Ally Sykes, Peter Colmore, Albert Rothschild na Oscar Kambona

Ally Sykes, Peter Colmore, Albert Rothschild na Oscar Kambona

Mohamed Said kuna habari kwamba Mwalimu Nyerere na baba ake Daisy Abdu Sykes waligombana, hata siku alipoenda na Daisy kuonana nae nyumbani kwake Msasan alikuwa na wasi wasi sana kama atakaribishwa vizuri, nini chanzo cha ugomvi wa hawa marafiki wa zamani?
Laki...
Hapakuwa na ugomvi baina ya hawa waliopata kuwa marafiki ndugu.

Ukweli wa mambo ni kuwa uhuru ulikuja na changamoto mpya ambayo na nitaeleza ule ukweli kuwa yale mapenzi yaliyokuwapo kati ya Mwalimu Nyerere na wote wale waliompokea mwaka wa 1952 wakawa bega kwa bega hadi uhuru ukapatikana yalitoweka taratibu kuanzia mwaka wa 1963 na kufikia mwaka wa 1968 miezi ya mwishoni kumaliza mwaka pakazuka mgogoro mkubwa.

Waislam chini ya East African Muslim Welfare Society (EAMWS) walikuwa wanajenga Chuo Kikuu ili kuwainua Waislam kutoka udhalili wa kukosa elimu dhulma iliyosababishwa na ukoloni.

Kuna ambao hawakupendezewa na hili na wakawa na hofu nini itakuwa hali ya baadae ya Tanganyika ikiwa Waislam watapata elimu.

Hapa ndipo pakazushwa mgogoro huu ulioishia kwa EAMWS kupigwa marufuku na serikali kuunda BAKWATA.

Baadhi ya masheikh walikamatwa na kuwekwa kizuizini na Mufti Sheikh Hassan bin Ameir akavamiwa nyumbani kwake usiku wa manane na kurudishwa kwao Zanzibar kama muhamiaji asiyetakiwa.

BAKWATA ikaundwa.
Matokeo yake miradi yote ya elimu pamoja na Chuo Kikuu ikafa pamoja na EAMWS.

Vidole vingi vya watu wa Dar es Salaam katika hali ya kufadhaika kwa yale yaliyokuwa yanatokea walikuwa wanamnyooshea kidole Abdul Sykes kama vile kumwambia, ''Wewe ndiye uliyosababisha haya yote.''

Mkasa huu nimeueleza kwa kirefu katika kitabu cha Abdul Sykes.
 
Daaa mzee MO una kitu adimu ndani yako.
Kwasasa kuna watu wanakubeza lakini hakika wewe ni hazina na lulu ktk histori.
Mimi nataka haya mavitabu yote,Wapi mahali haswa nitapata vitabu hivi kwa uhakika?
Tajiri,
Kubeza ni nafuu sasa wanakuja na matusi ya wazi kabisa.

Angalia alichofanya Njabu.

Mwalimu Nyerere huu ni mwaka wa 20 toka afariki na hadi leo anahutubia taifa na tunamsikiliza na hakuna aliyetukana.

Mimi nimesahihisha historia ambayo haikuwa sawa na watu wameipenda na ndiyo sababu ya mimi kuwapo humu ndani nikisomesha.

Yeye anaghadhibishwa na historia hii analeta matusi.
 
Mohamed Said, haki siku zote haiombwi bali inadaiwa, je, haouni kuna haja ya kwenda mahakamani ili kupata haki ya wazee wenu watambulike kama mashujaa wa taifa waliopigania uhuru wa Tanganyika? kama TAA ilitokana na AA , inamaanisha hata CCM chimbuko lake ni AA chama kilichoasisiwa na Kleist Sykes.
 
Mohamed Said, haki siku zote haiombwi bali inadaiwa, je, haouni kuna haja ya kwenda mahakamani ili kupata haki ya wazee wenu watambulike kama mashujaa wa taifa waliopigania uhuru wa Tanganyika? kama TAA ilitokana na AA , inamaanisha hata CCM chimbuko lake ni AA chama kilichoasisiwa na Kleist Sykes.
Laki...
Sijapatapo kusikia kuwa kuna kesi imefunguliwa ili historia ibadilishwe.

Hili ni suala la kisomi na mjadala si suala la watu kusimama mahakamani,

Mimi nilipogundua kuwa historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika ina makosa nilichofanya ni kuandika na kufanya masahihisho.

Matokeo yake ndiyo haya leo wengi waliokuwa hawaijui historia hii sasa wanaifahamu.
 
Mohamed Said kuna habari kwamba Mwalimu Nyerere na baba ake Daisy Abdu Sykes waligombana, hata siku alipoenda na Daisy kuonana nae nyumbani kwake Msasan alikuwa na wasi wasi sana kama atakaribishwa vizuri, nini chanzo cha ugomvi wa hawa marafiki wa zamani?

Sheikh Mohamed hivi wakati Abdulwahid Sykes anafariki Nyerere alikuwa kisha hamia Msasani?
 
Ndjabu...
View attachment 1252075
Kushoto ni Mzee Shebe, John Rupia na Julius Nyerere
Mzee Shebe alikuwa na studio yake Mtaa wa Livingstone na hii studio ilikuwa inatazamana na nyumba ambayo mama yangu mkubwa Bi. Mwanaisha bint Mohamed akikaa,

Hivi ndivyo Mzee Shebe alivyokuja kunipiga picha hiyo hapo chini mwaka wa 1952/52.
Mzee Shebe TANU ilipoanza akaja kuwa mpiga picha wa TANU na wa Mwalimu Nyerere.

View attachment 1252098
Mohamed Said 1952/53
Huenda uhusiano wangu na historia ya TANU ulianza hapa na picha hii kuwa aliyenipiga picha mimi mwaka wa 1952/53 akaja kuwa mpiga picha wa TANU na Mwalimu Nyerere.

Jirani na nyunba yetu hii ilikuwa nyumba ya Bi, Mruguru bint Mussa mama yake Abdul Sykes moja ikiwa Mtaa wa New Street ambako sasa kuna jumba la Washirika na nyingine Kirk Street.

Wazee wangu wameiona TANU ikianzishwa na kuhudhuria mikutano ya TANU ya kwanza hapo Mnazi Mmoja na wakiijua historia ya TANU vizuri sana.

Historia hii ndiyo hii mimi naieleza hapa ni bahati mbaya imakughadhibisha kiasi cha kukutoa fahamu unaleta matusi.

Hiyo picha hapo chini ni ya Mwenge wa Uhuru iko Mnazi Mmoja ambako mimi nimepita hapo wakati huo mnara haupo na hizo nyumba unazoziona nyuma ya mnara ziko New Street na moja katika hizo nyumba ni nyumba ya akina Sykes.

Mtaa unaofuatia ni Somalii Street alipokuwa akiishi Zuberi Mtemvu.

Mwalimu Nyerere akizijua vizuri sana nyumba hizi na ni moja katika sehemu ya historia ya TANU na harakati za kudai uhuru wa Tanganyika.

Nyumba zote hizi zilikuwa nyumba za harakati za TANU na Mwalimu akiingia kwa mlango wa mbele na akipenda akatokea mlango wa nyuma na hakuna wa kumuuliza kitu.

Hakuna wa kutufutia historia hii ya wazee wetu.


View attachment 1252114
Mnara wa Mwenge wa Uhuru

Mzee Shebe akawa mpiga picha wa Serikali. Mwalimu JK alikuwa kiongozi
 
Sichokagi kusoma insha zako Maalim. Nisaidie kujua Ally sykes alikifa lini ?
 
Mzee moh'd naomba kujua katika watu ambao walimpokea mwalimu akitoka shule ya St Francis Kama sjakosea n wangap walibahatika kupata madaraka ya juu nikimaanisha uwazir had ukuu wa wilaya na nyadhfa nyingine kubwa kubwa baada ya kupata uhuru Kama hautojari unaweza kuwataja majina na vyeo vyao au ndio aliwatosa kabisaa

Swali la pili baba yao hao akina Sykes aliyekuja na Jeshi la kiingereza alikuwa na elimu gani wakat huo maana naona Kama Mtu aliyekuwa na upeo Mkubwa Au exposure ya kutembea ilimfanya awe hivyo na je alipotoka huko likunya Mozambique hakuacha Mke na Watoto wengine Au alikuja bado hajaoa?

OMBI Kama hautojari unaweza kuorodhesha vitabu vyako vyote ulivyoandika ili nilienda pale ibn hazm kwa mtoro kariakoo nisihangaike kuuliza nitaje orodha ninunie tu

Shukran sana na Hongera kwa Mada zako tamu zenye kufungua kichwa japo sometimes znaleta taharuki kwa wasiopenda ukweli
 
Mzee moh'd naomba kujua katika watu ambao walimpokea mwalimu akitoka shule ya St Francis Kama sjakosea n wangap walibahatika kupata madaraka ya juu nikimaanisha uwazir had ukuu wa wilaya na nyadhfa nyingine kubwa kubwa baada ya kupata uhuru Kama hautojari unaweza kuwataja majina na vyeo vyao au ndio aliwatosa kabisaa

Swali la pili baba yao hao akina Sykes aliyekuja na Jeshi la kiingereza alikuwa na elimu gani wakat huo maana naona Kama Mtu aliyekuwa na upeo Mkubwa Au exposure ya kutembea ilimfanya awe hivyo na je alipotoka huko likunya Mozambique hakuacha Mke na Watoto wengine Au alikuja bado hajaoa?

OMBI Kama hautojari unaweza kuorodhesha vitabu vyako vyote ulivyoandika ili nilienda pale ibn hazm kwa mtoro kariakoo nisihangaike kuuliza nitaje orodha ninunie tu

Shukran sana na Hongera kwa Mada zako tamu zenye kufungua kichwa japo sometimes znaleta taharuki kwa wasiopenda ukweli
Mzee moh'd naomba kujua katika watu ambao walimpokea mwalimu akitoka shule ya St Francis Kama sjakosea n wangap walibahatika kupata madaraka ya juu nikimaanisha uwazir had ukuu wa wilaya na nyadhfa nyingine kubwa kubwa baada ya kupata uhuru Kama hautojari unaweza kuwataja majina na vyeo vyao au ndio aliwatosa kabisaa

Swali la pili baba yao hao akina Sykes aliyekuja na Jeshi la kiingereza alikuwa na elimu gani wakat huo maana naona Kama Mtu aliyekuwa na upeo Mkubwa Au exposure ya kutembea ilimfanya awe hivyo na je alipotoka huko likunya Mozambique hakuacha Mke na Watoto wengine Au alikuja bado hajaoa?

OMBI Kama hautojari unaweza kuorodhesha vitabu vyako vyote ulivyoandika ili nilienda pale ibn hazm kwa mtoro kariakoo nisihangaike kuuliza nitaje orodha ninunie tu

Shukran sana na Hongera kwa Mada zako tamu zenye kufungua kichwa japo sometimes znaleta taharuki kwa wasiopenda ukwelitano
Peramiho...
Waliompokea Mwalimu Nyerere ni wengi katika watu wa Dar es Salaam.

Walioishinae kwa karibu sana kuliko wengine wote ni watu sita - Abdul Sykes na mkewe Bi, Mwamvua, Ally Sykes na mkewe Bi. Zainab, Dossa Aziz na John Rupia.

Hapa kwanza nakupa tahadhari ili uijue hali za watu hawa.

Abdul Sykes alikuwa Market Master, Soko la Kariakoo na alikuwa na kituo cha mafuta Ilala Boma inaaminika ndiyo Mwafrika pekee katika miaka ile kuwa na biashara kama hiyo Dar es Salaam.

Abdul na mdogo wake Ally walikuwa na nyumba Mitaa ya Stanley, New Street (2), Kipata, Kirk, Ilala, Uhuru na Tandika nje kidogo ya Kariakoo.

Chache katika hizi walijenga katika miaka ya mwanzo ya uhuru na baada ya hapo walijenga au kununua nyumba kadhaa,

Ally Sykes alikuwa na biashara ya ''sales promotion'' kuanzia mwaka wa 1958 na akaingia katika mikondo mingi ya biashara ndani na nje ya nchi.

Dossa Aziz alikuwa na biashara akimiliki magari ya mchanga na kokoto saba na alikuwa yeye na ndugu zake wakimiliki nyumba kadhaa pamoja na nyumba maarufu ya vigae na vioo Mtoni kwa Aziz Ali.

John Rupia alikuwa na biashara kadhaa na alikuwa na gorofa kubwa maarufu mjini Dar es Salaam.

Uwezo huu ndiyo uliowawezesha kufadhili harakati za siasa kuanzia wakati wa TAA hadi wakaunda TANU wazalendo hawa wakiwa ndiyo wafadhili wakuu.

TANU wameianzisha wao na wakaihudumia hadi uhuru ukapatikana mwaka wa 1961.

Wazalendo hawa Nyerere mwenyewe akijua kuwa hakuwa na kazi yoyote ya kuwapa TANU imewakuta wao wakiwa na fedha zao.

Kwa sasa Ibn Hazm wana vitabu vyangu viwili tu watakuonyesha.
 
Back
Top Bottom