweli kabisa mkuu, nna classmate wa chuoni hadi leo hii anateseka na haya maaliance sijui karogewa
 
ni kweli kabisa mkuu, nna classmate wa chuoni hadi leo hii anateseka na haya maaliance sijui karogewa
Kuna tapeli mmoja nilikuwa nabonga nae pasipo yeye kutambua kama namchora, akanitonya kuwa wakati wa Magufuli hizi mambo zilipigwa stop ila awamu ya Mama ndiyo inaupiga mwingi, chakujiuliza je serikali hii inauchungu na affair za wananchi wake hasa vijana?

Kwa maana kampuni za namna hii hivi sasa zimeenea nchi nzima na zinakusanya pesa za walalahoi kama njugu na zinapotosha vijana wadogo wadogo waliomaliza form four mpaka ngazi za juu za elimu kwa kuwakamua wazazi masikini pesa kwa njia ya ulaghai na serikali yao ikibariki suala hili, pesa ambazo zingetumika kuwaendeleza vijana hawa kujiajiri, kiujuzi au kibiashara.
 
Ni kama akina chenza, unapewa sabuni na mafuta utembeze mitaani kama mchuuzi! Ukileta mtu unapewa commision huku ukiwa na matumaini ya kufika level za meneja [emoji23][emoji23][emoji23]
 
Ni kama akina chenza, unapewa sabuni na mafuta utembeze mitaani kama mchuuzi! Ukileta mtu unapewa commision huku ukiwa na matumaini ya kufika level za meneja [emoji23][emoji23][emoji23]

[emoji23]bora hii mtaji ni nguvu zako mwenyewe utachagua unyoe au usuke kuliko hawa akina forever unapigwa panga hata kabla ya kuanza hustle yenyewe[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Nyuzi kama hzi za kuwatahadharisha kuhusu utapeli ni nyingi sana sema watu nikama wamelogwa ivi wanekuwa vichwa vigumu kuelewa .....huwezi amini pamoja na ushauri wote huu utakuta kuna punguani mwingine atajichanganya aka tapeliwe na kuja hapa kulia lia ..... kwenye haya maisha hakuna shortcut kwenye mafanikio utapigwa kama ngoma na usomi wako na kugeuzwa fursa
 
Haaaah! Hivi hawa jamaa bado wapo??

Nawakumbuka hawa kwenye season ya Corona

ILIVYOANZA

Mwaka juzi kuna dada mmoja mtaani naheshimiana naye sana akaniomba siku ya jumamosi nikahudhurie semina.

Ni mtu ambaye namheshimu sana na aliponiambia hivyo hata sikuwa na wasiwasi nikasema sawa basi nitamwambia na rafiki yangu ili twende wote.

Kweli ilipofika jumamosi tukachomoka wote watatu mpaka pale mwenge kwenye stand ya daladala kuna ki ghorofa fulani ambacho floor ya juu kuna ukumbi.

Basi tukafika pale kwanza kila mtu naye muona pale kama ni mwanaume basi amegonga suti afu na funguo zina hang kwenye lux ya suruali.

Kulikuwa na baadhi ya watu ambao walivaa kawaida ambao baadaye hao ndio nilikuja kufahamu kuwa ni wageni kama sisi wamekuja hapo kwa ajili ya kusikiliza hiyo semina.

Ilikuwa majira ya saa 7 ndio semina inaanza, akaoita jamaa mmoja mbele akiwa na projector akatusalimia "Helloooo" akifuatia na Good morning japo ilikuwa ni mida ya mchana.
Mwendelezo tafadhali [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji119]
 
Back
Top Bottom