Amnesty International and Human Rights Watch: Hali ya ukandamizaji wa vyombo vya habari, watetezi wa haki za binadamu na vyama vya upinzani waongezeka

Babako angekuwa Kabendera au Mawazo au Gwanda ndio ungejua uchungu wa Wasiojulikana, kuwa kwako kwenye mirija ya utawala huu kusikufanye kuwa mpofu kwa mabaya yanayotendeka na watawala.

Wanachosema amnest ndicho ambacho wakosoaji wengi wanakipitia hivi sasa, Unazi wako na upenzi wako kwa utawala huu usikufanye kuwa kipofu kwa mabaya ambayo yanatendeka.

Leo kwa mwenzako ila kesho kwako, kumbuka "Kuimba kupokezana"
 
Wameamua kucheza na moto definitely lazima wataungua tu
 
@"besta mlagila,
Mkuu hatuna haja ya kuwapuuza wala Serikali isiharibu muda wake wa kazi kujibu wala kuongelea
 
@="kitonsa, ]
CHADEMA tunamtaka mjomba wetu Ben sanane nyie mnajua aliko Ila mmekuwa mkituaminisha ndugu zake heti serikali ndo inajua wakati nyie ndo wahusika namba moja. Taarifa zenu tunazo.
 
Hao watu Ni wapumbavu Sana Mkuu hatuna haja ya kuwapuuza Wala serikali isiharibu mda wake wa kazi kujibu Wala kuongelea hizi pumba..
Ya Zimbambwe yalianza hivi hivi watu walichekelea sana lakini vikwazo walivyowekewa wanasaga meno endeleeni kupuuza msifikiri hawaoni
 
@="Besta Mlagila,Mkuu

Ulisoma shule ya wapi? Ulitaka wahoji watu wote karibu million 60?

Sikua na haja ya kuendelea kusoma pointi hizo nyingine

Kwahili nadhani buku 7 umekosa.

Jaribu tena baadae
 
''The lion doesn't care about what the monkeys say about him, sitting up in the trees."
 
@="Besta Mlagila,

Nilipofika kwenye "serikali yetu makini" nikaacha kusoma maana partiality ishaondolewa
 
Habari wakuu,

Siku ya juzi kuna mashirika au taasisi hizo za kimataifa ziliinyoshea vidole Tanzania kuhusu haki za binadamu,uhuru wa kujieleza na Uhuru wa kisiasa.

Tangu habari hizi ziripotiwe kupitia mitandao ya kijamii na vyombo vya habari vya nje, huku Tanzania sijaona,sijasikia chombo chochote cha habari kikiripoti habari hii,au kuchambua habari hii kupitia mijadala.

Nimekaa na kujiuliza maswali yafuatayo:

1. Je, ni kweli vyombo vya ndani vimebanwa na mamlaka ndiyo maana hawawezi kuripoti habari kama hizi?

2. Je, huu ni uzalendo wa kutoripoti habari zinazoichafua Tanzania?

3. Je, kutoripotiwa habari hizi na vyombo vya ndani, hakuwezi kudhibitisha kuwa Tanzania hakuna Uhuru wa vyombo vya habari?

4. Hakuna mwandishi aliyefika kwenye mamlaka ya serikali kuhoji yaliyomo kwenye ripoti hiyo ili serikali itoe maoni ili mwandishi abalance stories?

5. Kwa nini vyombo vya habari vya Kenya vipo open sana kuliko vya Tanzania?
 
Viliona hali iliyopo ni tofauti na iliyo andikwa na hiyo Amnesty kwa sababu vinaiona hali.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…