Uchaguzi 2020 Ally Bananga atia nia ubunge Arusha mjini - CHADEMA

Uchaguzi 2020 Ally Bananga atia nia ubunge Arusha mjini - CHADEMA

Mimi Kafulila simjui kiasi cha kusema kuwa hakuwa na marafiki CCM ambao walisaidia kumshawishi ahamie huko. Vile vile simjui Banaga kiasi cha kusema kwa uhakika kuwa anatumika. Bahati mbaya uliishia kusoma nilichoandika kuhusu Kafulila. Hukusoma niliposema kuwa mke wake Kafulila hakumfuata mumewe CCM na amethibitisha pasipo shaka kuwa ni mfia chama chake. Banaga nae anaweza kuwa ni mfia chama kama alivyo mke wake Kafulila. Na inawezekana kabisa Lema kuwafuata nyendo za wakina Lijualikali na Slaa ingawa kwa mtazamo wa wengi huo uwezekano ni mdogo. Ninachokisema ni kuwa maswali ya commitment kwa chama chake yataulizwa zaidi kwa Banaga kuliko kwa Lema. Lakini commitment hiyo itathibitishwa zaidi kwa kila mmoja jinsi watakavyopokea kutoteuliwa nao. Kama watakubali matokeo na kumpigania atakaeteuliwa itakuwa ni uthibitisho zaidi kuwa wao ni wanachama committed wa chama chao. Kama watasusa au watahamia chama kingine basi itakuwa wamethibitisha kuwa hawakuwa committed.

Amandla...
Pia atakaepigiwa Kura za maoni nakushinda ,huko juu wasije wakakata majina ya watu, watakuwa hawana tofauti nayule aliesema itategemea nimeamkaje.
 
Leta ushahidi wa Dr Slaa kuchukua kadi ya CCM.
Kama nakumbuka vizuri ni kuwa hakuwahi kurudisha kadi yake ya CCM. Na sijui kama aliwahi kujitoa rasmi CCM. Lakini hizi zote ni speculations. Anaeweza kuthibitisha ni yeye na sioni sababu ya yeye kufanya hivyo. Ni mambo yake binafsi na inabidi tuyaache yawe hivyo.

Amandla...
 
Kwani Slaa kabla ya kuja Chadema haujui kwamba alikatwa huko CCM?

Weka ushahidi kwamba alishairudisha kadi ya CCM.
Unajua sifa za kupoteza uanachama cha chama cha siasa? Acheni siasa mgando hizo ...
 
Pia atakaepigiwa Kura za maoni nakushinda ,huko juu wasije wakakata majina ya watu, watakuwa hawana tofauti nayule aliesema itategemea nimeamkaje.
Hapana. Hapa tunatofautiana. Huko juu hawatakiwi kuwa rubber stamp. Wanachopelekewa ni mapendekezo na wanatakiwa kufanya uamuzi kwa kuangalia maslahi mapana zaidi ya chama. Kama Katiba yao inawapa uwezo huo basi ni wajib wa wanachama kukubali na kuunga mkono kwa dhati uamuzi wao. Kama wanataka kura za maoni ndio ziwe uamuzi wa mwisho inabidi wabadilishe Katiba yao. Sio kila chaguo la wapiga kura ni sahihi.

Amandla...
 
Kumbe huwa hamufuatilii mambo?? Dr slaa aliwahi hojiwa ITV miaka hiyo tena akiwa Katibu mkuu wa chadema kuhusu kumiliki kadi ya ccm, alijibu hv, kadi ni mali ya mwanachama hvyo kadi ni mali yng na ni kumbukumbu yangu...hvyo anayo ya ccm na pia anayo ya chadema
Kwahiyo miaka yote Chadema inajua ina katibu mwanaccm? Unajua kwanini wanaorudi CCM wanapenda upya kadi? Alafu alivyosema kadi ya CCM ni mali yake kwa kumbukumbu zake mbona mlimuelewa enzi zile? Si mngemtimua?
 
Kwahiyo miaka yote Chadema inajua ina katibu mwanaccm? Unajua kwanini wanaorudi CCM wanapenda upya kadi? Alafu alivyosema kadi ya CCM ni mali yake kwa kumbukumbu zake mbona mlimuelewa enzi zile? Si mngemtimua?
Unamtimuaje mtu ambaye kisheria ukishajiunga na chama kingine unakuwa umepoteza sifa ya kuwa mwanachama wa chama cha awali?? soma katiba uelimike
 
Hapana. Hapa tunatofautiana. Huko juu hawatakiwi kuwa rubber stamp. Wanachopelekewa ni mapendekezo na wanatakiwa kufanya uamuzi kwa kuangalia maslahi mapana zaidi ya chama. Kama Katiba yao inawapa uwezo huo basi ni wajib wa wanachama kukubali na kuunga mkono kwa dhati uamuzi wao. Kama wanataka kura za maoni ndio ziwe uamuzi wa mwisho inabidi wabadilishe Katiba yao. Sio kila chaguo la wapiga kura ni sahihi.

Amandla...
Inatakiwa waangalie maslahi mapana ya wananchi na wanachama, sio mtu hakubaliki na wanachama kisha umpitishe kuwa mgombea hapo jimbo litaenda ccm, hao wanachama wasipomkubali mtu huyo ndio ataenda kufanyanao kazi. Mimi hapo sikubalian kabisa , hapo inaleta mkanganyiko Kama wakubwa wahuko kamati kuu hawakukubali wanakata jina lako, utofauti na ccm kwa mantiki hio haupo, Kama wanashindwa kuheshima matakwa ya wanachama.
 
Unajua sifa za kupoteza uanachama cha chama cha siasa? Acheni siasa mgando hizo ...
Hivi karibuni kuna Mbunge alitangaza rasmi kuondoka chama kimoja na kuhamia chama kingine hadharani. Lakini Spika akamrudisha Bungeni aendelee kuwakilisha chama ambacho aliisha kikana kwa kusema chama chake cha awali kilikuwa hakijamuandikia barua ya kumfuta uanachama. Kwa mantik hii kama CCM haikumuandikia Spika wa wakati ule barua ya kumfuta uanachama Dr. Slaa basi aliendelea kubaki mwanachama wa CCM ingawa alikuwa anawakilisha CDM. Na CCM wanafanya makosa kuwapa kadi mpya wale wanaorudi ambao haikuwafuta uanachama rasmi.

Amandla...
 
Ili kutaka kujua kama anasifa za kuwa mbunge wa Arusha:
1. Jee ni Mchaga.
2. Ana nasaba zozote na waasisi wa chadema.
3. Ana ukaribu wowote wa kindugu, kijamaa, urafiki.
4. Jee ni mtiifu kwa Mbowe na genge lake ndani ya chama.
5. Ana msaada wowote kwa wafanyi biasha wakubwa na wasogo wa kichaga waliopo katika kata anazohidimia, hao ndio waxhangia wakubwa wa Mbowe na chama.
 
Huyu atakuja kujitoa katikati ya kampeni, ni team Lowasa.
Kwa hiyo hakuna faida yoyote ya mwanasiasa kuingia chadema, kwani kila mara watamuwekea vikwazo na kumkumbusha alikotokea.
 
Hii kushukiana ndio inapasua chama. Ziko standards za kupimana badala ya hisia na woga tu.
Mbona nyalandu hawamtilii mashaka kwa sababu bado anazo pesa alizozipiga alipokuwa waziri na alipiwauzia vitalu wamarekani
 
Inatakiwa waangalie maslahi mapana ya wananchi na wanachama, sio mtu hakubaliki na wanachama kisha umpitishe kuwa mgombea hapo jimbo litaenda ccm, hao wanachama wasipomkubali mtu huyo ndio ataenda kufanyanao kazi. Mimi hapo sikubalian kabisa , hapo inaleta mkanganyiko Kama wakubwa wahuko kamati kuu hawakukubali wanakata jina lako, utofauti na ccm kwa mantiki hio haupo, Kama wanashindwa kuheshima matakwa ya wanachama.
Wewe na mimi tunajua kuwa kura zinaweza kuwa corrupted. Tukumbuke pia mtu anaweza kukubalika na wanachama waliopiga kura lakini sio wanachama wote ( mara nyingi wapiga kura ni wachache kuliko wenye haki ya kupiga kura). Aidha, wasiokitakia mema chama wanaweza kuingiza watu kirahisi ili wampigie kura mtu ambae wanajua hana ushawishi katika jamii yake. Lakini ni kweli kabisa kuwa mara nyingi tuu wakubwa wametumia nafasi zao kumpitisha mtu ambae hakubaliki katika jamii. Wakifanya hivyo wananchi watawashikisha adabu kwa kumkataa katika uchaguzi mkuu. Aidha, ni kweli kuwa katika hili hawana tofauti na CCM. Tukumbuke kuwa kwa vile waanzilishi wengi walitoka CCM basi mambo mengi watakuwa waliyaiga kutoka chama pekee walichokijua. Kama inaonekana haifai, basi inabidi wanachama wakisukumize chama chao waibadilishe.

Amandla...
 
Kwa asili kila binadamu ni mbinafsi, ndio maana kwenye rasimu ya Warioba wananchi tulipendekeza mwisho wa ubunge uwe 10yrs. Lakini maoni yale yakachezewa na wahuni wachache kwa faida zao binafsi.
Wabunge wa upinzani wakiongozwa na Chadema walisusia bunge la katiba na kusababisha mchakato usikamilike.
 
Awe mwanachama wa kawaida siyo lazima agombee
Ok, kwa hivyo hakuna Democracy kama inavyosemwa. Mwanachama yoyote ana haki ya kugombea. Kama ni hivyo mtawavunja nguvu walio na nia ya kuhamia chadema.
 
Back
Top Bottom