Amiri Jeshi mkuu anaegopa wauza unga na wezi wa EPA ataweza kutuongoza vitani?

Amiri Jeshi mkuu anaegopa wauza unga na wezi wa EPA ataweza kutuongoza vitani?

Hamjaziona kesi za epa na watu kufungwa?

Hamuoni watu wa unga wanavyokamatwa kila siku?

Chuki zenu ni za kibinafsi na roho zanu zilivyombaya kila mnapoona mafanikio ya Kikwete nyie ndio mnazidi uhasidi. Mtaungulika sana, Kikwete ndio Rais na Mohamed Gharib Bilal ndio makamu wake.

Wewe upimwe akili sio mzima au ndio mama wa tanu
 
Kusema kweli kuna walakini kwa Rais wetu, mpaka Kagame kamtukana hivyo ujue kaona udhaifu. Na hili si jambo dogo, embu fikiria Rais wetu ana rasilmali ardhi, watu zaidi ya 45ml, kodi inayokusanywa kubwa lakini anashindwa kucheza na hizo rasilmali, anakwenda kuchezewa na mtu ana raslimali kidogo sana! Kagame aliwahi sema mimi nikipewa bandari tu ya Dar naweza kulisha TZ, lakini yeye hata ile kumpongeza Mwakyembe hamna! Magufuli,hamna!. Mkapa alilipa deni lote huku akijenga barabara yeye kalirudisha 20trn sa sijui ndo zinajenga barabara! Anasikitisha sana!nchi haina hata shughuli za uzalishaji zinazoeleweka wala mpango wa kuwa nazo! utapigana vita na mauzo ya mazao tena ya wakulima maskini! na hana wasiwasi anacheka tu!
 
Faiza Foxy zungumza kidogo basi juu ya madawa ya kulevya?
 
Last edited by a moderator:
Hivi tujiulize,Raisi asieweza hata kuwakamata na kuhakikisha wauza madawa ya kulevya na wezi wa EPA ndani ya nchi ataweza kweli kuongoza majeshi yetu katika vita dhidi ya taifa lingine?

Wabongo tusithubutu kuingia vitani chini ya Raisi wa sasa.Tutaambulia aibu na kipigo,Amiri jeshi mkuu wa sasa sidhani kama anaweza hata kuhamasisha majeshi yetu na siamini hata wanajeshi wetu wana imani na nae.

Mgogoro baina yetu na Malawi na sasa Rwanda ni bora tu ukaishia kuwa ni wa vita ya maneno tu.

Nina mashaka kama kweli Amiri Jeshi Mkuu wa sasa anaweza hata kuhutubia wanajeshi na kuwapa ujasiri.Ukishaonekana ni dhaifu ndani ya nchi yako hata wanajeshi wanapoteza imani na wewe na kujiona hawana kiongozi anaewafaa.

Tafakari ukiwa "realistic" na sio kishabiki uone utapata jibu gani.

Hakika Unahoja ya kuwaelimisha na kuwaasa Watanzania wenzako??!! Hili halina ubisha hata kidogo, mada yako iko wazi na inasomeka vema sana.

Binafsi naona umejichanganya na huna hakika haswa ulitaka tukuuelewe vipi! Kumdhoofisha Amiri Jeshi? Watanzania? Au Wanajeshi wetu!!?

Kwanza sio vizuri wala sio heshima Kuchangaya siasa za Ndani na nje ya Nchi!

"Wabongo tusithubutu kuingia vitani chini ya Raisi wa sasa" .. Tamshi kama hili linatia shaka kama kweli unamaanisha unachojaribu kueleza. Tamshi lako linaashiria kuwa Kuingia vitani ni jambo la kuchagua kama vile kuamua kunua mkate au koti. Yaani wakati wowote wabongo wanaweza kuchagua lini na wapi kuingia vitani! Hii si kweli hata kidogo. Vita inaweza kutokea saa yeyote baada au kabla ya uchaguzi uliopangwa.

Kama vita ikitokea leo huwezi kuiarisha hadi umpate Rais wako unayemtarajia!-Unatambua fika kuwa tunakuwa na Rais mmoja kwa kila wakati na huyo ndie atakabiliana na kila Tukio linalomuhusu. Kwa Sasa Ni Mheshimiwa J M Kikwete Amiri Jeshi mkuu wa serekali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mueleze Kagame au -Bi-Joyce-kuwa Tanzania ni Taifa kamili linalojiheshimu na lisiloyumbishwa. Waeelze kuwa Kila Rais anamapungufu yake na Uimara wake. Wape salaam kuwa Taifa lolote lina Uimara wake na mapungu yake wakati wowote.

Cha msingi waambie kuwa Tanzania Chini Ya JK Kikwete Iko Imara na Watanzania inapofikia Kuungana kwa ajili ya Kuitetea nchi yao mara moja watafanya hivyo na mambo ya ndani yatasubiri hada adui wa nje ya nchi amenyooshwa na kuwekwa anapostahili!!-Hiyo ndio Tanzania inayojulikana na watanzania wenye akili na utu kamili.

Namalizia kwa Kuwatakia kila la heri Amiri Jeshi Mkuu, Wanajeshi wote wa Tanzania waliopo nje na Ndani Ya Taifa lao kwenye kutekeleza kazi zao na kuwataka Watanzania wote kutoyumbiswa na watu wachache waliomiogni mwetu lakini - maadui wakubwa. Tuungane kuwatambua na kuwafikisha panapotakiwa.
 
umetumwa na kagame utingishe kibiriti, kamwambie umefeli
 
Faizafoxy,this is not about parties.Its about a person who has failed to perfom.Period.Slaa katokea wap tena!?
 
Mkuu!
Usichanganye siasa na masuala ya ulinzi wa nchi.
Hayo mambo ya EPA,dawa za kulevya yako kisiasa zaidi,ambapo yote hayo
yamezunguzwa sana.
Logical ni bora watu wetu wakaangamia taratibu kwa tamaa zao za kutumia
dawa za kulevya,kuliko nchi kuvamiwa na watu kuuliwa hovyo hovyo kila mahali.
Ni vema tusiingilie kabisa masuala ya operations za kijeshi au kutumika kuwavunja
nguvu wapiganaji wetu kupitia siasa.

Tanzania ya leo inahitaji mtu mwenye maono na uelewa kama wewe. Chukulia vita ni kesho Kipi kitangulie kuzuubaa huku tukivutana na matatizo ya ndani ya nchi yanayotuteganisha au tuungane na kuwajibikia adui wa nje? Kwanza wapi tutapata fursa ya kuzozana kama tayari nchi iko vitani?

Mleta Uzi huu mfuatlie kwa karabu! Unafikiri anabahatisha? Na kama uko makini wako wengi sana kwa sasa. Wanapiga watanzania vita kuanzia ndani ili kuja kuunganisha na maadui watakao kuja mipakani.AMKA NA UGUNDUE KUWA WAMEJIADAA HIVYO MUDA MREFU!!WAKIFIKIRI TUMELALA!!!-

Ni wakati wa kuacha mambo ya kitoto na kusimamia Usalama Wa Taifa kwa pamoja -kwani bila hivyo hata usalama wa kujadilina kuhusu EPA nk utapatikana wapi?

Ukiaangalia kwa makini Hoja iliyotolewa hapa ni kuwanyogonyesha Watanzania, Amiri jeshi mkuu na Wanajeshi wetu na kutufanya Watanzania tupigike kwa urahisi kutokea mipakani. Nani mjinga haoni hilo!!!

Jambo la msingi kwa sasa ni kutoa maoni tuunaganike vipi kumkabili adui aliyeko mlagoni baada ya hapo tutakuwa huru na salama kurudi kwenye vijiwe vyetu na kuanza kuwajibishana ... Hatuhitaji Mtu wa kumtukana Rais wetu wala Jeshi letu kwa sasa! Madhaifu yetu tunayajua yote na hajaanza leo na tunajua muda na mahali pa kuyafanyia kazi. Si kushauriwa hivyo kwa na Adui aliyetangulizwa Tanzania akapewa ukarimu wa kusomshwa na kuchukuliwa kuwa Mtanzania halisi kumbe sio!!

Hatuhitaji ADUI anaye jifanya MTANZANI kutu-demoralize-kiana akijitia kutupa moyo na ushauri usio na mshiko. Huyu ni adui tu hata kama kwa sasa hayuko Rwanda. Nakuahkikishai soon ataungana na wezake kutugeuka. Na AKOME kwani hilo tunaliona na tuwashgulikia wao kwanza ....!!!-
 
Kusema kweli kuna walakini kwa Rais wetu, mpaka Kagame kamtukana hivyo ujue kaona udhaifu. Na hili si jambo dogo, embu fikiria Rais wetu ana rasilmali ardhi, watu zaidi ya 45ml, kodi inayokusanywa kubwa lakini anashindwa kucheza na hizo rasilmali, anakwenda kuchezewa na mtu ana raslimali kidogo sana! Kagame aliwahi sema mimi nikipewa bandari tu ya Dar naweza kulisha TZ, lakini yeye hata ile kumpongeza Mwakyembe hamna! Magufuli,hamna!. Mkapa alilipa deni lote huku akijenga barabara yeye kalirudisha 20trn sa sijui ndo zinajenga barabara! Anasikitisha sana!nchi haina hata shughuli za uzalishaji zinazoeleweka wala mpango wa kuwa nazo! utapigana vita na mauzo ya mazao tena ya wakulima maskini! na hana wasiwasi anacheka tu!

Kwa Watanzania, Tanzania ndio nchi yao hata kama Rais atakuwa ni nani! Na Kwa wakati mmoja Rais ni mmoja ni aliyeko madarakani. Hilo halina ubishi. Tumheshimu Amiri Jeshi Mkuu ...!!

Kwa kuwa Kagame amesema aliyosema sasa tumpe Tanzania? Sasa amemtukana Rais Wa Tanzania kwa hiyo Kagame tuendelee kumruhusu kwani Kagame hana mapungufu? Rais wa Tanzania ataacha kuwa Rais wa Tanzania kwa kuwa Kagame hamheshimu, huku Kagame pia akiwa na udhaifu lukuki?

Hatuwzi kuwa na Rais mwingine kwa Sasa. Kagame amuheshimu Rais wa Tanzania kwa kuwa Tanzania ni Nchi huru! Vingine Tutamuwajibisha bila kusita!!! Hilo liigie kichwani na moyo kwa udani. Kagame hajuii UTANZANIA NI NINI siri hiyo atuachie sisi wenyewe! Na atashangaa kuutambua UTANZANIA siku si nyingi!! Utanzania hauyumbishwi na EPA na vitu kama hivyo ... !!

Hakuna Rais aliyekamilika hata Kagame ana Uhuni na Upungufu wake .. nenda Kigali utatambua hilo mara moja. Tena anaweza hata kupinduliwa na watu wake hata kabla hajafikia kuendelea kuitusi Tanzania iliyomjenga na kumfanaya alivyo na kulea wakimbizi wa nchi yake. Tunajua anawawakilishi wa kutosha kuanzia hujuma kuanzania nadani ya nchi yetu ...

Nasema Yote uliyoandika hapa ni sahihi ..!!

Lakini SI HAKI WALA SIO SAHIHI KUYAFANYA YAMPE ADUI WA TAIFA LETU USHINDI!! Na kusema KWELI HATAUPATA!!

Pamoja na yote hayo Watanzania kamaili hawatapotoshwa na Makosa yetu, Udhaifu wetu au halinyingine yeyote ILI KUMFANIKISHIA ADUI ALIYETANGULIZWA NDANI YA NCHINI USHINDI!!
 
umetumwa na kagame utingishe kibiriti, kamwambie umefeli

Wako wengi!!

Utawaona hivi karibuni kama utitiri! Wengine ulikuwa nao kuanzia darasa la kwanza, sekondari, JKT, Chuo kikuu, Maofsini, CCP, Mgulani, kunduchi, Tabora .... utawaona ...

LAKINI!!

Wasubiri wajikusnaye ndipo watajuta kuifanyia mzaha Tanzania!!
 
Hamjaziona kesi za epa na watu kufungwa?

Hamuoni watu wa unga wanavyokamatwa kila siku?

Chuki zenu ni za kibinafsi na roho zanu zilivyombaya kila mnapoona mafanikio ya Kikwete nyie ndio mnazidi uhasidi. Mtaungulika sana, Kikwete ndio Rais na Mohamed Gharib Bilal ndio makamu wake.

Kweli wanakamwata kila siku,south africa,china,taiwan brazil kikwete anajitaidi sana watu hawaoni tuu.
 
Hamjaziona kesi za epa na watu kufungwa?

Hamuoni watu wa unga wanavyokamatwa kila siku?

Chuki zenu ni za kibinafsi na roho zanu zilivyombaya kila mnapoona mafanikio ya Kikwete nyie ndio mnazidi uhasidi. Mtaungulika sana, Kikwete ndio Rais na Mohamed Gharib Bilal ndio makamu wake.

wapi, kagoda?, wapi Deep green, ?
 
Hamjaziona kesi za epa na watu kufungwa?

Hamuoni watu wa unga wanavyokamatwa kila siku?

Chuki zenu ni za kibinafsi na roho zanu zilivyombaya kila mnapoona mafanikio ya Kikwete nyie ndio mnazidi uhasidi. Mtaungulika sana, Kikwete ndio Rais na Mohamed Gharib Bilal ndio makamu wake.

Huwa wanawakata Tz? Waache b'ness eti kuna watu wanashinikiza wakamatwe!! Jaribu kukamata b'ness ya mzee kama kibarua hakijaota nyasi; watoto wakose karo buree eti kuna watu wanaathirika. Rais anawajua eti ntawataja. Hivi kati ya Kamishina aliekabidhiwa majina juzi na Rais nani muajiri wa mwenzie? Then tafakari chukua hatua.
 
Huwa wanawakata Tz? Waache b'ness eti kuna watu wanashinikiza wakamatwe!! Jaribu kukamata b'ness ya mzee kama kibarua hakijaota nyasi; watoto wakose karo buree eti kuna watu wanaathirika. Rais anawajua eti ntawataja. Hivi kati ya Kamishina aliekabidhiwa majina juzi na Rais nani muajiri wa mwenzie? Then tafakari chukua hatua.

Hizo pumba zenu hazina mshiko. Uchawi ni maradhi mabaya sana, ukishaanza kuonja nyama ya mtu huiachi, hilo ndio tatizo kubwa la mtu kama wewe,
 
Kweli wanakamwata kila siku,south africa,china,taiwan brazil kikwete anajitaidi sana watu hawaoni tuu.

Na hii ni China?

Na Makongoro Oging'
MAMBO yameiva, Jumamosi iliyopita serikali ilitimiza ahadi ya kuwaonesha wabunge mkanda wa video wa mtandao haramu wa biashara ya madawa ya kulevya, ulio chini ya viongozi wa dini nchini.


Kufuatia mkanda huo, Uwazi lina habari kamili jinsi kikosi kazi cha kupambana na madawa ya kulevya chini ya Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi, Godfrey Nzowa, kilivyomnasa Askofu Mkuu wa Kanisa la...
Soma zaidi, source: ASKOFU ANAEUZA MADAWA AKAMATWA NA KUTAJWA ~ Hassbaby's (Mapacha)

 
Lini zamu yetu sisi madalali kwenda kula futari ikulu? HOPE NEXT YEAR
 
Back
Top Bottom