Amempa mimba mwanafunzi, akamnunulia dawa za kutoa-hakuzitumia. Sasa anaomba ushauri!

Amempa mimba mwanafunzi, akamnunulia dawa za kutoa-hakuzitumia. Sasa anaomba ushauri!

Ni kijana ambaye nilikutana naye mahali fulani wakati nahitaji huduma fulani.
Nilipofika nilimkuta anaongea na simu, kwa kuwa nilikuwa sina haraka nikamwambia amalize kuongea atanihudumia wakati huo mi nimepumzika kidogo kwenye benchi.

Sikuwa najisikia vizuri sana kutokana na vurugu mbalimbali za kimaisha.
Kupanda kwa gharama za bidhaa, kila unachouliza kiko juu, gharama za usafiri nk. Kiukweli nilikuwa nimechoka.

Alipomaliza kuongea na simu, akaniuliza, "vipi unaumwa?" Nikamwambia hapana siumwi, ni stress tu za maisha.
Akaniuliza "wewe una stress kuliko zangu?" Nikamjibu mbona wewe bado kijana mdogo, stress unapata wapi?

Ndipo aliponisimulia kisa cha huyo binti ambaye ndiye alikuwa anaongea naye kwenye simu. Akasema alikuwa na mahusiano naye na akapata ujauzito, ila kwa kuwa bado ni mwanafunzi akamnunulia dawa za kutoa. Lakini binti huyo inaonesha hakuzitumia. Badala yake akaamua kwenda kumshtaki polisi. Alikaa polisi zaidi ya siku 10.

Kijana huyu aliendelea kusema kwamba, binti huyo hata hivyo 'hajatulia' anahisi ana wanaume wengi kutokana na tabia yake. Na kwamba kuna siku alimtumia ujumbe wenye jina la mtu mwingine kwamba anampenda huyo mtu. (Yaani kwa mfano yeye anaitwa john, basi akaandika juma nakupenda...)🤔😲

Akadai kwamba hiyo ni sababu ya kuacha kuwasiliana naye na kumtaka sasa atoe hiyo mimba.
Sasa akaomba ushauri afanye nini?
Maana tayari ameshalipa faini nyingi huko polisi nk. Na hana uhakika kama hiyo mimba ni yake kweli!

Ungekuwa ni wewe mtu kama huyu ungemshauri nini?
ushauri wana ajiandae kimwili na kiakiri maana nasikia nyapala uko jela zipu ya suruali yake imealibika na polisi nchi nzima wamezunguka kumtafutia jamaa zipu mpya wamekosa
 
Ni kijana ambaye nilikutana naye mahali fulani wakati nahitaji huduma fulani.
Nilipofika nilimkuta anaongea na simu, kwa kuwa nilikuwa sina haraka nikamwambia amalize kuongea atanihudumia wakati huo mi nimepumzika kidogo kwenye benchi.

Sikuwa najisikia vizuri sana kutokana na vurugu mbalimbali za kimaisha.
Kupanda kwa gharama za bidhaa, kila unachouliza kiko juu, gharama za usafiri nk. Kiukweli nilikuwa nimechoka.

Alipomaliza kuongea na simu, akaniuliza, "vipi unaumwa?" Nikamwambia hapana siumwi, ni stress tu za maisha.
Akaniuliza "wewe una stress kuliko zangu?" Nikamjibu mbona wewe bado kijana mdogo, stress unapata wapi?

Ndipo aliponisimulia kisa cha huyo binti ambaye ndiye alikuwa anaongea naye kwenye simu. Akasema alikuwa na mahusiano naye na akapata ujauzito, ila kwa kuwa bado ni mwanafunzi akamnunulia dawa za kutoa. Lakini binti huyo inaonesha hakuzitumia. Badala yake akaamua kwenda kumshtaki polisi. Alikaa polisi zaidi ya siku 10.

Kijana huyu aliendelea kusema kwamba, binti huyo hata hivyo 'hajatulia' anahisi ana wanaume wengi kutokana na tabia yake. Na kwamba kuna siku alimtumia ujumbe wenye jina la mtu mwingine kwamba anampenda huyo mtu. (Yaani kwa mfano yeye anaitwa john, basi akaandika juma nakupenda...)🤔😲

Akadai kwamba hiyo ni sababu ya kuacha kuwasiliana naye na kumtaka sasa atoe hiyo mimba.
Sasa akaomba ushauri afanye nini?
Maana tayari ameshalipa faini nyingi huko polisi nk. Na hana uhakika kama hiyo mimba ni yake kweli!

Ungekuwa ni wewe mtu kama huyu ungemshauri nini?
Ajipeleke tu police
 
Back
Top Bottom