Amenichumbia lakini hataki Ndoa

Amenichumbia lakini hataki Ndoa

Habari za asubuhi wakuu wote wa JF na hongereni kwa shughuli mbalimbali za kujenga taifa.

Kilichonileta kwenu asubuhi hii ni kunisaidia mawazo ya hili nalopitia kwa sasa, mimi na mwenza wangu tuna miaka mitatu sasa tunaishi pamoja na ni mwaka mmoja wa kuchumbiwa.

Kama mjuavyo, desturi zetu za Kiafrika baada ya mahari mnaulizwa tarehe ya Ndoa ndivyo ilivyokuwa na kwetu pia ila mwenzangu aliomba ajipange sababu hakuwa vizuri kwa kipindi hicho hivyo wazazi walimkubalia.

Sasa napata maswali mengi kutoka kwa wazazi na ndugu wakiniuliza ndoa lini mpaka nakosa majibu sababu nikimuuliza mwenzangu ananiambia nina haraka gani nisubiri.

Kilichonifanya nije kwenu ni kuomba ushauri je niko sahihi kuendelea kutumikia majukumu yangu ya ndoa kwa mgongo wa kuchumbiwa au nimechutama choo cha kiume?
Ukilipiwa mahari au barua ya uchumba tayari ushaolewa, kulipiwa mahali ni sawa na kuolewa kimila, ukitaka funga ndoa ya serikali nayo ina makaratasi, ya kanisani ina makaratasi na inagharama, kama hana utayari wa harusi ndio imetoka hio ni ndoa kama unaamini kwenye harusi zaidi achia ngazi mapema.
 
Habari za asubuhi wakuu wote wa JF na hongereni kwa shughuli mbalimbali za kujenga taifa.

Kilichonileta kwenu asubuhi hii ni kunisaidia mawazo ya hili nalopitia kwa sasa, mimi na mwenza wangu tuna miaka mitatu sasa tunaishi pamoja na ni mwaka mmoja wa kuchumbiwa.

Kama mjuavyo, desturi zetu za Kiafrika baada ya mahari mnaulizwa tarehe ya Ndoa ndivyo ilivyokuwa na kwetu pia ila mwenzangu aliomba ajipange sababu hakuwa vizuri kwa kipindi hicho hivyo wazazi walimkubalia.

Sasa napata maswali mengi kutoka kwa wazazi na ndugu wakiniuliza ndoa lini mpaka nakosa majibu sababu nikimuuliza mwenzangu ananiambia nina haraka gani nisubiri.

Kilichonifanya nije kwenu ni kuomba ushauri je niko sahihi kuendelea kutumikia majukumu yangu ya ndoa kwa mgongo wa kuchumbiwa au nimechutama choo cha kiume?

Yumo humu pia ukawa unauliza humu na maelezo kiuwazi hivyo!!!!! Sasa na mtoto anakuja, tulia na usali.
 
Ushauri mzuri ni huu:- Ukweli ni kuwa tayali we ni mke wa mtu (mahali ndo kiashirio) hivyo kaa tulia
Serikali inaitambua aina ya ndoa yako ila nakushaur achana na mambo ya ndoa mwombe mwemde boman mkafunge nyie wawili na mashahidi ili upate cheti
Kwa sababu hapo ulipo akifa serikali inakutambua kama mke halali ila kkitokea sahiz akaenda kwa siri kufunga ndoa(kupewa cheti na mtu mwimgine tofaut na wewe) hapo ndo kitaumana na hutokuwa na chako ila kama hatapata cheti na mtu mwingine basi we ni halali
Bomani kwani hawana dini hao?! Makanisani na misikiti wanafungisha ndoa za kimya kimya bila kelele tena siku za kazi katikati ya wiki,ni wewe tu na mwenzako kujiandaa kwenda na mashahidi wenu. Ndoa chap mnarudi kuendelea na maisha ya ndoa.
 
We sasa unataka mwenzako aje jutia. Badala ya kushauri azungumze na mwenzake vizuri unaanza story za yeye kurudi kwao.

Wanawake wa siku hizi sijui mpoje yaani wepesi sana kufanya maamuzi ambayo ukija kaa chini baadae unakuja kujiona ulitumia akili za kisichana kwenye mambo ya kiutuuzima. Unajuaje labda jamaa anajipanga kimya kimya kwasababu hali yake sio nzuri kifedha?!

Sometimes Wanaume tunakuwa kimya ni kwasababu ya aina ya wanawake tulio nao. Unakuta sio mwanamke ambaye ni mshauri mzuri na pia sio muelewa hata unaposema uketi nae chini mzungumze kiutuuzima anakuwa si mtu ambaye ni co-operative, ni mtu wa kulaumu na kukusomea list ya mahitaji au changamoto. Ila sio mwanamke ambaye atakuwa partner kiuchumi.
Mtu kama huyu unakuwa unamuona kama mwanao au mtoto mdogo kiasi kwamba akikwambia jambo zito kama ndoa ambalo linahusiana na fedha tena zaidi ya milioni 10 unabakia tu kumwambia angojee maana hata ukimuelekeza si mtu ataekupa positive contribution ya mawazo wala idea au hata kujiongeza atabakia kutumbua macho na kukwambia we ndo mwanaume.
Ajutie kwa kipi labla nimeandika kwenu umefukuzwa we umeelewa vipi naona unanishutumu yaani bibie kurudi kwao ata jutia inashangaza hajaolewa why ajutie kurudi kwao, yes arudi kwao ili kama Mwanaume kama ana nia kweli amuoe sio anafaidi tunda kufata utamaduni na mila hataki.
 
Wasiwasi Ndiyo Akili Japo Ukweli Sisi Wagalatia Mambo Ni Mengi Sana Ila Sijajua Upande Dini Ya Mudi Mambo Ni Rahisi
Chukua Hatua Lazima Lipo Jambo Tu
Napenda Baada Ya Ushauri Jitahidi Uje Baadaye Na Mrejesho Mzuri Sana
Kuna ndoa za vodafaster , inafungwa hata katikati ya wiki yaani zoezi ni la nusu saa tu kama ndoa ya mkeka.

Na kuiprocess fasta na masharti yake ni nafuu. Ndoa inafungwa hata na watu 10 tu hapo around no need ya mbwembwe.

Mambo mengi sana ndugu zangu why tuumize kichwa. Shida hawa warembo wetu wanapenda sana attention za mitandaoni ili awaringishie wenzake na kuonyeshana nani zaidi.

Wanaume hatuna mambo mengi sana tunataka ndoa sio harusi.

Sasa kama kwenye hiki kisa, bi dada anataka sherehe ya ndoa jamaa ameshapata ndoa ndo anaishi.
 
Kuna ndoa za vodafaster , inafungwa hata katikati ya wiki yaani zoezi ni la nusu saa tu kama ndoa ya mkeka.

Na kuiprocess fasta na masharti yake ni nafuu. Ndoa inafungwa hata na watu 10 tu hapo around no need ya mbwembwe.

Mambo mengi sana ndugu zangu why tuumize kichwa. Shida hawa warembo wetu wanapenda sana attention za mitandaoni ili awaringishie wenzake na kuonyeshana nani zaidi.

Wanaume hatuna mambo mengi sana tunataka ndoa sio harusi.

Sasa kama kwenye hiki kisa, bi dada anataka sherehe ya ndoa jamaa ameshapata ndoa ndo anaishi.
Nakazia
 
Aiseeeee..... Shikamooo wanaume jamani.

Maana makwazo hayana budi kujaaaa, ila ole wake yeye akwazayeeee.
 
Ushauri wangu,beba nguo zako nenda kwake km unaenda kumtembelea vile halafu unamaliza huko miezi kadhaa hadi unabeba mimba,ndo inakuwa tiketi.Sometime sisi Wanaume huwa tunakuwa wazito sana kuthubutu hadi tulazimishwe au tubembelezwe.
 
Ushauri wangu,beba nguo zako nenda kwake km unaenda kumtembelea vile halafu unamaliza huko miezi kadhaa hadi unabeba mimba,ndo inakuwa tiketi.Sometime sisi Wanaume huwa tunakuwa wazito sana kuthubutu hadi tulazimishwe au tubembelezwe.
Ndio atakua amesovu tatizo???!! Ameshasema kwasasa tayari ni mjamzito
 
Ndio atakua amesovu tatizo???!! Ameshasema kwasasa tayari ni mjamzito
Basi amefanya kosa kubeba mimba akiwa bado yupo nyumbani kwao, Ilitakiwa ang'ang'ane kubaki kwa huyo jamaa.Sasa Naona usingle mother unamnyemelea.
 
Kuna ndoa za vodafaster , inafungwa hata katikati ya wiki yaani zoezi ni la nusu saa tu kama ndoa ya mkeka.

Na kuiprocess fasta na masharti yake ni nafuu. Ndoa inafungwa hata na watu 10 tu hapo around no need ya mbwembwe.

Mambo mengi sana ndugu zangu why tuumize kichwa. Shida hawa warembo wetu wanapenda sana attention za mitandaoni ili awaringishie wenzake na kuonyeshana nani zaidi.

Wanaume hatuna mambo mengi sana tunataka ndoa sio harusi.

Sasa kama kwenye hiki kisa, bi dada anataka sherehe ya ndoa jamaa ameshapata ndoa ndo anaishi.
📌📌📌👍👍
 
Mahali ikipokelewa tayari kwa desturi wewe umeolewa.
 
Hiyo sio ndoa, ila sheria ina presume hivyo. Hata mkiishi miaka mia kama hakuna ndoa inayotambulika, yaani ya kidini, kiserikali mtu hawezi dai talaka maana hamna ndoa hapo
mkuu naomba kufahamu ,waliooana wakitalakiana kuna mambo ya kugawana mali walizochuma maana hiyo ndoa Sheria inatambua .

Pia kuishi pamoja kwa hiyo miaka 3 inatambulika kama ndoa Ila hamna makaratasi means kuachana haihitaji talaka ,Sasa kugawana mali hapo inakuwaje?
 
mkuu naomba kufahamu ,waliooana wakitalakiana kuna mambo ya kugawana mali walizochuma maana hiyo ndoa Sheria inatambua .

Pia kuishi pamoja kwa hiyo miaka 3 inatambulika kama ndoa Ila hamna makaratasi means kuachana haihitaji talaka ,Sasa kugawana mali hapo inakuwaje?

Mkuu tofauti iliyopo kati ya wana ndoa na watu walioishi pamoja kwa zaidi ya miaka miwili pamoja kwa kupika na kupakua pasi na ndoa ni kwamba mahusiano ya wanandoa wakishindwana wanaweza kwenda mahakamani kuomba wavunje ndoa (divorce) ama waachane kwa muda wakiendelea kusuruhisha (separation), hawa wa aina ya pili hawana haki hiyo ya kuomba kutalikiana ama kutengana kwa muda sababu in fact kati yao hapakua na ndoa.

Faida yake ni nini sasa hii presumption of marriage? Ni kulinda tu haki za watu waliokua katika uhusiano huo, mfano kama walipata watoto katika hayo mahusiano na wameshindwana itabidi mwanamke aombe mahakama iamuru mwanamme awe analipa gharama za matunzo ya watoto na yeye mwenyewe apewe matunzo lakini pia kama kuna mali walichuma pamoja pindi wakiwa katika huo uhusiano inabidi wazigawane.

In short Yale yote yanayotokea kwa wana ndoa walioona ki halali huku pia yatatokea isipokuwa tu hauwezi kwenda kuomba talaka wala kutengana.
 
Back
Top Bottom