Ally Sykes, Peter Colmore, Albert Rothschild na Oscar Kambona

Ally Sykes, Peter Colmore, Albert Rothschild na Oscar Kambona

Mohamed Said unaweza kutueleza chimbuko la ukoo wa Sykes hapa Tanzania? Kuna mtu kaniambia Sykes chimbuko lao ni Africa Kusini, Walihama kutoka Africa Kusini the late 1800, na kuingia Tanganyika kipindi cha utawala wa Sultani, ili wakubalike na sultani na wazawa wa Mzizima ilibidi wabadili dini na kuwa waislam. je ni kweli?
Laki si pesa,
Sykes Mbuwane alikuwa askari katika jeshi la Wazulu kutoka kijiji cha Kwa Likunyi, Imhambane, Mozambique.

Jeshi hili liliingizwa Tanganyika na Kamanda wa Kijerumani Herman von Wissman kuja kusaidia vita vya Wajerumani dhidi ya Bushiri bin Salim na Mtwa Mkwawa.

Wameingia nchini wakiwa Waislam kwani ndani ya jeshi lile alikuwapo ndugu yake Sykes Mbuwane jina lake Ally Katini.

Ally Katini alikuwa kipofu na hakukaa sana Tanganyika alirudi Mozambique na aliishi hadi mwaka wa 1952 ndipo alipofariki.

Ally Sykes alipozaliwa mwaka wa 1926 baba yake Kleist Sykes Mbuwane alimpa jina la ''Ally,'' ambae ndiye huyu Ally Katini.
 
hapo umenifumbua macho, kwa hiyo ukoo wa Sykes hapa Tanzania umeanzia kwa huyo Askari wa kijerumani, akawazaa Ally na Abduwahid Sykes ambae akamzaa Daisy Sykes, inamaanisha ukoo wa Sykes mzizi wake ni Mozambique, Huko ndio wako ndugu wengi wa ukoo kupita hapa Tanzania, inawezekana ndio maana historia yao ya kupigania uhuru imefutwa kwa sababu hawakuwa wazawa halisi wa Tanganyika, Je, mmeshawatafuta ndugu zenu wengine walioko Msumbiji
 
hapo umenifumbua macho, kwa hiyo ukoo wa Sykes hapa Tanzania umeanzia kwa huyo Askari wa kijerumani, akawazaa Ally na Abduwahid Sykes ambae akamzaa Daisy Sykes, inamaanisha ukoo wa Sykes mzizi wake ni Mozambique, Huko ndio wako ndugu wengi wa ukoo kupita hapa Tanzania, inawezekana ndio maana historia yao ya kupigania uhuru imefutwa kwa sababu hawakuwa wazawa halisi wa Tanganyika, Je, mmeshawatafuta ndugu zenu wengine walioko Msumbiji
Laki...
Sahihisho kidogo.

Sykes Mbuwane ndiye aliyemzaa Kleist Sykes Pangani.

Mama yake Kleist ni Mnyaturu.
Kleist ndiyo akawazaa Abdulbna nduguze.

Mozambique si kwao walikimbia kutoka Shangaan Afrika ya Kusini kukimbia vita vya Shaka.

Kuhusu akina Sykes kwenda kwao Mozambique.

Naingia Maktaba nitakupa kisa kizima In Shaa Allah.

Historia hii yote iliandikwa na Kleist Sykes kabla ya kifo chake mwaka wa 1949 na alielezwa na Chief Mohosh ambae ndiye aliyekuwa kiongozi wa jeshi la Wazulu wakiokuja kupigana Tanganyika.

Mswada huu wa Kleist alimwachia mwanae Abdul na Abdul akampa bint yake Daisy miezi michache kabla ya kifo chake mwaka wa 1968 na Daisy akiwa mwanafunzi University of East Africa akamwonyesha John Iliffe na Iliffe akauchapa katika kitabu mwaka wa 1973.

Mimi ni Mmanyema babu yangu mkuu kaingiapia na Wajerumani kutoka Belgian Congo.

Babu yangu Salum Abdallah kazaliwa Shirati Bomani, Musoma.
 
hapo umenifumbua macho, kwa hiyo ukoo wa Sykes hapa Tanzania umeanzia kwa huyo Askari wa kijerumani, akawazaa Ally na Abduwahid Sykes ambae akamzaa Daisy Sykes, inamaanisha ukoo wa Sykes mzizi wake ni Mozambique, Huko ndio wako ndugu wengi wa ukoo kupita hapa Tanzania, inawezekana ndio maana historia yao ya kupigania uhuru imefutwa kwa sababu hawakuwa wazawa halisi wa Tanganyika, Je, mmeshawatafuta ndugu zenu wengine walioko Msumbiji
Sykes alimzaa Kleist ambaye ndiye baba wa Ally
 
887AAAAAAAAAAAAA.jpg
 
Barbarosa,
Hapana mimi sikupatapo kujuana na Albert Rothschild.

Ukisoma tena kwa utulivu utaona nimeandika kuwa aliyejuana na Rothschild ni Ally Sykes.

Hivi huyu Msanii wa bongo fleva Dully Sykes baba yake ambaye ni marehemu ni Ukoo huu wa Sykes, naomba unijuze kivipi
 
hapo nimekuelewa, vipi kuhusu watoto/wajukuu Wa Abdu, Ally na Daisy Sykes, wako aware na hii historia ya babu/baba zao kuhusu kupigania uhuru? ilikuwaje Daisy akapata elimu kubwa hivyo maana inafahamika enzi za mkoloni shule za mission ili uweze kupata elimu lazima ubadili dini na kuwa mkristo, au na yeye alibadili dini kutoka Aisha akajiita Daisy.
 
hapo nimekuelewa, vipi kuhusu watoto/wajukuu Wa Abdu, Ally na Daisy Sykes, wako aware na hii historia ya babu/baba zao kuhusu kupigania uhuru? ilikuwaje Daisy akapata elimu kubwa hivyo maana inafahamika enzi za mkoloni shule za mission ili uweze kupata elimu lazima ubadili dini na kuwa mkristo, au na yeye alibadili dini kutoka Aisha akajiita Daisy.
Laki...
Daisy katika kumbukumbu ya miaka 50 ya kifo cha baba yake aliandika makala na ilichapwa Raia Mwema kama "series," akaeleza vipi alipata hili jina la "Daisy."

Daisy ni jina la ua lisilokuwa na msimu kuchanua na baba yake akawa kwa mapenzi anamwita bint yake "Daisy."

Hamza Mwapachu na Julius Nyerere walikuwa wakija nyumbani kwao hii ni mwanzoni 1950s wakawa wanamwita Daisy wakilitamka hili jina kwa mbwembwe za lugha ya Kiingereza wakiigiza London "accent."

Ikawa kichekesho fulani na hii ndiyo ikawa sababu ya jina hili kumganda likaua jina lake la Aisha.

Mama yake Bi. Mwamvua akawa anaitwa Mama Daisy hadi anaingia kaburini.

Daisy alianza kusoma Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika School kisha ajapelekwa Aga Khan Girls Primary School akiwa msichana wa kwanza Mwafrika kusoma shule hiyo.

Watoto na wajukuu wanaijua vyema historia yao na jinsi wazee wao walivyoshiriki katika kuunda African Association na TANU na mengi ya maendeleo ya Waafrika Dar es Salaam toka miaka ya 1930s.

Wale waliozaliwa nyakati zetu wakati ule wa 1950s hadi 1960s wakimchukulia Mwalimu kama rafiki ndugu ya baba yao katika familia hasa kutokana na jinsi Bi. Mruguru bint Mussa, mama yake Abdul alivyokuwa akiwahadithia yaliyokuwa yakipitika nyumbani kwao wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika.
 
Daaa mzee MO una kitu adimu ndani yako.
Kwasasa kuna watu wanakubeza lakini hakika wewe ni hazina na lulu ktk histori.
Mimi nataka haya mavitabu yote,Wapi mahali haswa nitapata vitabu hivi kwa uhakika?
 
Daaa mzee MO una kitu adimu ndani yako.
Kwasasa kuna watu wanakubeza lakini hakika wewe ni hazina na lulu ktk histori.
Mimi nataka haya mavitabu yote,Wapi mahali haswa nitapata vitabu hivi kwa uhakika?
Tajiri...
Vitabu hivyo utavipata Ibn Hazm Bookshop Msikiti wa Mtoro na Msikiti wa Manyema.
Bei ni shs:10,000.00.
 
Ndjabu...
1572706044556.png

Kushoto ni Mzee Shebe, John Rupia na Julius Nyerere
Mzee Shebe alikuwa na studio yake Mtaa wa Livingstone na hii studio ilikuwa inatazamana na nyumba ambayo mama yangu mkubwa Bi. Mwanaisha bint Mohamed akikaa,

Hivi ndivyo Mzee Shebe alivyokuja kunipiga picha hiyo hapo chini mwaka wa 1952/52.
Mzee Shebe TANU ilipoanza akaja kuwa mpiga picha wa TANU na wa Mwalimu Nyerere.

1572707156445.png

Mohamed Said 1952/53
Huenda uhusiano wangu na historia ya TANU ulianza hapa na picha hii kuwa aliyenipiga picha mimi mwaka wa 1952/53 akaja kuwa mpiga picha wa TANU na Mwalimu Nyerere.

Jirani na nyunba yetu hii ilikuwa nyumba ya Bi, Mruguru bint Mussa mama yake Abdul Sykes moja ikiwa Mtaa wa New Street ambako sasa kuna jumba la Washirika na nyingine Kirk Street.

Wazee wangu wameiona TANU ikianzishwa na kuhudhuria mikutano ya TANU ya kwanza hapo Mnazi Mmoja na wakiijua historia ya TANU vizuri sana.

Historia hii ndiyo hii mimi naieleza hapa ni bahati mbaya imakughadhibisha kiasi cha kukutoa fahamu unaleta matusi.

Hiyo picha hapo chini ni ya Mwenge wa Uhuru iko Mnazi Mmoja ambako mimi nimepita hapo wakati huo mnara haupo na hizo nyumba unazoziona nyuma ya mnara ziko New Street na moja katika hizo nyumba ni nyumba ya akina Sykes.

Mtaa unaofuatia ni Somalii Street alipokuwa akiishi Zuberi Mtemvu.

Mwalimu Nyerere akizijua vizuri sana nyumba hizi na ni moja katika sehemu ya historia ya TANU na harakati za kudai uhuru wa Tanganyika.

Nyumba zote hizi zilikuwa nyumba za harakati za TANU na Mwalimu akiingia kwa mlango wa mbele na akipenda akatokea mlango wa nyuma na hakuna wa kumuuliza kitu.

Hakuna wa kutufutia historia hii ya wazee wetu.


1572707924930.png

Mnara wa Mwenge wa Uhuru

 
Mohamed Said kuna habari kwamba Mwalimu Nyerere na baba ake Daisy Abdu Sykes waligombana, hata siku alipoenda na Daisy kuonana nae nyumbani kwake Msasan alikuwa na wasi wasi sana kama atakaribishwa vizuri, nini chanzo cha ugomvi wa hawa marafiki wa zamani?
 
Back
Top Bottom