Ambao mna marafiki huwa mnawapataje?

Ambao mna marafiki huwa mnawapataje?

Kazini sina marafiki 😂😂 nikifika nafanya kazi zangu zikiisha hata kama ni saa nne naleft, nipo kwenye kikundi cha vicoba kazini lakini sipo interested na hao watu wana umbea uliopitiliza, nipo tu kwasababu nna faida nacho sana
Marafiki wa shuleni?
Chuoni?
Kanisani?
Wazazi wa marafiki wa watoto wako?
Wake wa marafiki wa mumeo?
 
Kuna kitu tunaita "network building" mara nyingi uandaliwa na balozi za nchi za kigeni kama USA, Denmark, Sweden,Japan,Canada, Japan, France & Germany etc japo baadhi unalipia around $30, 40,50 japo nyingine ni bure mara nyingi zinafanyikia Serena, Southern Sun Hotel,Four Season, Kempinsky na Cape Town fish market muda wa jioni baada ya kazi hasa ijumaa/alhamisi zinachukua lisaa 1 mpaka 2 hii utoa fursa ya wageni kupata marafiki na wenyeji kubadilisha mawazo.

Uwa zinaambatana na bites na vinywaji laini ni network building ambazo hamjuani unaenda kwa ajili ya kujuana na watu wapya, ni nzuri na zinakupa exposure kwakuwa hutaki marafiki wasioleweka zinakufaa, ikiwa utafeli/kuogopa kwenda kuna hizi nyingine ila nzuri kwa vijana zaidi hizi balozi za Nordic Countries,UK,France,Swiss,Germany etc huwa zinaandaa cinema kila alhamisi na huzialika balozi nyingine ni free entrance kwa wale wapenda wazungu zinawafaa kwasababu whites wanakuwa wengi mno na wanapenda watu weusi hapo ujanja wako tu wa kupata rafiki au hata mpenzi pia.
Nimehudhuria sana nimejifunza mengi.

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Ni nzuri sana hii ila sikuhizi ulimwengu ulivyo wa
kibepari kila mtu anaangalia anafaidika vipi na wewe. Mnaweza mkawa marafiki ila kama mmoja atahisi kunyonywa inakuwa mbaya.

Wengine wanaenda mbali anakuwa ana filter kama mademu wa kibongo ndio hasa wana tabia hizo...Ukionekana huna hela au mwelekeo wa hela hata salamu anaweza asikujibu. Achilia mbali
kukupa namba ya simu.

Mtu mwenye hii tabia ya ujivuni mwisho wa siku anajikuta kabaki yeye na hela zake maana wenye hela huwa hawabembelezani. 😂
 
Kwakweli najiona mi mwenyewe ni tatizo sio mwepesi wa kuchangama sasa nshaanza kuwa mzee ndio nashtuka....
Usiogope kuchangamana na watu. Huwa kuna mambo mawili 1-Aibu na 2-Ego...

Hilo la kwanza ni rahisi kurekebishika sana, you only need one confident guy ambaye ni mwepesi ku interact na watu ili aweze kukuondoa aibu then unakuwa vizuri kwa interactions.

La pili huwa zito zaidi ila unaweza kulibadilisha kama utafanyiwa special counseling. Inaweza chukua muda ila utaimprove.
 
Nina rafiki mmoja ambaye ninaweza ku-claim kuwa ni rafiki yangu popote pale bila kupepesa macho, urafiki wetu ulianza tukiwa advance miaka ya 2007 yani ile kukesha msuli wote, kushare pocket money, kutoroka skuli wote na uchafu mwingine wote, kisha chuo tukakutana chuo kimoja course moja na kuanza safari zetu za kimaisha mkoa mmoja.

Ni rafiki ambae kuna mpaka baadhi ya mali zake ambazo hataki zijulikane kwake na kwao ila kwangu peke vivyo hivyo mimi, urafiki ambao hata nikiwa mbali na nyumbani anaweza kuwasha gari kumfata mama yangu na kumpeleka hospitali akiwa anaumwa (bila mimi kuchangia gharama zozote), familia zetu ziko linked bila kuambiwa ni lazima uhisi ni za ukoo mmoja .Mungu azidi kutubariki mimi na jamaa yangu.


The first time nakuja kugundua jamaa sio fake ni pale niliposanda kupata hela miaka ya 2014 na wakati huo mke wangu ni mjamzito, nikashitukia tu 4.5M inaingia bila hata kuomba na wala kutegemea.

Na hata mafanikio yote na mifereji yangu ya kuingiza pesa 70% ilianzia kwake from the scratch mpaka leo hii ambapo naweza kusema ninaishi miongoni mwa watu, Nina washikaji wengi ila rafiki ni mmoja na tu tangia niingie kwenye harakati za kujitegemea, ingawa kampani niliyo nayo ni kubwa ila najua ni kwasababu ya vitu na sio urafiki wa dhati.

NB: Kwenye hii dunia marafiki wapo ila sidhani kama huwa wanatafutwa, they just come.
 
Ngoja niandike uhalisia na ukweli wa maisha, even though sijui kwanini watu wengi wanaogopa uhalisia.
Sababu naona mnalazimisha kitu kisicho kuwepo wala kisichowezekana.

At the end utabaki peke yako tu na ukilinganisha marafiki wengi ni wanafiki ni kutumiana kwa faida na huo ndio uhalisia, I have got experience.
Kingine marafiki hawatafutwi bali mtajikuta mnakuwa karibu tu then baadae unaitwa urafiki lakini bado kamwe hamuwezi kuwa pamoja every moment.

Marafiki wa kweli ni familia yako tu namaanisha watoto na mke/mume. Lakini zaidi ya hapo watu baki watakuwa ziada tu kwenye maisha yako sababu siku zote watakuja na kuondoka lakini familia yako mtakuwa pamoja milele hata kama wengine wataenda mbali lakini siku zote mtabaki pamoja. trust me.
Familia yako hao ndio mtakao lia, kucheka na kufurahi wote pamoja na ndio mtakaozikana na watakao kuzika wewe.

Utapata mke/mume then mtazaa watoto wenu wanne au nane, mtawalea na kuwakuza kwa maadli mema mkiwa pamoja, mtakula na kunywa pamoja, mtacheka na kufurahi pamoja, mtaenda beach, Cinema, Vacations milimani, misituni na mijini.
Mtakwenda Shoppings, hotelini pamoja. Na wao watoto watakuwa wakubwa na kuwaletea wajukuu huku nyie mkianza kuzeeka lakini it doesn't matter sababu mtakuwa pamoja na hautokuwa alone na cycle itazidi kuongezeka huku wajukuu wakiwachangamsha na kuwakumbusha dhumuni na maana ya maisha. kutoka wawili wapendanao mpaka familia ya watu 16 au 20. kundi kubwa la watu ambalo ni your own creation imagine that? ni proud na furaha kiasi gani utajisikia just kutambua hilo?

Mtakutana na kupika na kula na kunywa pamoja huku mkifurahi kila siku hata kama haitokuwa kila siku it doesn't matter sababu siku zote watakuwepo pale utakapopata shida au utakapowahitaji.
Na siku ukifa hao ndio watakaokuja kukuzika na kukulilia na kukukumbuka milele na jina lako litaishi ndani yao.

Lakini kusema watu baki muwe wa kufa na kuzikana hiyo itabaki kuwa theory tu na ni kitu kisichowezekana kabisa.
Familia yako ndio marafiki zako wa kufa na kuzikana, huo ni Uhalisia. that's all.

Na ndio maana siwaelewi watu wanaosema Usioe au usizae na usiwe na mwanamke mmoja mimi nawaona bado watoto na akili zao hazijakua na kukomaa kiasi cha kuona uhalisia wa maisha. that's why nataka nioe mapema before it's too late, my future wife is a lucky woman I admit sababu dunia imejaa wahuni wasaka vitamu bila future wala kujua wanachokitaka au wanapokwenda bali wanaangalia sasa hivi tu.

Umesema unaanza kuzeeka then I'm really sorry kama ninachokifikiria ni kweli na wala sijamaanisha wala kukusudia kumuumiza yoyote.
Wale wanaoendelea kula tunda kimasihara na kula ujana sijui kuenjoy life na kula bata good luck, siku mtakuja kusoma hii comment na kukumbuka it's too late kumbe Uncle butcher alikuwa sahihi.
 
Njia ya kupata marafiki saidia vitu au kitu kwa kadri unavyoweza sio usaidie hela tu hata ushauri...

Tatua changamoto zinawakabili jamii yako ya karibu kwa namna utakavyojaaliwa...

ukiwa mtu wa kutoa bila kujali unapata nini utapata marafiki wengi wabaya na wazuri, unachotakiwa kufanya ni hv,

Wale wazuri wachache unawaweka karibu, wale marafiki wabaya unawaweka mbali na ww bila ya kuwaambia..

Ukiendelea na hyo cycle utajikuta unapata marafiki wengi ndani ya mfupi kaz yako itakuwa moja kuwapunguza na kuwaongeza kwa kadri ya matarajio...

NB: Principle ya urafiki ni kutoa(GIVING) without expecting anything in return, ukifanikiwa utaanza kupokea kutoka kwao.

UCHOYO NA URAFIKI HAVIKAI PAMOJA.

Sent from my Infinix X609 using JamiiForums mobile app
 
Good morning jf....
Tusio na marafiki tukutane hapa😔

Kuna hili swala nimekua nikijiuliza hivi karibuni, baada ya kuona sasa uzee umeanza kupiga hodi. Najiona umri umetangulia mbele halafu maisha ni kama nayaacha nyuma, ni kama naishi tofauti na umri wangu. Nimesogea umri wa kuozesha, kuondokewa na wapendwa (waliozeeka) na kukutana na mambo mengi ambayo nadhani yanahitaji watu....ila bahati mbaya sasa hao watu ndio sina.

Natamani kuwa na marafiki kuwa na watu, watu wa faida, watu ambao wanaweza kushare ramani za maisha, watu ambao tunaweza kupanga safari kwenda vituo vya wahitaji tukawape misaada, watu ambao nikihitaji kumwagilia moyo najua wapo, watu ambao nikikwama najua watakuwepo, kina mama wenzangu huwa wana vyama umuhimu wa vyama naujua ila mi hata chama sijawahi kuwa nacho....naishi mwenyewe mwenyewe tu hadi nawaza si nitakosa wa kunizika mie mwisho nizikwe na manispaa.

Wenye marafiki mnawapataje???
Mama malizia muda wako tu hapa duniani umeshachelewa.

Inaonekana ulikuwa na nyodo sana ukajiona huhitaji kuwa na watu kwa sababu kila kitu una uwezo nacho.

Hii ni tabia ya wagu wengi vijana wenye pesa. Huona wale wa chini hawana msaada kwao.
 
Back
Top Bottom