Anachofanya Waziri Mkuu sio sawa, sio haki, sio Good Governance! Ni udhalilishaji na kuaibishana!


Kuna kitu nakiona hakiko sawa kwenye hii serikali.

But I just can't put my finger on it just yet.
 

Fyuuu Hivi Unaelewa Unachoandika Mkuu
 
Muda wa vikao haupo hapa kazi tu vikao ndo vimetufikisha hapo
 
Sasa wewe #Pasco ulitaka Waziri Mkuu atoe mfukoni bahasha ya kaki sio? Hivyo vijibahasha vya kaki mlivyovizoea sasa vimeota mbawa. #HapaKaziTu.
 
Kuna kitu nakiona hakiko sawa kwenye hii serikali.

But I just can't put my finger on it just yet.

Ngabu iko very clear hawana 'blue print' ya nini wafanye
kubadili hii nchi iondokane na kero
so wanashiriki ku expose kero na kukaripia on tv
lakini 'what to do to change things permanently' ndio hawajui...
'the blue print' ya ku replace hii failed system hawana
 

Ufatilii mambo kazi yako ni kudandia treni kwa mbele tu.

Mara ya kwanza alivyoenda bandarini alikuwa hana tatizo na bandari....bali alikuwa na ishu na TRA na data zilikuwa za mwezi june hadi novemba.

Leo ameenda kutoa data za mwezi june hadi octoba za mwaka 2014 na zinahusu bandari. Ishu ni kwamba data zinaonyesha makontena yamefika bandarini...ila bandari haina rekodi ya kupokea makontena hayo.

Hivyo unaweza kuona hizo ni cases mbili tofauti na kwa taasisi mbili tofauti.
 
Mkuu Pasco, kwa nchi hii hiyo good governance bado, bila mijeledi ya style ya PM hatuendi popote.
Ngoja waaibishwe ndipo chembe za uwoga na uwajibikaji zitakapojengeka miongoni mwetu
 
Last edited by a moderator:


S niliweka uzi kuuliza bandari imesafishwa nini na kina Mwakyembe na Sitta?
mkanijibu bandari iko safi tatizo liko TRA?
 
Ni kweli sio good governance, anauliza maswali mfululizo bila kutoa nafasi kwa upande wa pili kujibu.
 
NImeangali maoni ya wengi kati ya wale wanaopinga hatua zinazochukuliwa na serikali ya awamu ya tano, nimegundua kuwa watu hawa aidha wao wenyewe wameathirika na matukio hayo moja kwa moja, au ndugu/rafiki zao wa karibu ni wahanga wa matukio hayo. Mahali ambapo taasisi imeruhusu makontena 349 yatolewe bila kulipa ushuru, lugha nzuri ya kuto kudhalilishana hapo ilikuwa ni ipi. Mahali ambapo makontena zidi ya elfu mbili yametolewa bandalini bila kulipa ushuru, lugha tamu ya kuwafurahisha waliofanya hayo ilikuwa ni ipi. Tuache unafiki, hapa kuna upotevu wa kodi ya serikali, hakuna kuchekeana maana ukicheka na nyani utavuna mabua. Mtumishi wa serikali bila aibu anamiliki nyumba zaidi ya ishirini, ni kitu gani hicho, acha wafu wawazike wafu wao.
 
Weeewe! acha kusema hayo, ni 'dhambi'
Wabeba njuga na manyanga labda wasione bandiko lako, watakushukia kama mpinga mabadiliko

Unatakiwa kuimba. hapa ndima tu, hapa shughuli, hapa kazi, pale mapigo tu. Hutakiwi kuhoji ni kosa
Shauri yako!

Umekua mshabiki sana..nazani unasubili Magufuli ateleze Tu ufungue uzi kabisa ..uyatoe yako ya mayoni
 

Gombea basi urais usaidie taifa kwa kutumia hiyo blue print yako. Wewe kalisha tu kalio lako hapo na uache wanaume walio thubutu waongoze nchi. Wewe ambae hata kugombea ujumbe wa nyumba 10 huwezi unakuja kutueleza nini kuhusu taifa!? Bora hata Rungwe alithubutu kugombea urais, anaweza akaongea kitu tukamuelewa. Sio wewe coward.
 
Kwa nchi ilipofika sijui nani anaelewa huu wimbo wa utawala bora tena, kuna watanzania wameteseka sana na wamekata tamaa ya kuishi kwa maovu na unyonyaji mkubwa uliofanyika na wamekosa haki zao kwa visingizio vya process, sasa hutaeleweka kwa watanzania hawa wanaotaka kuona utu wao unarudishwa kwa gharama yoyote ile, nchi hii ni yetu sote na tuna haki ya kufaidi utajiri wa nchi yetu pia, kwanini wachache wajinufaushe wao halaf leo tuwaonee huruma wakat wao walikosa huruma? Mh. Majaliwa fanya hivyo kwa maslah ya wengi na sio wachache na nyie mnaotaka process na sijui utawala bora subirien kwanza kama tulivyowasubiria kwa mateso wakati mnakula nchi yetu
 
Pasco suala la kodi sio siri ni jambo ambalo wananchi tunapaswa kujua, kumbuka kuwa japo s kwa njia ya moja kwa moja lakini sisi ndio tuliyoipa ajira serikali kwa kura zetu na tukawapa watu wasimamie sasa kama watu waliopewa kazi ya kusimamia idara zao hawafanyi vizuri tunatakiwa tuwatambue kwa sura ili mwisho wa miaka mitano tufanye tathmini vizuri kama serikali inatufaa au haitufai.
Kumbuka hata ulivyokuwa shuleni mwanafunzi mtukutu alikuwa anaadhibiwa katika parade(mstarini) ile ni trick yaa kutoa warning kwa wengine kuwa jambo husika halikubaliki.
the same way to MKM anavyofanya
 
Mkuu Pasco, sasa na wewe hii siyo sawa kabisa, huu siyo utawala bora na wewe yaani unamsema PM mbele ya kadamnasi kwamba hajui uongozi? Sasa na wewe si ungempenyezea pembeni kuliko kuja kumwanika hapa JF? Ila nakubaliana na wewe kwamba PM hafanyi vizuri hivyo, lakini napingana na wewe kuja kumvua nguo hapa hadharani mpaka watoto wadogo wanamwona kwamba ni mvivu katika "modern management". Hawa jamaa waangalie wasije wakawa madikteta!!
 
Nasikitika kuona kumbe kuna watu bado wana element ya kubembelezana,nchi ni,yetu sote tushirikiane
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…