Ambao mna marafiki huwa mnawapataje?

Ambao mna marafiki huwa mnawapataje?

Marafiki hawatafutwi hivyo wewe ukitaka kuamini rafiki siku upate tatizo kama atakusaidia.Waswahili wanasema Ndege wafananao ndio huruka pamoja"Marafiki wengine matatizo yao tu ila unapokua na shida hakusaidii hivyo kuwa makini unaweza sema rafiki kumbe adui anakuombea uporomoke kiuchumi.
 
Good morning jf....
Tusio na marafiki tukutane hapa😔

Kuna hili swala nimekua nikijiuliza hivi karibuni, baada ya kuona sasa uzee umeanza kupiga hodi. Najiona umri umetangulia mbele halafu maisha ni kama nayaacha nyuma, ni kama naishi tofauti na umri wangu. Nimesogea umri wa kuozesha, kuondokewa na wapendwa (waliozeeka) na kukutana na mambo mengi ambayo nadhani yanahitaji watu....ila bahati mbaya sasa hao watu ndio sina.

Natamani kuwa na marafiki kuwa na watu, watu wa faida, naishi mwenyewe mwenyewe tu hadi nawaza si nitakosa wa kunizika mie mwisho nizikwe na manispaa.

Wenye marafiki mnawapataje???
Tumia njia kama hizi

Mkuu kama wewe ni mkristu jitahidi uwe unasali jumuiya na kwenda church huko utafahamiana na baadhi ya majirani zako mnaosali pamoja.

Pia jitahidi uwe unahudhuria shughuli za kijamii za mtaani kwako kama misiba au hata sherehe za harusi,kipaimara,kumunio zinazotokea hapo mtaani unapoishi.lazima tu utafahamiana na majirani zako.

Pia siku ukiwa off jitahidi utumie hata mda mchache kujimix mtaani,kama kufanya manunuzi kwenye maduka ya mtaani unapoishi, kaa kwenye vigrocery vya mtaani unywe hata Maji Kama sio mtumiaji wa alcoholic drinks, jitahidi uwe unakaa hata kwenye vijiwe vya mtaani sikumojamoja na pia uwe unasalimia watu wa mtaani hata Kama unagari na pia uwe unawapa lift ukikutana nao.

Kibongobongo ni hatari sana unapoishi bila kufahamu majirani zako.
Jirekebishe haraka

Huyu jirani yangu upande wa kushoto yeye hajaweka fensi na yupo muda kidogo hapa mtaani, kama miaka minne mitano ivi. Juzijuzi nilienda kumsalimia maana bado ni kijana kijana tukawa tunabadilishana mawazo.

Aisee nilishangaa jinsi anavyofahamiana na kila mtu, watu wakipita (kuna barabara kwa mbele, kama mita 20 - 30 kutoka ilipo nyumba) lakini wanasalimia, wanapunga mikono nk. Wenye magari wanapiga honi, wanashusha vioo wanapunga mikono... kwakweli nilisikia wivu sana.

Hata mimi nilikumbwa na hali kama yako kwa kipindi cha miezi 6. Nilipoanza kusali Jumuiya na siku moja wakaja kusali kwangu yaani nilipata marafiki wengi mpaka wakaniunganisha kwenye group lao la whatsup

Utashangaa jirani na mbali zaidi wote wanakufahamu wanakuangalia tu. Nikupe incident tatu zimetokea nikajua kumbe watu wanakuchora tu
1.niliharibikiwa na gari mbali kidogo na home nikachukua bajaj kurudi home kutafuta alternative, yule wa bajaj akaanza kukata mitaa nikamuuliza wewe unajua unapoenda? akasema blaza si unakaa pale pako hivi na hivi...nikaishiwa pozi
2.Nimeenda dukani hardware kununua vitu sasa nataka mtu apeleke nyumbani mimi naenda kazini, kaitwa bodaboda akapewa nampa maelekezo ananiambia aah blaza si kwenye kona pale hivi na hivi!
3.wengine nimekuta masela wanaziba mashimo barabarani wakaniwahi blaza wa pale hivi na hivi tutoe leo pozi likaisha
Yaani watu wote wanakufahamu unapokaa,unaendesha gari gani etc ila unapita huongei na mtu wanakuangalia tu. siku moja moja shusha kioo wasalimie watu mtaani
 
Good morning jf....
Tusio na marafiki tukutane hapa😔

Kuna hili swala nimekua nikijiuliza hivi karibuni, baada ya kuona sasa uzee umeanza kupiga hodi. Najiona umri umetangulia mbele halafu maisha ni kama nayaacha nyuma, ni kama naishi tofauti na umri wangu. Nimesogea umri wa kuozesha, kuondokewa na wapendwa (waliozeeka) na kukutana na mambo mengi ambayo nadhani yanahitaji watu....ila bahati mbaya sasa hao watu ndio sina.

Natamani kuwa na marafiki kuwa na watu, watu wa faida, watu ambao wanaweza kushare ramani za maisha, watu ambao tunaweza kupanga safari kwenda vituo vya wahitaji tukawape misaada, watu ambao nikihitaji kumwagilia moyo najua wapo, watu ambao nikikwama najua watakuwepo, kina mama wenzangu huwa wana vyama umuhimu wa vyama naujua ila mi hata chama sijawahi kuwa nacho....naishi mwenyewe mwenyewe tu hadi nawaza si nitakosa wa kunizika mie mwisho nizikwe na manispaa.

Wenye marafiki mnawapataje???
 
Wengi tunaowaona sio kwamba ni marafiki bali watu waliozoeana,na mazoea huja kupitia kusoma pamoja,kufanya kazi pamoja au kwenye mazingira yanayofanana na hayo!

Kupata rafiki ambae atakuthamini na kuwa mwaminifu kwako sio kazi rahisi yani hapo na maombi yahusike,bila hivyo it is better hapo ulivyo alone kuliko upate watu wataolazimisha downfall yako kilazima kabla ya muda!

Cha mwisho kama uko desperate sana jaribu kwenye vikoba huko utapata watu na ikitokea una shida basi hao wataambatana nawe,kama uko dar wafatilie buta vikoba hawa wana branches kila kona ya dar!
 
Good morning jf....
Tusio na marafiki tukutane hapa😔

Kuna hili swala nimekua nikijiuliza hivi karibuni, baada ya kuona sasa uzee umeanza kupiga hodi. Najiona umri umetangulia mbele halafu maisha ni kama nayaacha nyuma, ni kama naishi tofauti na umri wangu. Nimesogea umri wa kuozesha, kuondokewa na wapendwa (waliozeeka) na kukutana na mambo mengi ambayo nadhani yanahitaji watu....ila bahati mbaya sasa hao watu ndio sina.

Natamani kuwa na marafiki kuwa na watu, watu wa faida, watu ambao wanaweza kushare ramani za maisha, watu ambao tunaweza kupanga safari kwenda vituo vya wahitaji tukawape misaada, watu ambao nikihitaji kumwagilia moyo najua wapo, watu ambao nikikwama najua watakuwepo, kina mama wenzangu huwa wana vyama umuhimu wa vyama naujua ila mi hata chama sijawahi kuwa nacho....naishi mwenyewe mwenyewe tu hadi nawaza si nitakosa wa kunizika mie mwisho nizikwe na manispaa.

Wenye marafiki mnawapataje???
Kwa nini usitumie jf kama chanzo cha kupata rafiki? Angalau umeshasema aina ya rafiki unayetaka (maandishi meusi). Unachotakiwa kusema anayekidhi hivyo vigezo tuwasiliane na utapata wengi tu. Sijui vikoba etc unapoteza muda tu. Watu wameoana kupitia jf, sembuse urafiki?
 
Good morning jf....
Tusio na marafiki tukutane hapa😔

Kuna hili swala nimekua nikijiuliza hivi karibuni, baada ya kuona sasa uzee umeanza kupiga hodi. Najiona umri umetangulia mbele halafu maisha ni kama nayaacha nyuma, ni kama naishi tofauti na umri wangu. Nimesogea umri wa kuozesha, kuondokewa na wapendwa (waliozeeka) na kukutana na mambo mengi ambayo nadhani yanahitaji watu....ila bahati mbaya sasa hao watu ndio sina.

Natamani kuwa na marafiki kuwa na watu, watu wa faida, watu ambao wanaweza kushare ramani za maisha, watu ambao tunaweza kupanga safari kwenda vituo vya wahitaji tukawape misaada, watu ambao nikihitaji kumwagilia moyo najua wapo, watu ambao nikikwama najua watakuwepo, kina mama wenzangu huwa wana vyama umuhimu wa vyama naujua ila mi hata chama sijawahi kuwa nacho....naishi mwenyewe mwenyewe tu hadi nawaza si nitakosa wa kunizika mie mwisho nizikwe na manispaa.

Wenye marafiki mnawapataje???
Evelyn Salt kuna ujumbe wako PM naomba ufungue
 
Back
Top Bottom