Ally Kessy: Katiba sio msaafu, Rais Magufuli akimaliza muda wake tutatengua Katiba aongezewe muda | Spika Ndugai amuunga mkono

Ally Kessy: Katiba sio msaafu, Rais Magufuli akimaliza muda wake tutatengua Katiba aongezewe muda | Spika Ndugai amuunga mkono

Anafanya kwa mshahara wake?
Rais Magufuli kodi za wanachi anazisimamia vizuri.
Wakati pesa za ruzuku Mbowe kashindwa hata kujenga ofisi za chama.kaiba bilioni 8.9 michango ya wabunge.
 
Watanzania tumelala sana mpaka Bunge limegeuzwa soko, badala ya Bunge kujadili mambo yanayowagusa wananchi wao wamegeuza kigenge cha kusifiana na kujadili umbea usio na faida yoyote kwa Watanzania
 
Sio anafanya vizuri, ila ana uchu wa madaraka, na kakuta wananchi wamelala, hivyo anafanya atakacho. Akina Mkapa waliokuwa wanahubiri katiba yetu mwisho wa kiongozi ni miaka 10, wako kimya maana sio wasafi, hivyo hawana la kufanya. Na jamaa kashajua ni waoga, anawasanifu kwa kuwapa ndege tausi!
Ile ya tausi nilishangaa sana. Kana kwamba hao ndege hawajawahi kuwapo hapo ikulu.

Ulr ni mtego wa yeye naye kujimegea mema peke yake. Unaweza kuta hata akipiga hela mgao unakwenda kote huko.
 
Wenye masikio mmemsikia Spika wetu jana na baadhi ya Wabunge kuwa Bunge lijalo tutakuwa wenyewe na tutaibadilisha Katiba na kwamba Katiba sio Msaafu.

Binafsi nawatakia kila la heri ila nawakumbusha kuwa Katiba hiyo ndiyo aliyokuwa Anailinda na Kuitetea Hayati Mwl. Nyerere.
Baba wa taifa lako ni "BERLIN CONFERENCE"
 
Aliyoyaanza na anayoyatekeleza Rais Magufuli hakuna mwenye uthubutu wa kuyaendeleza. Ni vema tukamuongezea muda ili ayakamilishe. Hoja nzuri sana... Kessy ni hazina kwa Taifa hili.

Huo ni upumbavu inamaana magufuri ana akili kuwazidi watanzania zaidi ya millioni 50.

Acheni dharau he's not God, we all deserve that chair.
 
Kama Marekani wamekuja na BLACK LIVES MATTER sisi tutakuja na OPPOSITION LIVES MATTER. Naona wamejisahau na kwenda one step too far. Having said all that bado namkumbuka Da Mange aliposema " this is our only chance"
 
Kuuza nchi kwa mabeberu na mafisadi ni kuacha nchi salama jinga kabisa wewe ,tulikuwa tunaambiwa ni mchanga kumbe ni madini ya zaidi ya $360mil yanatoroshwa na uchafu wa IPTL
kwa hiyo hakuna kiraka mwingine huko lumumba?!Magu akigoma akaamua kustaafu mtaandamana na kumshikia bakora?!aisee!😂😂
 
JPM hajazuia rushwa, alichofanya ni kuminya uhuru wa vyombo vya habari ili visitangaze mambo ya rushwa. Lengo hasa ni kuhadaa umma kuwa hamna rushwa ili akae madarakani atakavyo. Hilo la yeye kutaka kukaa madarakani alianza toka alipoingia madarakani kwa kuwatuma kuna Nkamia. Hii kunajisi chaguzi za nchi hii, ni ili kupata watu watakaomuongezea muda wa kukaa madarakani zaidi ya muda wa sasa wa katiba. Ila mjue mnacheza mchezo bwana hatari ile mbaya. Mchelea mwana kulia ...
Ni kama alivozuwia Corona data na kuonesha kuwa hakuna maambukizi.
 
Watu waliopangwa na jiwe hawa, sasa hivi atajifanya hataki kuongeza muda, ikifika 2025 utaanza kuona anajifanya kubadili mawazo, mtachezeshewa shoo kibao ila anajua anataka kua rais wa milele kama wenzake wa uganda na rwanda tu. Afrika haitoendelea na washenzi design hii
 
Back
Top Bottom