ALLIANCE GLOBAL: Kampuni ya kitapeli inayoendelea kuliza wasomi wengi nchini

ALLIANCE GLOBAL: Kampuni ya kitapeli inayoendelea kuliza wasomi wengi nchini

Hakuna ufala kama masikini kumwibia masikini mwenzie..siku zote ukiona utapeli unafanyika na usiposema juu ya utapeli huo jua na wewe ni tapeli.
Kwa jinsi ulivyo elezea unaonekana na wewe ni mwenzao sema wamemurusha ndo maana umekuja kuwachomesha.

Malipo ni hapa hapa ndugu yangu
 
Hio mbona kitambo sana tunaifahamu..Acha wajinga waliwe...katika maisha haya tafuta mfumo wa kuwapiga wajinga ni wengi mnooo
 
Yaani hadi inatia hasira, kwanini vijana wa siku hizi hatuna ufuatiliaji wa mambo, unaambiwa kuhusiana na Kampuni usiyoifahamu vyema kama msomi na mkononi una simu janja kazi kufuatilia stori za mwijaku na baba levo, unashindwa kuingia Google uandike Alliance Global utapeli uone kama utapata walahu dondoo kuhusu experience za users i.e kwenye Google kuna makala ya gazeti la Mwananchi kuhusiana na utapeli wa Alliance Global huko Kilimanjaro n.k, Umeshindwa huko basi pitia Jamii Forums, Haya tuseme facebook ingia search andika Alliance Global moja kwa moja itakuijia video ya makala ya Ripoti Maalum kutoka ITV..June 15, 2022 kuhusiana na matukio ya hawa matapeli n.k

wanasema mwafrica ukitaka kumnyima maarifa yaweke katka mfumo wa maandishi.

fikiria ndugu yetu huyu katoa elimu kupitia JF,kuna kirundu amekaa sehemu na ana degree hajui hata JF ni kitu gani[emoji28][emoji28][emoji28].

yaani huyu ni mhanga ajaye wa Alliance Glabal mpya yenye jina jingine lakini lengo likiwa lile lile kupiga mazezeta.watu hawako aware kabisa na hivi vitu wanaishi kama maiti.
 
Hawajibu maswali wale

Walichoniambia ni kuwa hilo swali atakujibu aliyekuleta.

Nikawaambia atanijibuje huyu wakati yeye bado sio mnufaika wa hii biashara kama nyinyi.

Hamuoni kama naye huyu yupo hapa kujifunza na moja ya sababu za kumfanya atoe hela ni pale anapokuwa hana mashaka na hii biashara.

Na mashaka yetu yanahitaji majibu mazuri kutoka kwenu ili yaweze kuondoka.

Hawakujibu kitu wakanisisitiza nije semina ya pili nitapatiwa majibu nikaamua kuwapotezea.

jamaa yangu aliitwa na wale jamaa wanajiita Qnet 2018[emoji28][emoji28]akapigwa seminar ya kutosha kwa maelezo yake anasema aliwaelewa kabisa,kimbembe kikawa kiingilio.

anasema aliporuhusiwa kuuliza swali akiwa tayari na goosebumps akauliza,sasa bro si unikope hiyo 5mln niingie then baada ya mwezi nikianza kuingiza $$$$ unakata percent yako mpaka hela yako irudi[emoji28][emoji28],jamaa akamjibu kwa swali,kwani hakuna hata sehemu unaweza kukopa au hata kuuza mali uliyo nayo ukapata hiyo hela???

mwamba kwa swali hilo akili ikafunguka,kumbe lengo hapa ni hii 5mln yangu sio mimi nifanikiwe,akaaga na kusepa[emoji23][emoji23]
 
jamaa yangu aliitwa na wale jamaa wanajiita Qnet 2018[emoji28][emoji28]akapigwa seminar ya kutosha kwa maelezo yake anasema aliwaelewa kabisa,kimbembe kikawa kiingilio.

anasema aliporuhusiwa kuuliza swali akiwa tayari na goosebumps akauliza,sasa bro si unikope hiyo 5mln niingie then baada ya mwezi nikianza kuingiza $$$$ unakata percent yako mpaka hela yako irudi[emoji28][emoji28],jamaa akamjibu kwa swali,kwani hakuna hata sehemu unaweza kukopa au hata kuuza mali uliyo nayo ukapata hiyo hela???

mwamba kwa swali hilo akili ikafunguka,kumbe lengo hapa ni hii 5mln yangu sio mimi nifanikiwe,akaaga na kusepa[emoji23][emoji23]
Wezi wale bora jamaa alisanuka mapema
 
Daaah nimecheka sana shuhuda za wadau hapa [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji114]
 
Watotl wa kibongo wengi wanapenda mafanikio ya haraka mwisho wengi wanaishia kutapeliwa
 
Vanilla kilo 1 = 1,000,000
Afu hawa bado nawasikia kwenye kipindi cha michezo cha Wapo Radio wanaendelea kufanya promosheni

Japo humu kuna mdau alileta habari kuwa tayari watu washapigwa, ila inaonekana Vanilla hawajafikia malengo ya idadi ya watu waliopanga kuwapiga na ndio maana promo inaendelea
 
Hapo kahsaletwa mrembo mkaliii anakokota begi

Eti katua kutokea Ohayo Missouri kwenye maonyesho na kilele Cha mafaniko ya bidhaa na testimonies za watu mashuhuli..... Eti huyo ndio yule tulikuwa tunaongea nae akiwa kwa Flight ameunga kuwawahi ..me mbavu sina.[emoji23][emoji23]
Aisee tutafika mbinguni tumechoka sana na hawa matapeli uchwara[emoji23][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
hata universisty abroad ya mtu anaitwa Tonny ya kupeleka wanafunzi nje ya nchi ni matapeli kuliko matapeli wote duniani mshenzi sana huyo TONNY na genge lake ofisini
Nitaanzisha Uzi wa kutaja makampuni yote ya Kitapeli.

Hapa nimeshagundua kuna

-MTFE
-GLOBAL ALLIANCE
-TONNY
-Q-NET

Endelea.........
 
Ahahaha na wabongo tunavyoamini mtu anae miliki Gari ndio mwenye pesa na tajili lazima watu walizwe [emoji848] watu wanacheza na akili tu

Sent from my A37fw using JamiiForums mobile app
Kuna motivation spika mmoja enzi hizo nilikuwa natoka na sista'ake, hivyo kila day akosi kuja kumpiga dada mtu mizinga ya mafuta kwa ajili ya gari lake na kila day mchana na jioni lazima aje kula, sasa siku moja nipo na washkaji tumeongozana sikujua mara moja wanaelekea wapi nikawafata tu, saa ngapi wasizamie kwenye ukumbi fulani wakaniambia kuna mchongo mmoja wa fursa za pesa upo mahali hapo tusikilizie,

Tukatafuta chobingo moja tukajiseti kupata mawaidha ya kifilipino na kijack mali, wakati motivesheni speech yakutusuka inaendelea kiasi tumeanza kukonvisika, ghafla tukaambiwa anaingia mtu mzito aliyefanikiwa kupitia mpango biashara huo na tukapewa cheo chake sijui executive what, Kijana akashuka kwa madaha na mwendo wa mikogo kutoka kwenye ist yake huku kaning'iniza funguo kibarobaro,

Kila mtu jicho kwake wakionesha kumu-admire, chakushangaza mimi na washkaji zangu ilikuwa nusra tupass out kwa mshangao huku tukijizuia iwezekanavyo ku-spoil shughuli kwa kuangua kicheko cha nguvu, kwani kamjaa kalikokuja si kengine bali kale kajamaa kanakokulaga kwa dada yake na huwa kananiudhi kila nikimgeia sista yake pesa ya kutumia kanapewa kenyewe na suti yake moja kauka nikuvae..nachokumbuka hakuna aliyemwambia mwenzie twen'zetu tulijikuta nje ya ukumbi wote tukiangua vicheko kama wendawazimu tokea siku hiyo huwezi niambia chochote kuwahusu hawa matapeli.
 
Unavyoitwa kwenye fursa wewe ndio fursa watu hawaitani kwenye hela aise
Ni kweli mkuu, katika dunia hii ya sasa siyo kila fursa ni fursa kuna fursa zingine wewe ndiye fursa yenyewe.[emoji23]
 
Kwa jinsi ulivyo elezea unaonekana na wewe ni mwenzao sema wamemurusha ndo maana umekuja kuwachomesha.

Malipo ni hapa hapa ndugu yangu
Hakuna siri ndugu yangu hapa duniani hata ungefanyia uvunguni bado watu watajua tu, kama ungekuwa makini stori yangu inamwelezea dada mmoja aliyetaka kuingizwa mjini kupitia mchezo huu wa kitapeli na nilichokielezea chote nimesimuliwa na huyo dada na nilimsindikiza mpaka eneo la tukio bila kusanukiwa na matapeli, na nikamwelekeza chakufanya aende tu kuwa-enjoy kama vile haelewi chochote kisha aniletee data za kinachojiri huko ukumbini.

NB: Hii siyo fiction story bali ni stori ya kweli na nilichokieleza sijajitungia bali ndiyo uhalisia, na hao wezi mpaka muda huu wako mahali husika nilipopataja kwenye uzi huu.
 
wanasema mwafrica ukitaka kumnyima maarifa yaweke katka mfumo wa maandishi.

fikiria ndugu yetu huyu katoa elimu kupitia JF,kuna kirundu amekaa sehemu na ana degree hajui hata JF ni kitu gani[emoji28][emoji28][emoji28].

yaani huyu ni mhanga ajaye wa Alliance Glabal mpya yenye jina jingine lakini lengo likiwa lile lile kupiga mazezeta.watu hawako aware kabisa na hivi vitu wanaishi kama maiti.
Ni kweli kabisa, vijana wa kisasa nowdays tunatumia interneti vibaya sana, yaani muda wote MB's zinateketea kuangalia video za ovyo (maselebu, pono, michezo,vichekesho)TikTok, facebook, X na instagram, kutwa nzima huna hata site moja uliyoitembelea kujihabarisha au kujinoa ufahamu matokeo yake unakuwa msomi mwenye stupidity ya hali ya juu na matokeo yake ni kukumbana na hakina Alliance Global.
 
Back
Top Bottom